Nataka kufahamu mambo muhimu katika Uwekezaji kwenye shule ya awali

Nataka kufahamu mambo muhimu katika Uwekezaji kwenye shule ya awali

Mkuu hiyo approach yako nakiri it was the best in the previous era! Zama hz haifai! ItakuCost more! November kuna pahali nilienda kuchukua flem ya biashara. Nikaenda TRA, tukayajenga kisha wakanambia MAKADIRIO niende January! Nikaenda Halmashauri tukamalizana leseni! January pia nikamalizana na TRA.

JIRANI na flem yng kuna jamaa ana biashara ya mambo ya vioo na aluminum, akawa anancheka ninavojihisisha na Mambo za TRA na Halmashauri!

Km wiki 2 zilizopita TRA wametimba kwa jamaa! Walichomfanya ktk hesabu walizompa! Kasema akimaliza DENI LA TRA anafunga Biashara!
bahati mbaya Sana Mimi nakuwa tofauti na wengine pindi ninapotaka kuanzisha Jambo langu, Mimi huwa naanzishaga tu bila kujiuliza maswali mengi, naanzishaga Kisha TRA watakuja, wizara itakuja, na wengine watakuja,Kisha tunakaa meza moja tunayajenga safar inaendelea, lakini ukifuata vigezo na mashart hata duka la vyombo la kawaida hutofungua.....inchi ngumu hiii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo sio majengo tatizo ni usajili wa hiyo shule kwa mjibu wa wizara husika.
Eneo liwe na 2accre ikiwa town ukiwa sio town accre7
Uombe kubali cha kujenga kwa kuwabatanisha yafuatayo
Hati ya kiwanja, uwezo wako 60m nk.


Sent using Jamii Forums mobile app
Kitu nilichojifunza wasomi tunachelewa sana kufanikiwa sababu tuna fanya analysis nyingi sana mwisho wa siku zinatukatisha tamaa.

Nilipata kukutana na dogo wa miaka 22 anamiliki shule ya private elimu yake form 4 nilijifunza kitu toka kwake.

Nakushauri we kulupuka tu ,wakija hao wajomba unakaa nao mezani mambo yanaisha hiyo ndio formula
 
Nitakushauri hivi wewe na watu wote wenye mawazo ya kuanzisha shule: Jambo muhimu sana sana ni kujitofautisha na wengine. Ilivyo ni kwamba kuna utitiri wa nursery school na kila unayokwenda unakuta ina sifa zile zile (kwa bahati mbaya sana ni sifa mbaya). 1. Ujanja janja wa kupiga fedha: Ukiondoa zile shule za maana kama Internatinal school, hizi nyingine zote wana vi-ada, vi-michango na tozo zisizo na maana. kwa mfano tu hili la kumpa mtu tenda ya kushona sare ni kero moja mbaya sana. Kwa nini kama umeamua wanafunzi wavae sare fulani usiwape uhuru wa kushona au kununua wanapotaka? Je, hakuna uwezekano wa wanafunzi kusoma kwa nguo za kawaida tu kama nchi nyingine? 2. Mazingira ya shule: Shule karibu zote nilizozungumzia zina mazingira yanayofanana i.e. ya hovyo, machafu, hakuna maua, miti wala bustani. 3. Vyakula vya hovyo: Vyakula navyo utadhani kuna sheria inataka walishe watoto vyakula vya aina moja. Wengi ni uji wa dona, ugali wa maharage nk. Anyway, kuna mengi sana yanafanya nursery zetu ziwe za kijima na wewe una nafasi ya kuanzisha kitu kipya (japo kwa style uliyoanza nayo tu naona utafuata mkondo). Mwisho nikuambie kuwa kama unataka kutengeneza faida ya mara moja kwenye shule, basi hiyo siyo biashara inayokufaa. Shule kwanza inatakiwa u-invest kwa muda ndiyo utaona matokeo yake.
mkuu umenena vyema, hizi shule zimekosa mvuta zaidi ya mtoto kujua English ya kuungaunga hakuna lingine pia inawadumaza watoto sana.
 
Back
Top Bottom