Nasra Mohamed: Ukatili na unyanyasaji uliovuka mipaka!

Nasra Mohamed: Ukatili na unyanyasaji uliovuka mipaka!

Ila mkuu labda kwa upande mwingine, nadhani tunatofautiana pale ambapo unajaribu kuonesha kuwa Nasra ambaye tayari alishakuwa victim, may be ndiye alitakiwa kujitafutia msaada wa kisaikolojia. Kumbuka, wakati huo tayari alishakuwa psychologically compromised. Kama ni kweli, basi mume na ndugu ambao walimwona mtu anabadilika sana kutoka kwenye hali yake ya kawaida na hawakuchukua hatua wanabeba shea kubwa ya lawama!!

Babu DC!!

Anhaa hiyo ndio point yako...!!
Labda kama tunaupungufu wa taarifa katika hii hadithi, ila kwa jinsi ulivyoeleza ni kuwa Mwanaume alirudi na kuwa mpole ndio "dada yetu" akapamba moto.....
Silengi kutetea upande wowote, au kuhalalisha kwa upande wowote ndio maana kama utakumbuka ulipoleta hii stori mwanzoni tu nilimlaani huyo "Kaka" kuwa "nyumba ndogo imefanya mambo"....
Leo baada ya kupata upande wa pili wa hadithi nimejaribu kutoa mawazo ya jumla kuwa katika nyumba kwa mujibu wa maandishi ya kidini yangu (japo kwa ufinyu) Mwanamke ana nafasi ya pekee sana katika kusimamia nyumba yake na familia....
Pamoja na u-victim wa dada Nasra ila tatizo rasmi limeanzia pale alipojaribu kulipiza kisasi, na yeye akatengeneza Victim mwingine "mumewe"... Sasa tukitaka kujenga hoja za nani ni Victim na alistahili nini basi wote ni victim!

Ndio maana nikaona kuwa turudi kwenye msahafu sahihi wa maisha (inaweza kuwa dini au asili yetu waafrika).....

  • Nini majukumu ya wanawake kwenye familia na nafasi zao?
  • Nini majukumu ya wanaume kwenye familia na nafasi zao?

NB: Tatizo limeshatokea, kujenga hoja kwamba nani ana makosa au nani alionewa inaweza isiwe na utamu sana Babu, tusaidiane kuelimishana namna bora katika ujenzi wa familia kama enzi zenu za miaka ya 47....

Bado naamini katika nafasi ya pekee ya Mama zetu katika kujenga Familia yenye furaha sana!
 
Mie siku zote huwa naamini mwanamke aliyeko kwenye ndoa anajiheshimu, anamuheshimu mumewe, anawaheshimu ndugu wa mume na wake pia, ukikuta mwanamke kabadilika mara nyingi chanzo ni mume wake, wanaume wanachangia kwa asilimia nyingi kubadilisha tabia za wake zao,


matatizo yanapotokea ndani ya ndoa sio wote wanaweza kuyamaliza kwa njia za busara babu DC, angalia mf. wa Nasra, kamfumania mumewe na njia pekee aliyoona itamwondolea machungu yake ni kulipa kisasi kwa kuwa na mwanaume mwingine, simlaumu manake hapo ndipo akili na maarifa yake yalipoishia. Mwingine labda angeamua kulewa wakati hapo kabla hakuwahi kutumia kilevi chochote, mwingine labda wangekaa wayazungumze then wasameheane na maisha yasonge... Hapa pia inabidi kumpata mume wa Nasra na kumuuliza ni kwanini aliamua kutoka nje ya ndoa yake... Usishangae pia akikwambia chanzo ni mke wake..

Babu DC ndoa zina siri nyingi usione milango na madirisha ukafikiri kuna amani sana!


Nasra alimkosea heshima mumewe, ila pia hakustahili kufanyiwa ukatili wa namna ile...ndoa ni ngumu babu DC, mie hata nashindwa nimtete yupi...

HIVI ULISHAJARIBU PIA KUJIULIZA SABABU ILOMFANYA HUYO MWANAUME ATOKE NJE YA NDOA, USIKIMBILIE KUTETEA JINSIA TU.. WANAWAKE wengine ndani ya nyumba wanamadhila hadi hupelekea mme kutafuta relief elsewhere unajuaje kama huyo nasra alikuwa ampalii huyo jamaa wakati wako ndoani!!?? Ishaonekana mwanaume ni mkimya sio varuvaru kama huyo nasra huoni hilo lilimfanya areact kimyakimya kwa kutafuta ahueni nje huko???
USILAZIMISHE CHANZO NI KUFUMANIWA KWA JAMAA.. JE WAJUA NINI KILIMPELEKEA AKAENDA NJE????
 
Jamani kwa kusoma tu hapo huyo mwanaume alikuwa mzembe na hamjui mke wake vizuri! ushauri wangu kwenu wanaume mnaojali ndoa! mpaka hapo walipofika huyo mwanaume adhabu ambayo alistahili kumpa mkewe ni kumvuta hadi guest ya karibu hapo yangeishia kwenye sita kwa sita! yes kama aliweza kumvuta police asingeshindwa hilo! nasema hivi kwa sababu huyu mwanamke alikuwa anampenda sana mume wake yote aliyofanya zilikuwa ni hasira za kulipiza kisasi ila akifanyeje ndo alifanya kila lililokuwa linakuja kichwani mwake!

kumbuka wamesema ilikuwa couple ya kuigwa so mwanamke alikuwa na imani kubwa juu ya mumewe! na hofu yangu huyu kaka hata huyo mwanamke alimuopoa ktk mazingira ya kuzoeana kupita kiasi na bidada akawa na nia ya kumnasa mana alikikwa mpole sasa yeye baada ya kufumwa akawa anajutia kimyakimya! kama aliomba yaishe alipaswa kuendelea hivo hata baada ya huyo mwanamke kufanya kosa mana yeye si mkosaji bwana! sasa upole wa kutoongea hausaidii wanawake vile hatakupiga hatuwezi tunaanza na kununa! kisha kuongea mpaka dukuduku liishe! kisha vitendo kama unaona ujumbe haufiki it just comes automatically! sasa kwenye vitendo itategemea na ukubwa wa kosa. na kila mtu anavoweza kubeba maumivu yake! Mwanamke alikosea lakini kuuwa!? hata nyie wanaume hapa mnaosema alikwa wapi siku zote kuua iwe mnajifurahisha hapa haya si maneno ya kuongea hata mbele za watu! mtu anaetaja kuuwa kama.ni sawa ni mtu wa kumuangalia mara mbili!

Huyu kaka hakuwa akichukua atua za kurudisha mapenzi yao mwanamke hasira zilikuwa zinaongezekasiku hadi siku na kuona hakuwai kupendwa this is just sycologically ukweli kwamba matusi yalizidi ni sawa lakini wanaume msiitaji phd kumjua mwanamke kuweni watu wa kubembeleza hatuna uwezo wa kuwapiga so mkituudhi tunatafuta matusi ya uzani wa makosa yenu! ikibidi nikwambie mtoto si wako! joka la kibisa! sasa hapo it depends with one's education and background! binafsi siwezi fanya in public kulinda status yangu lakini i know ambavyo huwa nachukia na saingine nisipoyatoa mdomoni hasi kimoyomoyo lol. . mapenzi yakirudi hata hukumbuki hivo vitu we need to be loved bwanaaa. .
 
Kitu mura mbuya saguru ghati! haya kina mwita chacha,wankuru,ni mambo gani haya mnafanya?

Unajua umerukia treni kwa mbele wakazi wa bunda siyo wakurya, ni wazanaki na wasweta, wakurya wapo tarime msipende kuwabeza hawa jamaa watakuja kuwazalisha ohoooo
 
HIVI ULISHAJARIBU PIA KUJIULIZA SABABU ILOMFANYA HUYO MWANAUME ATOKE NJE YA NDOA, USIKIMBILIE KUTETEA JINSIA TU.. WANAWAKE wengine ndani ya nyumba wanamadhila hadi hupelekea mme kutafuta relief elsewhere unajuaje kama huyo nasra alikuwa ampalii huyo jamaa wakati wako ndoani!!?? Ishaonekana mwanaume ni mkimya sio varuvaru kama huyo nasra huoni hilo lilimfanya areact kimyakimya kwa kutafuta ahueni nje huko???
USILAZIMISHE CHANZO NI KUFUMANIWA KWA JAMAA.. JE WAJUA NINI KILIMPELEKEA AKAENDA NJE????
Soma tena hiyo quote yangu paragrafu ya pili mstari wa mwisho....

Humalizi kusoma unakurupuka kujibu!
 
Sijasema hivyo sl...
Naamini kulikuwa na njia bora zaidi kuliko kulipa kisasi...
Ila pia naamini unakubali kuwa "Mwanamke mwerevu huijenga nyumba yake na mpumbavu huivunja"

Hapa tunaenda pamoja jG, ni kweli Nasra hakutumia njia bora kumaliza tatizo lake!...

Najiuliza hakupata hata ndugu/ rafiki wa karibu akampa japo ushauri ambao ungemsaidia asifike huko?
 
Ni kweli ila kutokufikiria huko kulisababishwa na nini? Mume aathiriwe na nini wakati yeye ndie kafumaniwa?... Hapa wote wawili walikosa busara, ila ukumbuke mioyo yetu ni tofauti yaezekana Nasra alishindwa kulipokea tatizo na kujipa muda wa kufikiri,..amini nakwambia alichokuwa anakifanya Nasra ni kujipooza maumivu alokuwa nayo...

kama mume kakosea kwa bahat au kwa kukusudia atakuwa mkosefu je afanyae kwa kumuumiza mwenzie kusud atakuwa na dhamira. yawezekan mume alivumilga na yamefika pomon
 
Mapenzi, mapenzi, mapenzi. NI utoto ufanywao na watu wazima, ni uendawazimu, ni aina mojawapo ya ukichaa. Naam, ni ujinga tu tunaouendekeza. Kwa kweli sijui nimlaumu nani. Lakini iwe itakavyokuwa NAsra ana kosa la "provocation" na anastahili adhabu aliyopatiwa.Bazazi ni Bazazi!
 
Maamuzi ya Kuua hayapaswi kufanywa na binaadamu yeyote yule hata mwenzio awe amekukosea vipi. Huyo bwana alikosea tu hamna kitu kitakachomsafisha kwa kitendo alichofanya.

nimeipenda picha yako na jina lako safi sana ila unatakiwa uendane nalo,sidhani mwanaume ni wakulaumiwa kwasababukama sikosei kwenye sura moja ya quraaan tukufu ya ASHUURA..INASEMA HIVI.k
ama mtu amedhulumiwa na akaamua kulipiza kisasasi asilaumiwe aliyelipiza kisasi bali alaumiwe aliyedhulumu,ila mwenye kusubiri ujira wake upo kwa mungu na subira ni jambo kubwa sana
kama nimekosea si vibaya ukanisahihisha
 
Hebu basi tupe misingi ya kisheria basi...Kwa nini unadhani kesi inaweza kutupwa na DPP (Nolle presequi)?

Mbona aliodoka sehemu ya tukio, halafu akarudi tena? Hii haiwezi kujenga mazingira kwamba alienda pembeni akakaa na kupanga kitu cha kufanya?

Hapa itabidi niwatafute maloya (lawyers) wanipe mwanga kidogo!!

Babu DC

tuongee ukweli, heat of passion hapo bado ilikuwa haijaisha. huwezi jua ni kwanini aliondoka na kurudi pale stand, labda kuna kitu cha muhimu alikuwa ameenda kukifanya pale au alikuwa anakifanya pale, hivyo alivyoondoka, alifikiri labda mwanamke yule atakuwa ameshaondoka. kutembea na mwanaume mwingine hiyo haikumuumiza sana....ila kitendo cha mwanamke kumtukana mwanaume stand kwamba hana nguvu za kiume, na kwamba hata watoto wale si wake ni wa mwanaume mwingine aliyemsaidia, maneno hayo ni wazi kwamba hayakuondoka mapema kichwani mwa mwanaume yule, nafikiri yalikaa katikati ya ubongo wake hata zaidi ya wiki au miezi. sasa kitendo cha yeye kuondoka, naweza sema kuwa alitaka kuepusha shari kama alivyokuwa amezoea kuepusha shari kipindi cha nyuma alipokuwa akiletewa mwanaume na kufuatwafutwa hata bar na mwanaume na mkewe. nafikiri alikuwa anaondoka pale stand alipokuwa amevuliwa nguo kuepusha shari.

alipofika mbali, aliamua kudrive kurudi, labda kuja kumzuia yule mwanamke asiendelee kumchafua pale stand, kwasababu huwezi jua, alipoondoka yeye aliendelea kurap yoyoo you know what i am saying.... pale stand kumwanika ex wake. ningesema mwanaume alirudi pia ili kumwondoa mwanamke pale kwa amani ili wakayaongee nyumbani, lakini ghafla, ALIPOMWITA NA KUMWONA YULE MWANAMKE ANAKUJA, GHAFLA KICHWANI MWAKE ALIYAKUMBUKA YALE MATUSI, HANA NGUVU ZA KIUME, WATOTO ALISAIDIWA, AMEANIKWA HIVYO STAND, hasira kubwa sana ikamjia kichwani kwake, akajikuta ameamua kumshambulia kwa kumgonga na gari.

jambo hilo hatuwezi kusema ya kuwa alilipanga kabla. wasnt pre-meditated kabisa. pia, maneno hayo ni makali sana, katika jamii yeyote ile yanaweza kuamsha hasira kali kufanya tukio lisilo la kawaida. pia, heat of passion ilitulia alipoondoka, lakini aliporudi na kuwita mwanamke aje kwenye gari, alipomwona, kukumbuka tu yale maneno hasira ilimjia tena ghafla akafanya alichokifanya.

hata jaji mwenyewe atakayesikiliza kesi hii, akifanyiwa kitendo kama hicho, atafanya jambo kubwa kuliko hili alilofanya uyo mwanaume. any ordinary person katika jamii akikutana na jambo hili, atafanya kitu kikubwa.

historia inayonesha kuwa, huyu jamaa alikuwa na uvumulivu sana, alishavumilia sana kuletewa wanaume na huyu mwanamke, siku zote alivumilia, lakini jambo alilokutana nalo mwishoni pale stand lilikuwa juu ya uwezo wake. what do you think would be a reasonable time for the heat of passion to cook kwa maneno kama yale? hata kama principle ni kwamba alitakiwa awe amefanya tukio kubwa wakati uleule wa maneno makali kabla hajaondoka, lakini kwa any ordinary person hakika kichwa chake kilikuwa hakijatulia kwa muda mrefu kuliko....

NB; nimejitahidi kuongea kama layman, lakini kusema ukweli, ni nusu kwa nusu, si rahisi sana kutumia defence hii ya provocation, pamoja na kwamba inawezekana, na labda yeye ataanzisha principle mpya kupitia kesi yake (kulingana na kesi nyingi zilizopita, heat of passion hapa ilikuwa imeshatulia pale alipoondoka) lakini kila kesi huamuliwa kulingana na facts zake. kitendo chake cha uvumilivu kabla, na ukali wa maneno yale (pengine aliwapenda sana wale watoto, walikuwa moyoni mwake, pengine pia aliamua kuoa mwanamke mwingine ambaye alikuwa hajazaa na hivyo angesikia kuwa hana nguvu basi tena, pengine kuna watu wengi wanamfahamu pale na yeye alianikwa kuwa hana nguvu na watoto alisaidia...hakika hapa anastahili provocation kama mimi ningekuwa jaji)....ciao.
 
Mie siku zote huwa naamini mwanamke aliyeko kwenye ndoa anajiheshimu, anamuheshimu mumewe, anawaheshimu ndugu wa mume na wake pia, ukikuta mwanamke kabadilika mara nyingi chanzo ni mume wake, wanaume wanachangia kwa asilimia nyingi kubadilisha tabia za wake zao,


matatizo yanapotokea ndani ya ndoa sio wote wanaweza kuyamaliza kwa njia za busara babu DC, angalia mf. wa Nasra, kamfumania mumewe na njia pekee aliyoona itamwondolea machungu yake ni kulipa kisasi kwa kuwa na mwanaume mwingine, simlaumu manake hapo ndipo akili na maarifa yake yalipoishia. Mwingine labda angeamua kulewa wakati hapo kabla hakuwahi kutumia kilevi chochote, mwingine labda wangekaa wayazungumze then wasameheane na maisha yasonge... Hapa pia inabidi kumpata mume wa Nasra na kumuuliza ni kwanini aliamua kutoka nje ya ndoa yake... Usishangae pia akikwambia chanzo ni mke wake..

Babu DC ndoa zina siri nyingi usione milango na madirisha ukafikiri kuna amani sana!


Nasra alimkosea heshima mumewe, ila pia hakustahili kufanyiwa ukatili wa namna ile...ndoa ni ngumu babu DC, mie hata nashindwa nimtete yupi...


usiseme unashindwa kumtetea yupi, ni sahihi kabisa kuto mtetea yoyote, maelezo yako ni sahii,wote wawili wameitika vibaya katika kutatua matatizo yao. sisi hapa tujifunze tu kutokana na makosa yao na tuache sheria iwahukumu.

pole mume wa nasra kwa kudhalilishwa, pole nasra kwa kuuumizwa na mume, pendaneni sameheaneni
 
Anhaa hiyo ndio point yako...!!
Labda kama tunaupungufu wa taarifa katika hii hadithi, ila kwa jinsi ulivyoeleza ni kuwa Mwanaume alirudi na kuwa mpole ndio "dada yetu" akapamba moto.....
Silengi kutetea upande wowote, au kuhalalisha kwa upande wowote ndio maana kama utakumbuka ulipoleta hii stori mwanzoni tu nilimlaani huyo "Kaka" kuwa "nyumba ndogo imefanya mambo"....
Leo baada ya kupata upande wa pili wa hadithi nimejaribu kutoa mawazo ya jumla kuwa katika nyumba kwa mujibu wa maandishi ya kidini yangu (japo kwa ufinyu) Mwanamke ana nafasi ya pekee sana katika kusimamia nyumba yake na familia....
Pamoja na u-victim wa dada Nasra ila tatizo rasmi limeanzia pale alipojaribu kulipiza kisasi, na yeye akatengeneza Victim mwingine "mumewe"... Sasa tukitaka kujenga hoja za nani ni Victim na alistahili nini basi wote ni victim!

Ndio maana nikaona kuwa turudi kwenye msahafu sahihi wa maisha (inaweza kuwa dini au asili yetu waafrika).....

  • Nini majukumu ya wanawake kwenye familia na nafasi zao?
  • Nini majukumu ya wanaume kwenye familia na nafasi zao?

NB: Tatizo limeshatokea, kujenga hoja kwamba nani ana makosa au nani alionewa inaweza isiwe na utamu sana Babu, tusaidiane kuelimishana namna bora katika ujenzi wa familia kama enzi zenu za miaka ya 47....

Bado naamini katika nafasi ya pekee ya Mama zetu katika kujenga Familia yenye furaha sana!


Nakubaliana na wewe ila ujue haya unayoongea ni katika hali ya amani kabisa....Na pia tukumbuke kwamba hiyo misahafu imekuwepo kwa karibia miaka 1000 sasa. Hata hivyo binadamu hajaacha kufanya vitu vya kuchefua.

Kwa hiyo nadhani tunaongelea jambo lile lile ingawa labda tunatokea kwenye angles tofauti..kati ya hali halisi na nadharia!!

Babu DC!!
 
[/B]usiseme unashindwa kumtetea yupi, ni sahihi kabisa kuto mtetea yoyote, maelezo yako ni sahii,wote wawili wameitika vibaya katika kutatua matatizo yao. sisi hapa tujifunze tu kutokana na makosa yao na tuache sheria iwahukumu.

pole mume wa nasra kwa kudhalilishwa, pole nasra kwa kuuumizwa na mume, pendaneni sameheaneni
Sante ndugu kwa ufafanuzi...simuhukumu yeyote kati yao...
 
Jamani nakumbuka Thread kuhusu hii Issue iliwahi kuwekwa hapa na Dark City(Babu DC) kumhusu huyu Mwanamke aitwaye Nasra wa Bunda,Mara aliefanyiwa kitendo cha kikatili na Mumewe ambapo alimgonga na Gari kisha kumburuta umbali wa KM 150 katika barabara ya Lami. Hizi ni picha zake nimezitoa Blog ya Dina Marios.
Nasra ameshafariki, Tuombe Mungu amlaze mahali pema peponi.
Dah Wanaume wenzangu this is too much!!


Wiki iliyopita tuliongea katika leo tena juu ya kisa cha Marehemu Nasra pichani.Mama huyu alikuwa mkazi wa Bunda mkoani Mara lakini Dar es salaam alifika kufanya matibabu katika hospital ya Muimbili.Kwa miaka takribani 23 alikuwa mke wa bwana Elia Makumbati na kujaaliwa kupata watoto wanne mkubwa kabisa yupo chuo kikuu cha UDOM.Kwa miaka yote wamekuwa na misuko suko sana kwenye ndoa mama akiwa anapigwa sana hata kuchanwa na viwembe.
Mwezi wa pili walitofautiana baada ya bwana kuoa mke mwingine.Wakiwa wametofautiana na Nasra kuendelea na maisha siku hiyo bwana akamfata akamkuta barabarani anatoka kazini.Akiwa na rafiki yake wanatembea akamfungia breki mguuni akamwambia anataka kuongea nae.Nasra akakataa akamwambia kama kuna maongezi hawezi kuongea nae kama vipi amfate nyumbani huku anaendelea kutembea.Bwana yule akamfata kwa nyuma akamgonga na gari na baada ya Nasra kuanguka akanasa chini hivyo kuendelea kumburuza umali wa kama mita 150 hivi.Alipofika kwenye tuta akanasuka bwana ndio kushuka kwenye gari kukimbia.
Kiukweli aliumia sana sana ngozi yote ya mgongoni,mbavuni,makalio,ikavuka na kubaki kwenye lami.Sikio lake la kushoto lote likaliwa na lami,mbavu 7 zilivunjika pamoja na mguu.Akapelekwa hospitali na baadae kulazwa Bugando Mwanza lakini ikawa anahitajika kuhamishiwa hospital ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.Akiwa muhimbili alikuwa na hali mbaya sana baadae ikathibitika kuwa ameumia ndani kwa ndani kwani alibadilika sana akavimba na kuwa mweusi.Kwamuda wote wa miezi takribani sita alikuwa katika maumivu makali na bahati mbaya hakuweza kupambana tena kupigania maisha yake.

Nasra pichani kulia mwenye kilemba chekundu akiwa na ndugu zake wakati akiwa mzima.


Usiku wa kuamkia jumanne ya tarehe 10 Nasra akaaga dunia.Ilikuwa ni huzuni sana jinsi alivyoteseka na namna mazingira ya kifo chake kilivyotokea.Tulikuwa na matumaini kuwa angeweza kupona maana dakika za mwisho alikuwa anaongea japo kwa shida.
Tunaomba mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Nasra mahala pema peponi,Amina.
Hii ni picha ya muwewe Elia Makumbati ambae mpaka sasa anatafutwa na jeshi la polisi kwa kitendo cha kinyama alichokifanya.Jeshi la polisi mkoani Mara wanafanya juhudi za kila namna kumkamata lakini amekuwa akikimbia mara aonekane Kenya,Botswana na kwengineko lakini bado hajakamatwa.Kwa utakae muona usisite kutoa ripoti zake.Mpaka askari wa upelelezi wa kimataifa interpol ina taarifa zake.
 
Last edited by a moderator:
hayo maumivu sio ya kawaida aise aliyokuwa anapata huyo mama
Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema
Na huyo mwanaume ni katili kiasi gani aise unajua kabisa umemgonga mtu na then bado unaendelea kudrive mita mia na hamsini kwenye lami aise
So sad
 
Back
Top Bottom