Natafuta Rafiki, Mchumba

Nawe pia toa wasifu kwasababu wapo wadada kibao wanatafuta wachumba pia ila hawajajitokeza kusema wazi, siunajua kina dada wanaona aibu kusema. Usisahau kusema kabila pia wengine wanaogopa makabila fulani fulani yanayojua kupiga mangumi na ambayo mama mkwe huwa anasauti kwenye nyumba zote za watoto wake wawe wa kike au wa kiume na ambayo mwanamke ni sawa na ng'ombe kuna kiboko maalumu cha kumchapia.

Nakushauri utafute mwenyewe, ila mwombe sana Mungu atakupatia unayehitaji watu wanaweza kusaidia kukuonyesha ila mambo mengine ukamaliza mwenyewe. Ujue makucha huwa yanafichwa kabisa kabla ya ndoa, ila mkishatoka kanisani tu yanakuwa huru kutokeza. Ila ukimpata uliyepewa na Mungu hayo yote hayatakuwepo.
Ukumbuke kupima afya yako na ya utakaye mpata kabla ya chochote na msubiri kupima tena miezi mitatu.

Ukumbuke kuwa tabia yako inaweza ikamharibu mwenzako au ikamgeuza mwenzako kabisa hata kama alikuwa changudoa akaacha kabisa akawa mama wa mfano wa kuigwa au kama alikuwa mtakatifu hata mwanaume hajamjua (Bikra) akawa malaya wa kutembea hata na ndugu yako wa damu.
 

Mimi ninaye girl friend wangu, tumeshindwana dini, mimi muislamu yeye RC, nikutumie namba zake?
 
Mziwanda acha mambo yako bana,mchumba utampata hapa jamvini?,Wachumba wanapatikana Makanisani,Misikitini,kwenye Social places,but hapa jamvin i am sure hautapata!!!!!
 

Kwanini usiende kanisani? kule utakuna wengi wenye tabia nzuri ambao mtaelewana vizuri kuliko wale viruka njia.
 
Eh Fidel mwaliko nimeupata ila mwenzangu sera zako kwangu ngumu! Maana mh hata sijui nijiteteeje kusema ukweli ile idara ambayo kwako ni muhimu sana mie siiwezi!!........ sina budi

Why don't you let him be the judge of that?
 
Nakaa hapa Africa kusini
pretoria. Natafuta mchumba wakuoa ambaye anazo sifa zifuatazo:

Natafuta mwana mke wakuoa ambaye alikata tamaa kwa sababu ya kukosa
mchumba.
Awe na umri wa kati ya miaka 27-35
Awe ana moyo wakuishi kwenye upendo
Awe mweusi
Asiwe malaya
Awe na matiti makubwa sana
Awe mwenye sura mbaya
Asiwe mlevi
Asiwe anavuta sigara
Awe na elimu ya secondari
Awe tayari kunitumia picha yake.
Asiwe mtu wakujivuna
Awe mchaa mungu
Asiwe na virusi vya ukimwi na awetayari kucheck afya.

Tafadhali kama unawazo au unajua m-dada mrembo na myenyekevu..nipashe ili niwasiliane naye.

NITAMPA SIFA ZANGU KUPITIA EMAIL
 

JosM................................ karibu
 
Weka na wewe sifa zako hapa hapa wengine tuna mashemeji zetu wanahaha kutafuta wachumba.
 
Hivi huwezi kumpata mchumba mpaka utangaze kwenye mtandao? Hapo unapoishi vipi? Nyumbani kwenu vipi? Angalia vizuri, utaopoa hata ambavyo haviopoleki!
 
hueleweki kabisaa!! maana sifa ya sita "awe na sura mbaya" halafu mwisho unauliza mrembo! wapi na wapi??
 

mzee hapo unanikanganya.
Hizo nyakundu mbili ndo vipivipi?
Awe na sura mbaya, then awe mrembo, hueleweki
 
wachumba wanapatikana kanisani.....
 
Tafadhali fafanua, usikikoseshe kiswahili maana lakini!
Mkuu, uzuri ni wa kuzaliwa nao kutoka kwa wazazi. Urembo ni wa kujitafutia. Urembo ni nomino inayotokana na kitenzi "kujiremba", yaani kujitengeneza, kujiunda, kujiweka sawa, kujibadili kama utakavyo kwa kutumia vifaa na vyombo mbalimbali kv. madawa, malosheni, mavazi, nk. ili upendeze na kuvutia watu.

Kumbe hata aliye na sura mbaya anaweza kujiremba kwa kutumia mavifaa na akajiunda na kuvutia watu akawa mrembo. Mrembi si lazima awe mzuri japo warembo wengi kama hatua ya mwanzo wanaanza kujichuja kwa uzuri (sura) na baadaye wanaongezea mambo mengine ya kuwa-qualify kama warembo. Nawasilisha!
 

Kwa hiyo wewe hutaki uzuri, unataka ulimbwende, au siyo?
 
Mkuu Idimi
Natafuta mchumba wa kike awe naelimu sio chini ya kidato cha sita,
Awe mrefu na mwembamba wa wastani as well as umbo na sura ya kulidhisha.
Asiwe mweusi wala mweupe sana(asiwe wa kutumia mkorogo,pombe)
Dini yoyote ila asiwe mlokole.
Asiwe mhaya au mchaga
Umri:18-24

Wasifu wangu!
Umri:28
Elimu: Degree
Mrefu kiasi
Rangi:Maji ya kunde
Napenda sana kufanya kazi mda mwingi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…