Mkuu hizi mechi 2 walizocheza Yanga na kupoteza, haziwezi kutoa picha ya kusema moja kwa moja Simba tutachukua ubingwa!
Ukiangalia ile mechi ya awali(Yanga Day), Walicheza na timu yenye muunganiko bora kabisa , alafu wao wakawa bize kubadilisha wachezaji ili kutoa nafasi ya kila mmoja kuonyesha uwezo wake kwa mashabiki ikiwa ni sehemu ya utambulisho.
Mabadiliko ya aina ile ni lazima yataathiri timu na kama mpinzani mnayecheza nae ana kikosi kizuri ni lazima apige goli.
Pia kwenye hii mechi ya juzi dhidi ya Rivers united, Yanga waliingia uwanjani wakiwa tayari wameshavurugwa kisaikolojia na mambo mawili, Jambo la kwanza ni kocha wao kuanza kujitetea kuhusu muunganiko wa timu na kuonyesha wasiwasi wa kushinda!
Jambo la pili ni kitendo cha wachezaji wake kadhaa ambao Yanga iliamini wangekuwa na msaada kwa timu katika mechi ile lakini wakazuiwa kucheza na kufanya Yanga wabaki wakihangaika na suala lao hadi siku ya mchezo, hapa ni dhahir hawakuwa na plan B ya haraka!
Binafsi pamoja na kuwa shabiki wa Simba bado naona Yanga inaweza kufanya vizuri zaidi hasa wakiachana na mpira wa maneno mengi na kuanza kucheza soka la uwanjani!