Mfano, Alikiba, Diamond, na wengine sasa, hawaitaji mainstream media kupush kazi zao, platforms zipo za kutosha wanazitumia ipasavyo.
Kukaa na bidhaa yako nyumbani ukisubiri watu wakupigie simu ni UZAMANI.
Don't underestimate nguvu ya mainstream media kwenye kushape society thoughts. Mainstream media (Radio, TV) ndiyo 'mass' media inayoifikia jamii kwa wepesi (gharama nafuu) na kwa haraka zaidi, unlike other media platforms (online/social media).
It all starts with 'mind setting'... na huwezi kuspark 'mind setting' pasipo kutumia kwanza mainstream media. Nitakupa mifano hai:
Je, ni watu wangapi kila siku watananua bundle/data za kuperuzi social media na YouTube? Jibu ni kwamba ni watu wachache, hasa hasa waliopo mijini tu, kwasababu ni gharama kuaccess social media & YouTube. Inataka mtu mwenye uwezo wa kununua smartphone kwanza, then awe na uwezo wa kununua data bundle. Pia inahitaji maeneo yenye internet coverage. Ndiyo maana unaenda sehemu vijijini huko ambako internet haishiki kabisa lakini Diamond wanamfahamu na yupo akilini mwao, kwanini? Kwasababu wana radio na mabanda ya video/tv yapo.
Kwa mazingira ya Africa, ambapo milo tu mitatu ya siku ni changamoto kwa walio wengi, mainstream media (TV and/or Radio) bado ndiyo njia kuu ya kuifikia jamii kwa wepesi. Hizo other media platforms are just 'alternative'.
Mtoto anazaliwa mpaka anakua anawasikia Diamond, Alikiba, Harmonize, Zuchu, kwenye radio au TV mara 20 kwa siku. Mtoto huyo akikua na kuajiriwa as radio presenter, unatarajia atapiga nyimbo za Nikki Mbishi? au mtoto huyo akikuwa na kuanza kuaccess YouTube, unatarajia atasearch amsikilize Nikki Mbishi? au mtoto huyo akikua na kuja kuwa miongoni mwa majaji kwenye Music Award Platform, unatarajia atampa tuzo Nikki Mbishi kwa wimbo bora?
Mkuu, sijuwi unanielewa? ama nije nimelewa?
So katika kushape mitazamo, mapokeo, na fikra za jamii, it all begin with mainstream media, kisha ndo hizo other media platforms hufuatia.
Social engineering in a global agenda package... Utasikia na kuangalia kile wanachotaka wao usikie na kuangalia, sio kile ukitakacho wewe. Yote hii ni through the Mainstream Media a.k.a mass media. Ndiyo maana sasahivi si ajabu tena kumkuta Baba, mkewe, watoto, mama mkwe, wote kwa pamoja wamekaa sitting room wanawatch video ya 'Nampa Papa' by Gigy Money. Au wanaangalia 'Nyege Nyegezi' by Diamond. Au wanasikiliza wimbo 'Mwagia ndani' by Maua Sama... vile vile Baba kavaa mlegezo (kata k) + kanyoa kiduku, na watoto wamenyoa viduku!
Why the social engineering? Go figure yoself...
Pamoja na obstacles zote hizo za kimedia, Maalim Nash amekuwa mbunifu kusambaza kazi zake kwa njia hizo ambazo wewe unaiita 'UZAMANI'... and so far the guy is doing good as per his fan base level. Binafsi nadhani, huyu mwamba anastahili pongezi sana.
Kwa taarifa yako, Nash MC yupo registered YouTube kitambo tu. Hebu isikilize video hii halafu ujiulize ni kwanini wimbo safi kama huu mainstream media haiupush kwa jamii?
-Kaveli-