Tetesi: Nasikia Panya road wako Mbagala Zakheem

Tetesi: Nasikia Panya road wako Mbagala Zakheem

Kwa taarifa yako sasa,juzi aliuwawa mmoja wa hao panya road,jana mchana wakati anazikwa wakaja field force gari si chini ya4,vijana wakakimbia,wakakamatwa baadhi,na maiti police wakasaidia kuzika..

Jana hiyo hiyo Usiku hao vijana wakajiorganize tena wakawa wanapita mitaani kulipiza mwenzao kuuwawa ..

Ila kuna baadhi wametiwa mbaroni...
Over and out mkuu....

Copy that
 
Imefikia hatua hata ugomvi wa vijana mtaani wakigombea demu ukitokea mnasema Panya Road acheni kutia watu hofu
Mkuu huo ndio kweli,yani hata ukimpiga mkeo tu utasikia panya road wamempiga Mdada
 
tumechoka na kelele zenu, nawashauri kila mwanaume mtaani anunue moja ya hizi nyenzo pamoja na firimbi.
Wakija hao watoto piga firimbi kila mtu atoke na shoka au panga lake. Ni kukata na kufunua tu hakuna kuchukua mateka.

images (1).jpeg


images.jpeg
 
Kuna kipindi hizi Panya Road zilisumbua, mpaka wakati mwingine hata kama ni uongo watu wanakimbia na kufunga maduka
 
Mkuu hawa panya usiseme hivo, ni zaidi ya tatizo! Kuna mdogoangu nae ni kijana wa hovyo, anaishi kwa mama sio mbali na nyumbani kwangu siku moja amekuja kwangu usiku akanigongea vzr tu akaingia tukawa tunaongea lakini akaniambia yuko na wenzake wachake wapo nyuma ya nyumba wamekaa kwamba nisiwe na wasi, akatoka kwenda kukaa nao'

Nikawa nasikia sauti chache za chinichini, nikakadiria labda kuna watu hawazidi 6, nilivotoka nusu nizimie! Nilikuta kuna watu kama 30 na zaidi! Na huwezi amini hakuna hata moja ninaemjua zaidi ya huyo dogo tu!

Na kila muda anatoka mmoja akirudi anakuja na wengine tena! Mpaka wanaondoka pale mida ya saa sita usiku wameshakuwa wengi mnooo!

Dogo akawa ananitambulisha' nikagundua wantokea kiwalani, mbagala, wengine bunju nk.
Kesho yake nikasikia tukio la ajabu!

Wale madogo ukiwa unaongeanao ni wana heshima saana! Na wako wazi hawafichi kitu.

Ila wakati wanaondoka niliwaambia pale wasije tena. Wakasema "heshima kwako bro popote tukikuona tutakulinda"

Kuwazibiti panya inatakiwa weledi tofauti kbs na hizi operation za polisi.
Kuwa makini huyo dg usikubar akuletee wauni itakucost trust me utakuja jikuta nyuma ya nondo
 
Watoto wadogo wanaleta fujo. Wakipata bastola wataleta fujo zaidi? Siyo kweli. Wanapofanya hii light trouble ndio wanavumiliwa.
Hata hivyo,inaleta wasiwasi Hawa vijana wengi wanavyokamatwa na Polisi.
Kwamba ile fujo inaonekana dhahiri inafanywa na watoto kutokana na madhara madogo yanayotokea.
Na Polisi wanaonekana hawana interest sana. Yule Mama mmoja anasema,"tuliwaita Polisi,Polisi wakafika wamelewa chakari'
 
fake story msitoe taarifa za uongo itukapojulikana unatoa taarifa za uongo mtashughulikiwa kwa mujibu wa sheria acheni kutisha watu na kutoa taarifa ovyo wewe ukikamatwa utahesabika panya road
 
Back
Top Bottom