Nataka kuanza kusoma masomo ya sekondari kupitia elimu ya watu wazima

Nataka kuanza kusoma masomo ya sekondari kupitia elimu ya watu wazima

Joyeuse

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2013
Posts
275
Reaction score
182
Wazima wana Jf.
Kama nilivyoeleza kwenye kichwa cha habari hapo juu.

Nina umri wa miaka 31. Nilimaliza shule ya msingi miaka 18 iliyopita. Sikufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari. Japo nilitaka sana kuendelea lakini hali ya nyumbani ilikuwa ngumu mno hivyo ikashindikakana hata kwenda zile shule za taasisi enzi zile.

Katika purukushani za maisha nilijichanga kipesa mwaka 2006 nikajiunga na elimu ya watu wazima ila majibu hayakuja mazuri bado nikashindwa tena kurudia kutokana na hali ya kifedha. Nikajitahidi tu kwenda English course nashukuru nimejua kingereza na pia nikasoma french course pia kifaransa najua.

Ila bado najiona sijakamilika bila elimu ,nataka kusoma. Mpaka leo hii kiu yangu nisome nifike chuo hasa. Japo naona watu wanaambizana haina haja ya kusoma bora kujiajiri lakini kujiajiri bila elimu sidhani kama unaweza fika mbali unless watu wakuendeshee.

Nina watoto 3 na mume pia.
Ila bado naitaka elimu ya sekondari.. na mara hii nimejipanga vizuri kabisa.
Je niko sahihi ama ndio nakumbuka shuka kushakucha??

Ushauri wenu ni muhimu sana kwa hili
Nannahitaji faraja na munipe moyo niweze kufanikisha hili

Natanguliza shukrani.
 
Zikipungua pumba zangu,zinabaki za kwako uliyesoma .. na ndizo hizi ulizozimwaga hapa.
Shukran

Fuata haja ya moyo wako. Lakini endapo una muda si bora ungejiunga na hizi QT?

Utaratibu wa elimu ya watu wazima unaweza usiwe rafiki sana kama hauna kujisimamia vizuri na msaada wa karibu.
 
Fuata haja ya moyo wako. Lakini endapo una muda si bora ungejiunga na hizi QT?

Utaratibu wa elimu ya watu wazima unaweza usiwe rafiki sana kama hauna kujisimamia vizuri na msaada wa karibu.
Ahsante sana kwa kunifungua

Nitafanya hivyo.[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Kuna wenzako wana miaka kama yako na wamekuzidi kidogo wapo chumba cha pili nawasikia wanadiscus muda huu kwa ajili ya mtihani wa taifa. Je, wewe unaweza? Fuata kile moyo unapenda.
Ila kama lengo ni kuongeza elimu tu, soma. Kama lengo ni kupata ajira, kwa kweli ni changamoto.
 
Ukishamaliza secondary ulitaka uchukue degree gani???

Sikushauri uende secondary .. mambo ni magumu na yamepitwa na wakati...

Sijui utaratibu ukoje huko lakini kama unaweza anza kusoma cheti then uende diploma kama hata usipofika chuo kikuu tayari una qualifications zinazokufanya uwe na uwezo kujiajiri ama kuajiriwa mamii..

Best of luck!
 
azima wana Jf.
Kama nilivyoeleza kwenye kichwa cha habari hapo juu.

Nina umri wa miaka 31. Nilimaliza shule ya msingi miaka 18 iliyopita.. sikufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari.. japo nilitaka sana kuendelea lakini hali ya nyumbani ilikuwa ngumu mno hivyo ikashindikakana hata kwenda zile shule za taasisi enzi zile. Katika purukushani za maisha nilijichanga kipesa mwaka 2006 nikajiunga na elimu ya watu wazima ila majibu hayakuja mazuri bado nikashindwa tena kurudia kutokana na hali ya kifedha. Nikajitahidi tu kwenda English course nashukuru nimejua kingereza na pia nikasoma french course pia kifaransa najua.. ila bado najiona sijakamilika bila elimu ,nataka kusoma. mpaka leo hii kiu yangu nisome nifike chuo hasa. Japo naona watu wanaambizana haina haja ya kusoma bora kujiajiri lakini kujiajiri bila elimu sidhani kama unaweza fika mbali unless watu wakuendeshee..
Nina watoto3 na mume pia.
Ila bado naitaka elimu ya sekondari.. na mara hii nimejipanga vizuri kabisa.
Jee niko sahihi ama ndio nakumbuka shuka kushakucha??

Ushauri wenu ni muhimu sana kwa hili
Nannahitaji faraja na munipe moyo niweze kufanikisha hili

Natanguliza shukrani.
Anza
 
Ukishamaliza secondary ulitaka uchukue degree gani???

Sikushauri uende secondary .. mambo ni magumu na yamepitwa na wakati...

Sijui utaratibu ukoje huko lakini kama unaweza anza kusoma cheti then uende diploma kama hata usipofika chuo kikuu tayari una qualifications zinazokufanya uwe na uwezo kujiajiri ama kuajiriwa mamii..

Best of luck!
Shukran
 
Kuna wenzako wana miaka kama yako na wamekuzidi kidogo wapo chumba cha pili nawasikia wanadiscus muda huu kwa ajili ya mtihani wa taifa. Je, wewe unaweza? Fuata kile moyo unapenda.
Ila kama lengo ni kuongeza elimu tu, soma. Kama lengo ni kupata ajira, kwa kweli ni changamoto.
Naongeza elimu tayari nimejiajiri
 
Back
Top Bottom