Natafuta kombinesheni Nina ekari 50 za mashamba Bora kabisa ya mahindi Rukwa

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Wadau mwaka jana nililima ekari 9 tu huku Rukwa nikapata Tani 21 na kulingana na Hali ya mvua ilivyokuwa na bei za mbolea nahisi ningepata zaidi mwaka huu nimeandaa ekari 50 kama Kuna mzamiaji Kwa msimu huu unaoanza Novemba anitafute tuunganishe nguvu.
 

Unatafuta wa kuungana naye kwa hii fake I'd. Au we ndio wale wa tuma kwa namba hii?
 
Unatafuta wa kuungana naye kwa hii fake I'd. Au we ndio wale wa tuma kwa namba hii?
TAPELI huyo. Msimu uliopita huwezi kutapa gunia 200 za mahindi kwenye ekari 9 . Kila ekari gunia 20?? Kilimo Cha wapi hiki Cha mahindi
 
Mpumbavu huyu, kwa msimu uliopita ulivyokuwa unawezaje kupata gunia 200 kwenye ekari 9?? Yaani kila ekari gunia 20?? Mpumbavu sana huyu
Labda mazao mengine alinunua kwa watu, huwezi kujua
 
Uko Rukwa sehemu gani?
 
Andaa wosia wakati unaingiza mguu hapa kwani utafia shambani kwa kitakachotokea
 
Mbona inawezekana vizuri kabisa! watu wanavuna hadi gunia 30 kwenye heka moja we wawapi wewe!!

Uvune gunia 30 kwa heka kwa hiki kilimo cha kutegemea mvua? Hata Japan hawavuni hizo gunia 30@heka. Kama ni hivyo kila mtu si angeenda kulima mahindi? Kama unaweza kuvuna gunia 30 kwa heka, huyo muhuni si aende bank ya kilimo akakope badala ya kuleta utapeli wa kitoto hapa kutaka mshirika?
 
tani 21 ni kilo 21,000 ukigawa kwa 100 sawa na maguni210 ukigawa eka 9 kwa magunia 210 ni wastani wa gunia 23 kwa eka.
ulitmia utaalam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…