Nashauri: Kuongea Kiingereza kwa unyoofu (fluency) ibaki kuwa kigezo cha kumpima Mtanzania mwenye Degree

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Wasomi wengi hawawezi kuongea Kiingereza kwa unyoofu na kwa kujiamini.

Kuna msomi mmoja ilibidi nimuandikie barua ya kazi maana alikuwa anaenda kuabika kwa madudu aliyoandika. Ajabu ana 1.6 ya HGL na UpperSecond ya Sociology.

Naamini kama huwezi kujieleza kwa unyoofu na kwa lugha nyepesi kile unachokielewa basi wewe hukielewi na kama ulijifunza kwa Kiingereza tunataka ukieleze kwa uzuri kwa lugha hiyo.

Moja ya majuto yangu katika elimu ya juu, nikutojipa muda wa kutosha kujiendeleza kuongea na kuandika kiingereza kwa ufasaha. Niliashumu najua.

Nini maoni yako?
 
kwanini kisitumike kiswahili kwenye interview na iko kingereza kitume kwnye organization za kimataifa huko..
mtu anaenda kuajiliwa almashauri ambapo asilimia 90 atatumia kiswahili kwenye utendaji kazi wake ila interview inalazimishwa kufanywa kwa kiingereza tena kwnye nchi ambayo kiingereza sio mother tongue kama tumerogwa yaani.!
 
nadhani itabaki vivyo hivyo ๐Ÿ’

Kiswahili ni kigumu zaidi wa walumbi wa kufaulu watakua wachache sana ๐Ÿ’
 
Naunga mkono hoja!
 
Kiingereza ni lugha na si kipimo cha kuelewa mambo.
 
Kiswahili ni kigumu kuliko kingereza ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ ..Ngoja aanze kuandaa madokezi sabili hapo ndip utajua kiswahili ni nn.

Binafsi bora watumie kingereza ila kiswahili jau sana kina maneno magumu na ndio yanatumika ofisini.

English kina njiw nyingi rahsi kama ulikuwa hujui watu wanaweza kuandika kwa ms word then ikamsahihisha spelling mpaka grammar ,kuna tools kibao za AI .
 
Aiseeh! Kwahiyo nikifahamu kingereza tu nami najitapa nina degree.

Anayefahamu anifundishe please,Nitamlipa.l..ani PM .

"Godu morningi sa"
Mbwembwe zangu huwa zinaishia hapa,nataka nielewe zaidi ya hapa.
 
Shida ni pale mpimaji na mpimwaji wote ni walewale masalia ya Jiwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ