Nataka kuanza kuuza nguo kwa mtaji wa Tsh. 50,000/-

Nataka kuanza kuuza nguo kwa mtaji wa Tsh. 50,000/-

Habarini wana group, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. mwishoni mwa mwezi huu nina mpango wa kuanza biashara ya NGUO, akiba yangu ni elfu 50.

Sehemu nilioiwaza ya kununua mzigo ni karume nasikia hapo ukiwai asubuhi saa 11 au 12 unapata nguo mzuri sana kwa bei ya elfu 5 au chini yake reja reja kwa nguo 1.wana jamvi naomba mnipe maujanja jinsi ya kupata wateja haraka na changamoto zake hii biashara.

Nataka kutembeza maana sijapata sehemu ya kuweka ndo kwanza naanza.Najua humu wapo watu wazoefu waliobobea kwenye biashara hii.pia nitashukuru sana mkinipa ramani ya sehemu ya kutembeza zenye wateja wengi hata mikoani nitashukur sana.
Kwa kufanya biashara ya kutembeza nguo huo mtaji unatosha. Ushauri wangu nunua nguo za mtumba za watoto zinanunulika sana. Ni rahisi mteja mmoja kununua nguo zaidi ya tano kwa ajili ya mtoto/ watoto. Ukienda Ilala kuna nguo nzuri za watoto za mtumba, unanunua nguo ya 1000 wewe unaenda kuuza 2000, ya 2000 unaweza kuiuza 3000 hadi 4000 au zaidi ya hiyo kutegemea na nguo ilivyo. Unaponunua katika mzigo wako baadhi ya nguo jitahidi kumechisha kama ni suruali iwe shati yake, kama ni sketi iwe na blauzi yake. Kila la heri.
 
Mtaji unatosha huo ukipata t-shirt kali uwe unapost na humu ,fungua pia page insta huko kila la heri mkulu.
 
Habarini wana group, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. mwishoni mwa mwezi huu nina mpango wa kuanza biashara ya NGUO, akiba yangu ni elfu 50.

Sehemu nilioiwaza ya kununua mzigo ni Karume nasikia hapo ukiwahi asubuhi saa 11 au 12 unapata nguo mzuri sana kwa bei ya elfu 5 au chini yake reja reja kwa nguo 1. Wana jamvi naomba mnipe maujanja jinsi ya kupata wateja haraka na changamoto zake hii biashara.

Nataka kutembeza maana sijapata sehemu ya kuweka ndo kwanza naanza. Najua humu wapo watu wazoefu waliobobea kwenye biashara hii. Pia nitashukuru sana mkinipa ramani ya sehemu ya kutembeza zenye wateja wengi hata mikoani nitashukur sana.

Mwanangu, ngoja nishare uzoefu wangu

Nilifanya hii mambo 2015/16 japo indirect. Aisee inalipa, siku za wkend nilikua naenda Ilala pale asubuhi saa 11 niko kweny gari kutokea River-side. Nilikua nikifika pale nafanya survey kwanz kama dakika 10 to 20 hiv kuona wapi leo napata viwalo vikali.

Baada ya hapo nikawa naanza kuchagua sasa na bonge la fuko la debe 6 mwana. Siku wahi kulijaza ila manunuzi ya pale pia sikuwahi zidisha lak 1. Nilifanikiwa hadi kufahamika na baadhi ya wauzaji, wakanijua ni mzee wa wkend.

Aisee pale masaa yanavyosogea bei zinapanda. Niliwahi acha nguo za 1500 nikaja baada ya nusu saa nikakuta anauza 2500 [emoji1787]

Ila sikua nauza reja reja mwenyew. Nilikua mwajiriwa, nikawa na ndugu zangu wa 4 vijijin nikinunua natuma wanauza, so wkend nilizigawanya kila mmoja nikienda leo ni hadi wk 3 au 4 zipite, sometimez vijijin biashara ilikua inakua mbaya ila anawez enda hata mwez nanusu hajamaliza mzigo kwa mtu mmoja.

Ila baada ya sagula sagula ya Ilala nikawa nahamia k/koo kujazia vinguo special vya watoto, chupi za watoto, wanawake, shidilia, boxer kidogo japo hiz za wanaume hazikua fast moving.

Nilikua nikifika geto pale namwaga mzigo chin naanza kupanga bei za kuuzia kulingana na uzuri na bei niliyonunulia, nikawa natenga kwa kuweka kweny mifuko midogo midogo ikiwa na bei zake ndani. So kama waliuza zaidi ilikua no yao, mi nilikua nahitaji warudishe mtaji wangu tu, faida nilikua naigawa nusu yao nusu yangu.

Ila badae nilihama Dar nilikuana kero za usafiri na mafuriko nikasema nikajaribu maisha mikoani. Ila najipanga nitakuja tena nianze upya. Niliipenda hii biashara siyo siri.
 
Habarini wana group, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. mwishoni mwa mwezi huu nina mpango wa kuanza biashara ya NGUO, akiba yangu ni elfu 50.

Sehemu nilioiwaza ya kununua mzigo ni Karume nasikia hapo ukiwahi asubuhi saa 11 au 12 unapata nguo mzuri sana kwa bei ya elfu 5 au chini yake reja reja kwa nguo 1. Wana jamvi naomba mnipe maujanja jinsi ya kupata wateja haraka na changamoto zake hii biashara.

Nataka kutembeza maana sijapata sehemu ya kuweka ndo kwanza naanza. Najua humu wapo watu wazoefu waliobobea kwenye biashara hii. Pia nitashukuru sana mkinipa ramani ya sehemu ya kutembeza zenye wateja wengi hata mikoani nitashukur sana.

Pale mwenge Kuna sehemu wanauza nguo yoyote ile 3000. Vinguo vizuri quality nzuri Sana..
Pia vipo vikoti 5000. Ningekuwa naanza biashara ya nguo ningeanzia pale. Ila labda karume wapo cheap zaidi
 
inawezekana nmeshuhudia mtu anakuza 30,000/ mpka milion kwa mwaka huu tu kwa biashara ya nguo. alianza december hv
 
Ongeza kidogo mtaji bro huwezi kuanza biashara na nguo nne (4)

Matajiri wa Jf!!

50,000 ni nguo nne?

Changanya karume na Ilala
Kuna wanao tega karume,Ilala, na Tandika

Pia Manzese jumatatu na Alhamis wanafungua Ballo

Chagua blouse nzuri za kuanzia na visuruali

Pita Maduka ya Kariakoo wadada wengi hawapati Time ya kuzunguka utapata wateja

Pita mitaa ya chuo na maeneo yenye watu wa kipato cha wastani

Siyo kazi ndogo ila ukipambana utafika
 
Pale mwenge Kuna sehemu wanauza nguo yoyote ile 3000. Vinguo vizuri quality nzuri Sana..
Pia vipo vikoti 5000. Ningekuwa naanza biashara ya nguo ningeanzia pale. Ila labda karume wapo cheap zaidi

Wa mwenge wanachukua nguo Karume
Zina fungiliwa Jumatatu na Ijumaa saa 12- saa 4 hivi

Ni za kupigania unapata gauni nzuri kama ya dukani wanaanzia 10,000 kuendelea kulingana na ubora wa nguo

Uwe tu na nguvu za kupigania
 
inawezekana sana
wahi saa kumi uwe pale su tisa mtafute bro yoyote pale anaefungua mizigo muite chemba mwambie "bro mimi nina mtaji wa 50k ndo naanza naomba sapoti" mtaelewana tu basi wakifungua mzigo unachagua chagua na anakuelekeza hii acha hii chukua hivyo basi mdogo mdogo unakuwa mzoefu


ukianza uje nikuungishe mkuu niletee mablauzi ya kike free size yakuvalia suruali mimi chibonge hivi



Mungu akutangulie
 
Back
Top Bottom