Natafuta nafasi ya kuichezea klabu yoyote inayoshiriki NBC Premier League Tanzania

Natafuta nafasi ya kuichezea klabu yoyote inayoshiriki NBC Premier League Tanzania

Tumia vizuri mashindano ya ndondo cuo ukija Dar. Ila pia wakatiligi inapokwisha kusubiri msimu mungine timu nyingi sana zinaruhusu wachezaji kwenda kufanya majaribio.

Kwa umri ulionao wa miaka 26 ili utoboe unatakiwa uwe na kipaji extra ordinary ili uingie moja kwa moja kwenye nbc premier ligi. Yaani uwe na kipaji kuzidi kina ndemla, ambundo, kibu na wengineo.

Kila la kheri.
 
Miaka: 26
Kitambulisho cha NIDA: Ndiyo ninacho
Height: 163cm
Elimu: Degree
Mkoa ninaoishi: Kigoma (ila naweza kuondoka hivi karibuni na kwenda Dar es Salaam)

Mkuu hapo kwenye 'Clip' mpaka nijipange (uchumi umenikwamisha sana kwenye vitendea kazi).

Sent using Jamii Forums mobile app
Ondoka huko nenda Dar, Kuna viwanja vingi vya majaribio kaanzie hapo. Kama una ndugu Dar muombe akupokee na kukuhost ukapambanie ndoto yako, Vipaji ni vingi sana mtaani, unahitaji sehemu ukaonekane si humu kwenye mtandao mdogo wangu.

Kila la heri.
 
je unajihusisha na timu za hapo mtaani kwako?.

Kwa kucheza mtaani yaweza kuwa rahisi kuonwa na Mtu/Watu na wakaweza kukunadi kwa Wahusika...na ukinadiwa na Mtu au Watu itakuwa rahisi sana kuitwa kuliko kujinadi mwenyewe.

Ingawa hiyo haiondoi ukweli kwamba kama kipaji unacho unacho tu, wanasema Pembe ya Ng'ombe haifichiki...jitahidi kujichanganya kila kulipo na Kiwanja wanapocheza mpira ili Wadau wakuone.
Nimeshaanza mkuu, japo bado nina safari ndefu kidogo ya kuonekana.
 
Miaka: 26
Kitambulisho cha NIDA: Ndiyo ninacho
Height: 163cm
Elimu: Degree
Mkoa ninaoishi: Kigoma (ila naweza kuondoka hivi karibuni na kwenda Dar es Salaam)

Mkuu hapo kwenye 'Clip' mpaka nijipange (uchumi umenikwamisha sana kwenye vitendea kazi).

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa miaka 26 na Bado ujatoka duh angalia mishe nyingine
 
Ondoka huko nenda Dar, Kuna viwanja vingi vya majaribio kaanzie hapo. Kama una ndugu Dar muombe akupokee na kukuhost ukapambanie ndoto yako, Vipaji ni vingi sana mtaani, unahitaji sehemu ukaonekane si humu kwenye mtandao mdogo wangu.

Kila la heri.
Ahsante sana dada yangu.

Wadau wengi wa JF hawanikubali ndugu yao (ndio maana timu zetu nyingi hazina mafanikio ndani na nje ya nchi maana wenye nia na juhudi hawakubaliki, ukilinganisha na wenye vipaji. Tumezoea kupondana, kupeana destructive feedback na hatuna roho ya kusaidiana kwa upendo). Halafu mtu akitoboa, ndio watu wanaanza kumkumbuka.

Ninao familia na ndugu huko Dar ila nawakwepa maana hawani'support kabisa japo wanajua kuhusu hiki kipaji changu. Watu wangu wengi wa karibu hawaniungi mkono pia mimi kuendeleza kipaji changu katika soka, Ila wanataka nitafute kazi na kuajiriwa (na kama unavyoona kwa sasa - hali ya ajira ni mbaya nchini).

Yaani ni bora hata ningekuomba wewe unipokee na uni'host kama upo Dar kwa kweli (ningekuwa tayari kusaidiwa na wewe).
 
Kwa miaka 26 na Bado ujatoka duh angalia mishe nyingine
Acha tu ndugu. Toka kipaji changu kionekane, nililazimika (na kulazimishwa) kugeukia masomo mpaka namaliza chuo.

Nimehangaika na kutafuta ajira, internship na volunteering bila mafanikio, lakini moyoni mwangu tangu nikiwa mdogo mojawapo ya passion yangu ni kucheza mpira. Usifikiri nilikuwa sifanyi kitu mpaka nafika umri huu! Ni vile tu bado sijabahatika.
 
Sasa mtu akikuomba video clip si umpe mshikaji akurekodi ?
Nenda hata wanakofanya mazoezi vijana jiunge nao mtu aku rekodi
Nilipokea mawazo yote ya wadau. Ila hivi vitu sio vya kukurupuka.
Nilikuwa kwanza natafuta sehemu wanakofanya mazoezi (na nimeshaanza).
Mpango upo na nimeshaanza kulifanyia kazi hilo.
 
Tumia vizuri mashindano ya ndondo cuo ukija dar. Ila pia wakatiligi inapokwisha kusubiri msimu mungine timu nyingi sana zinaruhusu wachezaji kwenda kufanya majaribio.

Kwa umri ulionao wa miaka 26 ili utoboe unatakiwa uwe na kipaji extra ordinary ili uingie moja kwa moja kwenye nbc premier ligi. Yaani uwe na kipaji kuzidi kina ndemla, ambundo, kibu na wengineo.

Kila la kheri.
Shukrani mkuu! Hiyo ni mojawapo ya ajenda zangu nikija Dar.

Hata kama kucheza Ligi kuu ya NBC itakuwa vigumu papo-hapo, sio vibaya nikaanza na daraja la pili halafu timu hiyo niliyoichezea ikapanda daraja na kuingia Ligi kuu msimu ujao. Au pia mbeleni naweza nikaonekana huko-huko na kuja kusajiliwa kwenye klabu inayoshiriki Ligi kuu.
 
Habari wadau wa Jamii Sports?

Nina ombi moja kwenu.

Mimi ni kijana Mtanzania mwenye kujituma, mwenye nidhamu na mchapakazi. Ninaandika ili kuonyesha nia yangu ya kuomba nafasi ya kuichezea klabu yoyote inayoshiriki Ligi kuu ya NBC, kwa nafasi ya "Mid fielder" au "Defender". Nipo tayari kusajiliwa na klabu yoyote na kuanza kuchezea kikosi chochote.

Nilipokuwa form 3 nilicheza katika timu iliyofanikiwa kutwaa ubingwa katika mashindano ndani ya shule yangu. Wengi walikubali sana kipaji changu hadi baadhi ya wanafunzi wenzangu waliniita freemason kwa kunionea wivu, maana nilikuwa nikicheza kwa umakini, nidhamu na ustadi wa hali ya juu uwanjani.

Bahati mbaya familia na marafiki hawakuniunga mkono tokea hapo awali, hivyo nililazimika kuendelea na masomo. Wote niliowahi kuwashirikisha kuhusu shauku yangu ya kucheza mpira hawakunipa nafasi wala kunisaidia kiuchumi au kulea kipaji changu.

Lakini sijakata tamaa mpaka sasa. Nina ndoto ya siku moja kuichezea klabu mojawapo nchini hadi kutwaa kombe la klabu bingwa Afrika, pamoja na Taifa Stars (timu ya Taifa) hadi kufanikiwa kutinga katika timu zitakazocheza kombe la dunia 2026.

Natumaini kuwa wahusika mtanipokea na kunipa nafasi katika klabu. Pia, natumaini kuwa wenye connection mtazingatia na kuni'recommend kwa wahusika. Nami nitakubali kuwa chini kufundishwa, kuelekezwa na kushirikiana vizuri na wachezaji wenzangu ili kipaji changu kiweze kukua zaidi, nami niweze kucheza na kufanikisha malengo ya klabu.

Ahsanteni sana wakuu kwa kuzingatia.

Mawasiliano:
0743744471

Sent using Jamii Forums mobile app

Utafika tu, nenda taratibu,
 
Habari wadau wa Jamii Sports?

Nina ombi moja kwenu.

Mimi ni kijana Mtanzania mwenye kujituma, mwenye nidhamu na mchapakazi. Ninaandika ili kuonyesha nia yangu ya kuomba nafasi ya kuichezea klabu yoyote inayoshiriki Ligi kuu ya NBC, kwa nafasi ya "Mid fielder" au "Defender". Nipo tayari kusajiliwa na klabu yoyote na kuanza kuchezea kikosi chochote.

Nilipokuwa form 3 nilicheza katika timu iliyofanikiwa kutwaa ubingwa katika mashindano ndani ya shule yangu. Wengi walikubali sana kipaji changu hadi baadhi ya wanafunzi wenzangu waliniita freemason kwa kunionea wivu, maana nilikuwa nikicheza kwa umakini, nidhamu na ustadi wa hali ya juu uwanjani.

Bahati mbaya familia na marafiki hawakuniunga mkono tokea hapo awali, hivyo nililazimika kuendelea na masomo. Wote niliowahi kuwashirikisha kuhusu shauku yangu ya kucheza mpira hawakunipa nafasi wala kunisaidia kiuchumi au kulea kipaji changu.

Lakini sijakata tamaa mpaka sasa. Nina ndoto ya siku moja kuichezea klabu mojawapo nchini hadi kutwaa kombe la klabu bingwa Afrika, pamoja na Taifa Stars (timu ya Taifa) hadi kufanikiwa kutinga katika timu zitakazocheza kombe la dunia 2026.

Natumaini kuwa wahusika mtanipokea na kunipa nafasi katika klabu. Pia, natumaini kuwa wenye connection mtazingatia na kuni'recommend kwa wahusika. Nami nitakubali kuwa chini kufundishwa, kuelekezwa na kushirikiana vizuri na wachezaji wenzangu ili kipaji changu kiweze kukua zaidi, nami niweze kucheza na kufanikisha malengo ya klabu.

Ahsanteni sana wakuu kwa kuzingatia.

Mawasiliano:
0743744471

Sent using Jamii Forums mobile app
Una miaka mingapi ?
Height yako ikoje ?
Uko mkoa gani ?
 
Back
Top Bottom