Nashukuru nimeanza Mwaka 2025 vizuri bila makandokando

Nashukuru nimeanza Mwaka 2025 vizuri bila makandokando

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Leo asubuhi niliacha simu imezagaa zagaa bila kuifunga. Niliporudi nikakuta Afisa Upelelezi anaifanyia upekuzi wa kina bila kibali. Ikabidi nimtazame machoni kiwiziwizi kuona kama kuna chozi linalenga lenga. Sikuona chozi ila nikaona ni kama mtu anayevuta kumbukumbu fulani. Ikabidi nitoke nje kupanga mbinu ikiwa nitadakwa na kashfa yeyote basi nije na uongo gani. Lakini pia kukumbuka kama kuna sms nilisahau kufuta maana huu uchunguzi umekuja ghafla.

Baada ya muda nikaona ameendelea na mambo mengine. Nikajua hapa kuna amani, nikarudi. Akaniambia "Bahati yako leo, ila nitakukamata tu! Simu yako ile pale"

Daah nashukuru nimeanza mwaka kwa bashasha bila makandokando. Kwa hiyo nimeanza mwaka na kafeeling fulani kapekuliwa simu halafu usikutwe na umalaya wowote.
Aidha safari hii shetani amezembea kuniharibia amani.

Heri ya Mwaka Mpya Wakuu
 
Aisee kumbe tumekoswa koswa wengi , jana saa saba usiku namba ngeni inaingia nikasema hii sipokei nikajidai kama nimelala ghafla nasikia ,

Mbona hupokei simu na ni nani huyo nikasema wololooo yaeeee,
Nikapokea huku naona mwaka umeingia vibaya huu hapo Tiss wangu sikio limemsimama kupokea kumbe dogo mmoja tu hivi ananitakia heri ya mwaka mpya 🤣🤣 , cha ajabu Tiss wangu hapo hapo usingizi ukamrudia ghafla na kukoroma juu
 
Uzinzi hauwezi kumalizwa kama nimwanaume kamili
Wakubali ukwel tu
 
Shida ya wanawake wanadhani wanaweza kumthibiti mwanaume dhidi ya ngono
Hizo nguvu wanazotumia kumzuia mwanaume asifanye ngono na yeyote isipokuwa yeye bora angetafuta namna ya kumridhisha mwanaume kingino.
Maana maana mpaka dunia inaanza na itakapo kamilika mwanaume hatatosheka na mwanamke mmoja maisha yake yote.
 
Back
Top Bottom