Nataka kuingia Kariakoo kibiashara

Nataka kuingia Kariakoo kibiashara

Shirima nikisomaga comments zako napata picha ni mtu flani speed ya kuongea inasoma 70-80/120 sijui kwanini 😂😂😂
Over my dedi bodi! Kwanza sipo muongeaji sana na kigugumizi Cha mbaaali😁 nikiita jina lako

Dedededepl Sasa Kwa hali hyo ntakua comfortable kwel
 
Over my dedi bodi! Kwanza sipo muongeaji sana na kigugumizi Cha mbaaali😁 nikiita jina lako

Dedededepl Sasa Kwa hali hyo ntakua comfortable kwel
😂😂😂 sasa si unaanza kuongea fasta fasta pasipo kuita jina?
Tena nikizoom na hiyo avatar ndo basiiii unakuwa Shirima Mwijaku
 
Inapatikana kaka sema nyingi zina-range 800k mpaka 1.5M, kama huna haraka unalipia wakati ujenzi unaendelea mfano pale msimbazi B karibu na office za star times kuna ujenzi unaendelea unaongea na wahusika unatia pesa kabla hapajaanza kugombaniwa au pale karibu na sandaland Kuna ujenzi umeanza unalipia mapema hii wanafanya wale ambao hawana haraka na hawataki frame za ndani
Shukrani sana mkuu
 
ni kweli akiwa na mzigo mzuri na connection ya wateja sio mwenzetu miezi kadhaa tuu cha msingi connection hio hujengwa kwa uaminifu wako kwa wateja na mjiuze mzigo mzuri unaokimbia ili akimbize arudi kwako mapema nae atawaambia wenzake watajileta ukifanya hivyo kwa wateja watano kila mteja atakuletea mteja.
Hapo penye connection nzuri ndio uchawi unahusikaga
 
Bora ukaanzia kwenye meza ukakomaa ukausoma mchezo.

Ukayajua machimbo

Ukajua ABC watu wanasavaivu vipi kibiashara pale kariakoo.

At the same time ukawa unapata faida

Kuna mama Mimi namjua alikuwa na kimeza tu Leo Yuko kwenge fremu.

Anza huko

Ukiingia full msuli unaweza chanika msamba
 
Sema kariakoo watu Wana MAWE aisee!!! [emoji15][emoji15][emoji15]

Juzi kati nilikuwa hapo K/KOO natengeneza PC yangu kwa fundi mmoja kwenye kauchochoro kwenye haya maghorofa ya NHC.

Pembeni yangu alikaa mzee mmoja kavaa kawaida sana Wala sikumzingatia.

Mimi nilikuwa bize na mafundi wa Pc wakanipiga 30k Of ikapona.

Wakaja wadada wengine wawili wameleta mashine yao wakapigwa 40k matengenezo.

Sijakaa vizuri akatoka sista mmoja muonekano wa tomboy. Kavaa jinzi bwanga, tisheti KUBWAA!! na kasokota virasta kichwani. Mwendo wake wa kigumu sio kidada dada. Amevaa vile vibegi vya kiunoni kama vya diamond wanawekea simu sijui Hela.

Sasa akaja hadi kwa yule mzee ambaye sikumzingatia.

Sasa nahisi yule mzee kama sio mmiliki wa frem, meza, basi mganga yule [emoji2].

Sista akafungua zipu ya kile kibegi atakoa BURUNGUTU la Hela aisee Mimi mimacho kodoo!!! [emoji15].

Akahesabu fasta fasta kama teller wa benki wanavyojidai na Hela za watu, akampa mzee yule. Wakapiga stori mbili tatu, akaishia.

Nikasema tu huyu sista atakuwa na biziness yenye ujazo wa ukwasi hapa kati. At the same nikajionea huruma.

Kariakoo usimdharua hata wale wanatandaza biashara chini. Wanagonga Hela kuliko mtumishi wa umma wa huko TAMISENGA.
 
Back
Top Bottom