Nashukuru Mungu nimeacha uhuni

nzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,106
Reaction score
12,916
Hii ni kutokana na kuokoka siku kadhaa nyuma.

Kumbe wokovu ni mchakato, si kwamba ukiokoka leo basi leo leo vitendo, kauli, na fikra zinabadilika kwa ghafla. La hasha! Ni mchakato taratibu huku neema ya Mwenyezi Mungu ikikuongoza katika mabadiliko hayo kutoka giza kuelekea nuru.

Nimepunguza matusi, hii ni pamoja na kutenda na kunena. Kauli sasa ni njema; matusi zimepita siku kadhaa hayajanitoka kinywani.

Tena, kupiga kipara misambwanda zimepita siku kadhaa. Pombe na fegi nimeshasahau.

Bangi ndo kabisa sijalipuliza.

Hata nyimbo za kihuni hazina nafasi sasa; nasikiliza nyimbo za kuabudu.


View: https://youtu.be/W5nDAeEWvM0?si=UJe2wiAMk75GZk9n
 
Mungu akubariki. Endelea kumpenda Yesu. Soma neno lake yaani Biblia. usiache kwenda kanisani. zaidi sana endelea kumwomba Mungu akusaidie maana shetani yupo siku zote akitafuta wale waliomkimbia ili awarudishe kwenye utumwa wake.
 
Nimecheka Sana yaani unasema umeacha uhuni na sijaona Kama uliwahi fumaniwa na mke wa mtu .

Haujawahi kupigwa viboko na serikali ya Kijiji kwa kuendekeza chabo kwenye madirisha ya watu .

Yaani nakuambia umeacha tutabia twako mapema Sana ila usiseme ulikuwa muhuni
 
Sijaona uhuni wowote hapo mzee.

Hv ulishakula madem watatu kwa mpigo huku unawa-YAS? Ulishatongoza mama mchungaji na kumuonjesha forbidden fruit? Ngoja niishie hapo
 
Wokovu ni safari ndefu sana utayaona makubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…