Nashauri kuwepo pia kwa Mkapa Day, ameifanyia hii nchi makubwa sana, isiwe mapumziko

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Tuna Nyerere Day kuenzi mambo makubwa aliyotufanyia Nyerere (legacy) kama vile Uhuru wa nchi yetu pamoja na umoja na mshikamano

Lakini Nyerere pia alikuwa na mapungufu makubwa yaliyopelekea nchi kuwa na hali mbaya sana kiuchumi

Mtu aliyechukua maamuzi yaliyofufua uchumi wetu ni Mkapa, mkapa aliupandisha uchumi wetu mara dufu na kupandisha pato ka taifa kwa mara tatu (three fold) kwa miaka kumi.

Sera zake za ubinafsishaji na uwekezaji japo zilikuwa na kasoro lakini zilileta manufaa makubwa sana kwa nchi
Makampuni makubwa kama CRDB, Vodacom, NMB, TBL pamoja na taasisi muhimu za kiuchumi kwa nchi kama TRA zote ni matunda ya sera za Mkapa

Yafaa tumpe siku yake japo sio ya mapumziko
 
Nashauri Nyerere Day ibaki kama ilivyo,na kila mwaka iwepo Theme ya kumkumbuka kiongozi mwingine wa kitaifa kama vile Mkapa au yeyote yule aliyetoa Mchango mkubwa katika ujenzi wa Nchi..na si lazima awe RAIS tuu...kuna ata mawaziri ambao hawajapata bahati ya kupata nafasi kubwa but michango yao imetukuka...
HAPO VIPI!?
Nimesema isiwe ya mapumz
 
Huyo alikuwa Baba wa Mageuzi!
Kiongozi aliyeleta mabadiliko ya msingi everlasting Hero!
 
hakuna kupongeza mtu aliyefanya majukumu yake,na wewe tukuandalie siku yako kwa kumlipia mwanao ada
 
Uwe u afuatilia mambo kwa kina,TRA ilianzishwa na mwezi julai 1995,crdb ilikuwepo,nmb ilitokana na kuuzwa NBC kwa Bei ya kutupa Kisha waliouziwa wakampa mkapa mkopo wa 100m mwaka 1997,mkapa angeingia baada ya kutoka nyerere asingefanya hayo,mwinyi kwa miaka kumi aliiandaa mazingira ya uchumi huria
 
Kwenye movie sterling huwa ni mmoja tu.Hao wengine wabaki kuwa wanogesha sinema.
 
Baba wa taifa anatosha, tutakuwa na siku nyingi za mapumziko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…