Nashauri BASATA ipitie pia hizi movie zinazotafsiriwa na hawa maDJ wa mitaani, nyingine zinapotoshwa kimaudhui

Nashauri BASATA ipitie pia hizi movie zinazotafsiriwa na hawa maDJ wa mitaani, nyingine zinapotoshwa kimaudhui

WhoWeBe

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2022
Posts
2,299
Reaction score
4,282
Nimetoka kuangalia movie inayoitwa 'Tears of the sun' ya Bruce Willis iliyotafsiriwa na huyu DJ Mac wa Acheche Production, hakika tafsiri yake ya udini ameitia chumvi mno.

Yaani kila baada ya maneno matano sita, anataja ugomvi wa kidini kitu ambacho hata movie yenyewe haisemi hivyo; anaongopa yaani.

Maneno ya humo ni makali na yanayoweza kuchochea chuki kwelikweli ya kidini. Ikizingatiwa kuwa wapenzi wakubwa wa hizi movie zilizotafsiriwa ni watoto wanaohitaji kusikia upendo na wasiohitaji kusikia maneno ya kiuaji sababu ya dini.

Nashauri sasa BASATA iwe inapitia pia hizi movie kama inavyopitia nyimbo za kina ney wa mitego ili waweze kuzuia baadhi ya mambo yasiyo sahihi.

Nawasilisha.
 
Nimetoka kuangalia movie inayoitwa 'Tears of the sun' ya Bruce Willis iliyotafsiriwa na huyu DJ Mac wa Acheche Production, hakika tafsiri yake ya udini ameitia chumvi mno...
Kwanza hizo movies ni piracy?
 
kweli kabisa hata mimi naunga mkono.anayetafsiri ana kuwa comediani kwenye maelezo yake na watu wanafurahia kisicho cha kweli.unaposhusha hadhi ya muvi za wengine basi muvi za tanzania zitashuka ubora zaidi
 
Binadamu bwana!
Pewa wewe hio kazi ya kutafsiri kama utaweza!
 
Nilishakataa huu ujinga wa kuangalia movie iliyotafsiliwa,naonaga kama inashusha thamani yangu imagine unakuta umejenga nyumba nzuri umeweka samani za kisasa tv ya kisasa halafu eti unaenda kuchoma movie sijui za dj nani uje uangalie aghaaaa😂
 
Nilishakataa huu ujinga wa kuangalia movie iliyotafsiliwa,naonaga kama inashusha thamani yangu imagine unakuta umejenga nyumba nzuri umeweka samani za kisasa tv ya kisasa halafu eti unaenda kuchoma movie sijui za dj nani uje uangalie aghaaaa😂
haa noma sana
 
Nilishakataa huu ujinga wa kuangalia movie iliyotafsiliwa,naonaga kama inashusha thamani yangu imagine unakuta umejenga nyumba nzuri umeweka samani za kisasa tv ya kisasa halafu eti unaenda kuchoma movie sijui za dj nani uje uangalie aghaaaa[emoji23]
Ukiwa unasafiri kwenye mabasi ya mikoani huwezi kuzikwepa
 
Hiyo biashara imetajirisha sana watu.


Kuna kaka wa mwanangu mmoja alikuwa anafanya hiyo kazi .. amejenga majumba ya kutosha na dala dala kibao.

Kumtaja jina sio vizuri kwa sababu za kiusalama..

Ila kwenye movie alizo tafsiri yeye lazima utasikia uko nami ........... kutoka yombo kwa limboa
 
Mtoa mada umepuyanga, Kama tu kufuatilia miziki mibovu yenye kuamasisha ngono, mapenzi ya jinsia moja ubakaji na ulawiti imeshindwa, Hapo ndiyo itaweza "NCHI INALIWA NA WENYE NCHI"Basi nitongoze [emoji2][emoji2]
 
Nimetoka kuangalia movie inayoitwa 'Tears of the sun' ya Bruce Willis iliyotafsiriwa na huyu DJ Mac wa Acheche Production, hakika tafsiri yake ya udini ameitia chumvi mno.

Yaani kila baada ya maneno matano sita, anataja ugomvi wa kidini kitu ambacho hata movie yenyewe haisemi hivyo; anaongopa yaani.

Maneno ya humo ni makali na yanayoweza kuchochea chuki kwelikweli ya kidini. Ikizingatiwa kuwa wapenzi wakubwa wa hizi movie zilizotafsiriwa ni watoto wanaohitaji kusikia upendo na wasiohitaji kusikia maneno ya kiuaji sababu ya dini.

Nashauri sasa BASATA iwe inapitia pia hizi movie kama inavyopitia nyimbo za kina ney wa mitego ili waweze kuzuia baadhi ya mambo yasiyo sahihi.

Nawasilisha.
Picha Nzuri Sana na Haina udini wowote. Mtafsiri ni Feki [emoji35][emoji35]..
 
Back
Top Bottom