Nataka kufungua mgahawa ambao utakuwa maalum kwa kuuza Biriani tu maeneo ya Kinondoni

Nataka kufungua mgahawa ambao utakuwa maalum kwa kuuza Biriani tu maeneo ya Kinondoni

Asante sana kwa maua na pia kwa ushauri na nimekuelewa vyema. Nafkiria nikiweka huo mgahawa basi kitu “biriani” iwe ndio brand kwaiyo ningetamani iwepo siku zaidi ya moja, ikiwepo walau siku 3 ndani ya wiki (Ijumaa, Jumamosi na Jumapili) itakuwa safi zaidi. Kwa mfano Samaki Samaki ni brand lakini mbali na samaki, pia anauza kila kitu. Halkadhalika Cape Town Fish Market anauza hadi pork (Sina nia ya kuwa na kitimoto though) ingawa jina lake limejieleza lipo kisamaki zaidi. Kwenye hivyo vyakula vengine pia nazingatia mawazo yako.
Naendelea kupokea ushauri na I hope ndani ya wiki 2 nikafanye survey kwa sababu kwa mfano nyama choma almost kila pub/bar zinakuwepo kwaiyo nitajaribu kuangalia namna gani wanafanya ili nifanye kilicho bora zaidi. Halkadhalika kwenye vyakula vya kawaida kama ugali, wali na local foods nyengine.
Natanguliza shukrani.
Nimekusoma mkuu, kila la kheri
 
Nashkuru sana kwa ushauri.
Samahani, unafkiri kwa maeneo ya Kinondoni na viunga vyake biashara ya biriani haiwezi kuwa yenye mafanikio zaidi ya biashara ya mishkaki ya kuku?
Biriani ni chakula kizuri na nichakula pendwa hasa siku za ijumaa ukiweka mambo vizuri watu wanafuata kile kilicho bora. Usikate tamaa kwenye ushindani na Muamini sana Mungu wako
 
Asante sana kwa maua na pia kwa ushauri na nimekuelewa vyema. Nafkiria nikiweka huo mgahawa basi kitu “biriani” iwe ndio brand kwaiyo ningetamani iwepo siku zaidi ya moja, ikiwepo walau siku 3 ndani ya wiki (Ijumaa, Jumamosi na Jumapili) itakuwa safi zaidi. Kwa mfano Samaki Samaki ni brand lakini mbali na samaki, pia anauza kila kitu. Halkadhalika Cape Town Fish Market anauza hadi pork (Sina nia ya kuwa na kitimoto though) ingawa jina lake limejieleza lipo kisamaki zaidi. Kwenye hivyo vyakula vengine pia nazingatia mawazo yako.
Naendelea kupokea ushauri na I hope ndani ya wiki 2 nikafanye survey kwa sababu kwa mfano nyama choma almost kila pub/bar zinakuwepo kwaiyo nitajaribu kuangalia namna gani wanafanya ili nifanye kilicho bora zaidi. Halkadhalika kwenye vyakula vya kawaida kama ugali, wali na local foods nyengine.
Natanguliza shukrani.
Naipenda sana hii kazi ya chakula, hata hapa nilipo kuna vulnerability kubwa sana katika industry hiyo, in short watu ni kama wanachemsha chakula wanauza, hakuna hata siku 1 nimekula nikisema naam nimepata standard ya chakula kinachopendwa na kila mtu

ila tatizo kwangu Mimi kwenye suala hilo ni kama morinyo(yaani sjui kupika) sasa naogopa sana unaweza mpa mtu mawazo mazuri mazuri ambae ndio atakuwa mtaalam(chef) project yako umuombe mamba(The Quality & standard product) ila baada ya execution anakuletea kenge au mjusi mamba hahaha

ila kwa miji yote inayokuwa kwakeli kuna hii vulnerability hivyo kwa mtu anaeweza kuleta Quality na standard kwenye chakula bila kujali kwa aina gani kama ana capital basi aingie, in fact mama zetu(mama lishe) wengi wa huku miji midogo kama goba, Madale, tegeta na kwingeneko ukweli ni kwamba wanafanya kwa mazoea sana ukiwa fund na ukiwa serious unafanya kazi

Kuna watu wengi sana nikiwemo Mimi tunakula kwa hawa wamama sometimes kwasababu tu mazingira haya hamna mtu anaetua Huduma nzuri kuliko wao

Binafsi kwenye jambo hilo Mimi ni mbaguzi sana, naangalia kuanzia meza yako, kiti mpaka sahani yako kwa nje ipo vipi, chakula cha majumbani kwa watu huwa sifanyi hivi ila hivi vinavyouzwa basi kiukweli nakuwaga hivi sana
 
1694252368431.png
Nilikuwa nasikia tu biliani biliani, ... ile nakuja kukutana na hiyo biliani sasaa ... yaani ni mamichele tu kama michele mingine ... afadhali hata pilau tena BHAHEBHU!
 
Wabongo wanajua biryani ni ijumaa tu,sa itakuwaje?
 
Biashara ya chakula,yenye usafi,ubunifu na mapishi mazuri haijawah mkataa mtu….zingatia location,Jipe muda ijijenge na kujitangaza
 
Mkuu wazo zuri, na nikupongeze kwa ujasiri wako wa kuacha ajira ili kujiajiri, pokea maua yako, ni wachache sana wanaweza hili...

Kwanza kuhusu mgahawa ku deal na aina mbili za vyakula ( Biriani na pilau ) Naona kijiwe( mgahawa) utafifia kwa namna fulani, kwasababu...

Biriani ni aina ya chakula chenye viungo vingi sana, huwezi kufululiza kula kila siku lazima tu utakinai... yaani vile viungo ndio vitakukinaisha au utapoteza hamu ya hiko chakula.

Chakula aina ya biriani kinafaa kuliwa mara moja moja sana kutokana na uwingi wa viungo vyake, kwaicho ukifululiza kuuza biriani kila siku, kuna asilimia nyingi za chakula kubaki.

Ushauri wangu, mgahawa wako usi base kwenye biriani na pilau tu, Weka vyakula vyakula vyote vya kiswahili na jitahidi kuwa m'bunifu.

Mfano : ugali unaweza kuweka na mboga kama dagaa, kisamvu cha karanga, matembele, maharage yaliyoungwa nazi, samaki / kuku / maini / nyama choma ( kimoja wapo kati ya hivyo ) bila kusahau na mrenda.

Wali mzuri wa mafuta uliotiwa nazi na mboga mboga nyengine zenye ladha.

Hivyo biriani na pilau ni extras tu maana hapa katikati ya week watu hawatakua na mzuka navyo kama nilivyokwambia biriani inakinaisha.

Zingatio : Jitahidi sana kua mbunifu jikoni, hakikisha kinatoka chakula chenye ladha / kitamu sana.

Mwisho : Ukitaka kufanikiwa kwenye hii biashara cheza sana na social media hasa Instagram, inabidi uwe mtundu hasa wa kuandaa contents, kuandika captions zenye mtiririko mzuri unaovutia na usio chosha n.k

Naamini utafanikiwa, kila la kheri kwenye safari yako. Kwakua mimi naishi kinondoni, nitakua mteja wako wa kudumu.
Umemaliza kila kitu mkuu
 
Naipenda sana hii kazi ya chakula, hata hapa nilipo kuna vulnerability kubwa sana katika industry hiyo, in short watu ni kama wanachemsha chakula wanauza, hakuna hata siku 1 nimekula nikisema naam nimepata standard ya chakula kinachopendwa na kila mtu

ila tatizo kwangu Mimi kwenye suala hilo ni kama morinyo(yaani sjui kupika) sasa naogopa sana unaweza mpa mtu mawazo mazuri mazuri ambae ndio atakuwa mtaalam(chef) project yako umuombe mamba(The Quality & standard product) ila baada ya execution anakuletea kenge au mjusi mamba hahaha

ila kwa miji yote inayokuwa kwakeli kuna hii vulnerability hivyo kwa mtu anaeweza kuleta Quality na standard kwenye chakula bila kujali kwa aina gani kama ana capital basi aingie, in fact mama zetu(mama lishe) wengi wa huku miji midogo kama goba, Madale, tegeta na kwingeneko ukweli ni kwamba wanafanya kwa mazoea sana ukiwa fund na ukiwa serious unafanya kazi

Kuna watu wengi sana nikiwemo Mimi tunakula kwa hawa wamama sometimes kwasababu tu mazingira haya hamna mtu anaetua Huduma nzuri kuliko wao

Binafsi kwenye jambo hilo Mimi ni mbaguzi sana, naangalia kuanzia meza yako, kiti mpaka sahani yako kwa nje ipo vipi, chakula cha majumbani kwa watu huwa sifanyi hivi ila hivi vinavyouzwa basi kiukweli nakuwaga hivi sana
Nafkiri tumetofautiana kidogo.
Binafsi sikumbuki mara ya mwisho nilikula lini kwa mama ntilie kwa sababu ya kuchagua sana chakula kutokana na namna ya mapishi na mazingira ya kuanzia jiko, namna ya uandaaji, muandaaji wa chakula, mahali ninapotengewa chakula hadi vifaa na vyombo. Ikitokea nikila huona ni kheri niingie kwenye mgahawa nitumie hata 15,000/- kwa ajili ya wali samaki tu lakini nile hali ya kuwa nimeridhika. Bahati nzuri sina circle kubwa hapa mjini kwaiyo naweza kumaliza hata miezi sita bila kwenda nyumbani kwa mtu nikala chakula cha huko so kula kwangu zaidi ni nyumbani, na kama nakuwa na mizunguko mingi sana na kuspend muda mwingi nje ya nyumbani basi hutafuta mgahawa wenye kueleweka ninywe hata supu ya alfu 3 lakini sio kuingia kwa mama ntilie na kila wali maharage na mchuzi ambao naweza kula vijiko vitano nikaishia hapo.
 
Nafkiri tumetofautiana kidogo.
Binafsi sikumbuki mara ya mwisho nilikula lini kwa mama ntilie kwa sababu ya kuchagua sana chakula kutokana na namna ya mapishi na mazingira ya kuanzia jiko, namna ya uandaaji, muandaaji wa chakula, mahali ninapotengewa chakula hadi vifaa na vyombo. Ikitokea nikila huona ni kheri niingie kwenye mgahawa nitumie hata 15,000/- kwa ajili ya wali samaki tu lakini nile hali ya kuwa nimeridhika. Bahati nzuri sina circle kubwa hapa mjini kwaiyo naweza kumaliza hata miezi sita bila kwenda nyumbani kwa mtu nikala chakula cha huko so kula kwangu zaidi ni nyumbani, na kama nakuwa na mizunguko mingi sana na kuspend muda mwingi nje ya nyumbani basi hutafuta mgahawa wenye kueleweka ninywe hata supu ya alfu 3 lakini sio kuingia kwa mama ntilie na kila wali maharage na mchuzi ambao naweza kula vijiko vitano nikaishia hapo.
Basi nahisi utaenda kufanya vizuri sana pia nakutakia kheri nyingi sana katika hilo!
 
Itapendeza. Biriani isiwe dhana ya Chakula cha Kiislamu. Ipatikane kila siku.

Sehemu nyingi huuza Ijumaa, kama vile kishushio cha Swala..
Pale tanga kila ijumaa nilikuwa naenda sehemu moja hivi "Kwa HAMZA", walikuwa na biriana nzuri sana aiseeh.
 
Back
Top Bottom