#COVID19 Nashauri Serikali iandae mdahalo mubashara wa Television baina ya Askofu Gwajima na Waziri wa Afya ili kumaliza utata uliopo juu ya usalama wa chanjo

Update: 26/08/2021

Mliochoma Chanjo ya Johnson & Johnson mmesikia matokea ya utafiti huu mpya juu ya waliochanjwa ? 😂😂😂

 
Tunahitaji majibu ya hizo hoja, vinginevyo muache kelele za chanjo
 
Ndugu yangu kanishangaza sana, wiki mbili zilizopita alikuwa ananisomea makala moja nzuri sana iliyoandikwa na Mh. Askofu Gwajima (mb). Kuhusu chanjo ya Covid 19, na alionekana kuielewa vizuri sana ile makala na kunishawishi nikubaliane nayo nisichanje kabisa ili kuilinda afya yangu.

Siku chache zilizopita nikapata clip ikimuonyesha huyo ndugu yangu akiwa amelazwa anapumlia kwenye mtungi wa Oxygen. Sikuiamini hiyo clip na wala sikutaka kuuliza maana niliamini anaigiza tu.

Juzi nimekutana naye mbashara, mikamuuliza kulikoni ile clip, ndipo akanitolea simu yake na kunionyesha picha zake kuanzia alipofikishwa emergency hadi ICU.

Akanipa stori za kutisha juu ya watu aliowashuhudia wakikata roho pembeni yake huko ICU kutokana na kuugua uviko19.

Mwisho akaniambia wahi ukapewe chanjo ili ujikinge na makali ya Covid19. Nikamuuliza kuhusu makala akanijibu kwa kujiamini "achana na huo upuuzi wewe wahi chanjo."

Mpaka hapo nikabaki mdomo wazi.

Ninachojua mimi hii chanjo iwepo tu atakayeguswa afanye akili zikavyomtuma. Gwajima (Askofu) anayo haki ya kuwalinda kondoo wake na serikali ina haki ya kuwalinda raia wake. Chagua uwe kondoo au raia.

Alamsiki!.
 
Hakuna anaebisha kuhusu hii story, ILA, tunaomba majibu ya hizo hoja hapo juu
 
Mimi nimechanja, kwahiyo nitapata madhara lini ?

🤸🤸😂😂
 
Mimi nimechanja, kwahiyo nitapata madhara lini ?

🤸🤸😂😂
Hakuna anayejua, hilo ndilo tatizo, kwa muda mfupi, (chini ya miaka mi5), kwa muda wa kati (miaka mi5) na kwa muda mrefu (miaka 10)
 
Hakuna anayejua, hilo ndilo tatizo, kwa muda mfupi, (chini ya miaka mi5), kwa muda wa kati (miaka mi5) na kwa muda mrefu (miaka 10)
Hivi unajua chanjo zinatengenezwaje kweli ??

Mkuu, tafuta pesa hao YouTubers wanapiga pesa off Adsense, Admod na AM kwa ku-upload ujinga ujinga kama huo.

Kama kweli una nia ya kujifunza, tafuta credible sources. Achana na kuokoteza okoteza kila kivideo unachokutana nacho YouTube.

YouTube ni jalala ambalo hata Gwajima ambaye hana background yoyote ya mambo ya Afya anaweza kiweka video anaelezea vitu ambavyo havijui wala hana experience navyo.
 
Sawa, na vipi kuhusu hizo hoja nilizoainisha, ni lini mtatupa majibu yake?
 
Gwajima ni mwanasayansi ?
 
Sawa, na vipi kuhusu hizo hoja nilizoainisha, ni lini mtatupa majibu yake?
Hakuna hoja ya maana yoyote uliyoainisha hapo.

Ndio maana nimekwambia kama una nia ya kujifunza, chukua muda ujifunze maana naona umeweka juhudi kwenye kubishana huku ukijifanya unataka kujua.

Na kibaya unasikiliza mtu yeyote ambaye hajui chochote kuhusu anachozungumza.

Ndio maana mimi wala silaumu watu kama kina Gwajima au Magufuli.

Wewe unaemsikiliza mtu ambayr unajua kabisa hana background yoyote ya masuala ya Afya, tiba na chanjo ndio Taahira.
 
Kweli zinaweza zisiwe na maana, lakini upuuzi wa hizo hoja utadhihirika kwa kujibiwa tu, mi nadhani hizo hoja zijibiwe kwanza
 
Unaweza kutwambia kwanza wewe ni nini madhara ya bia au KVANT mtakayopata baada ya miaka elfu ijayo ?

Au madhara ya unga wa mashineni mnaopikia ugali baada ya miaka 50 ijayo, maana yale meno ya kusagia huwa yanaisha ?
2.) Je, chanjo ni nini? , yaani ili kitu kiitwe ‘chanjo’ kinatakiwa kiweze kufanya nini na nini? , na kwamba je, hicho kinachoitwa chanjo, kinaweza kufanya hayo?
Unataka definition ?

Huu muda unaoutumia kutafuta video za kijinga jinga na articles za kijinga mtandaoni unashindwa nini kutafuta maana ya chanjo ni nini ?
Kirusi kinanadilika kama kikiachwa active ndani ya HOST. Ndio maana leo unaweza kumeza dawa za ALU zikamaliza maralia ila ikitokea ukaanza kuharibu dose, wale plasmodium wa Malaria wanatengeneza drug resistance kiasi kwamba huwezo kuwaua tena kwa ALU.

Muhimu ni kudhibiti mapema ili kuepusha virusi visijiimarishe zaidi maana huwezi jua itakuwaje huko mbele.

Kwa kawaida virus havijawahi kutibika. The only solution ya rahisi ni chanjo.
Kama ikitokea zaidi ya 96% ya watu wamechanja, hakuna sababu ya kuvaa barakoa. Otherwise tahadhari ni muhimu.

The same applies kwa watu wa UKIMWI, mwathirika wa UKIMWI akianza kumeza ARV virusi vinakuwa dormant kabisa na viral load yake inakuwa vizuri tu. Ila akianza kuvuruga tena akakutana na virusi kutoka kwa mtu mwingine inakuwa ni hatari zaidi kwake.
5.) Nk, Nk, Nk, Nk.
Hii nayo ni HOJA ???

Anyway, internet ni JALALA unaweza kuchagua chochote unachoona kinakufurahisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…