Nataka kuacha kazi niingie kwenye kilimo nishaurini

Nataka kuacha kazi niingie kwenye kilimo nishaurini

Kilimo cha mchele boss

Sent using Jamii Forums mobile app
Hongera ni wazo zuri.
1.La msingi ni kuangalia wapi unataka kufanyia hiki kilimo
2.Utafanya kilimo cha aina gani,kutegemea mvua au utamwangilia
3.Upatikanaji wa maji huko shambani ukoje
4.Na mengine mengi ya kuangalia,ila fuata ushauri wa mdau hapo juu anza kwanza hicho kilimo kabla hujaacha kazi iliuweze pata experience na pia kujifunza .
 
kilimo konahitaji mtaji na usitegemee kilimo cha mvua fanya kilimo cha umwaguliaji cha muhumu ni mtaji na kutafuta shamba lililo karibu na mto
 
hii kweli kuna mtu alianza na njiwa kama wanne akiwa na umri mdogo sana chini ya miaka 10 lakini mpaka leo bado familia inafaidika na njiwa hao kama kitoweo huku yeye akiwa na miaka 50 hivyo mradi umekaa zaidi ya miaka 40 sasa.
Njiwa mbona naona miaka hii hawaja vuma sana kama miaka ya 94 na kuendelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku umeacha kazi umelima matikiti yako umeyapakiza kwenye fuso unayo kama 9,000 hivi kwa matarajio ya kuuza 2000 kwa piece unafika sokoni fuso kama 50 hivi hivyo inabidi uuze 500 hapo ndo utaelewa nini maana ya kuacha kazi
Na huu ndiyo ukweli,kilimo ni kizuri ila unahitaji mikakati mizuri kutoboa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upo mkoa gani mkuu?, ni muhimu kujua ili ushauri uendane na mazingira.

Unaposema masoko, yanatofautiana kulingana na mahali ulipo
mfano; Kilimanjaro, Arusha wateja tegemezi wa mazao ya kilimo ni wakenya.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usikulupuke kijana,utajiri hautafutwi kwa staili hiyo kwa nchi zetu za Africa.USA,CANADa unaweza kufukuzwa ajira rasmi Leo kesho asubuhi ukaanza kazi ya box na ukakusanya pesa ya maana kulingana na masaa utakayokomaa.Wakati bongo ukitimuliwa mpaka upate kazi kwa kipindi hiki ni lazima ulale njaa na kunyimwa unyumba.Nikupe mfano huku kusini nyanya ndoo kubwa shambani inauzwa chini ya 2000 na wateja hakuna na wakulima wameacha madeni na wengine wameteleleza mashamba ya nyanya.Sasa kwa staili hii kama umeacha kazi kwa mbwembwe utaacha kuwa mlevi.Kama walivyoshauri halo juu usiache kazi bila ya kuwa na uhakika na utakachokifanya,Huku kusini matajiri asilimia kubwa ni wafanyabiashara wa mazao ya wakulima na s wakulima wenyewe.
 
karibu me nina miezi minne baada ya kuacha kazi karibu sana
 
tikiti hizi! heka nne zimekula zaidi ya mill 4 ukija huku uwe na mtaji wa kutoshaView attachment 858236
IMG_20180904_102350.jpg
 
Kilimo ni fedha,na ili kikulipe kinahitaji fedha na si nguvu.Kabla ya kuacha kazi hakikisha mashamba unayoyategemea yana maji ya uhakika mwaka mzima,na zao unalolima liwe na sokoni la uhakika
 
Back
Top Bottom