Yaani kuna kitu huwa nashangaa sana utakuta humu mtu anasema vijana wanashinda kuzungumzia mpira hawalipambanii Taifa yaani mtu anaongea kama wenyewe sio Mtanzania, yaani anamlaumu wenzake wakati naye yupo hai anaona yanayoendelea nchini na hajafanya chochote sijui anataka nani ampambanie
Hao anaowalaumu hawajawahi kumuomba hata hela ya kula ila kila siku anaanzisha Uzi humu kuwalalamikia
Sasa nachojiuliza ukiona watu wapo bize na muziki au mpira kwani wanakupunguzia nini maana kama duniani ulikuja peke yako, shobo za nini?
Kila mtu abebe mzigo wake yaani umasikini wa mtu anakuja kulaumu watu wengine hii kali aise