Nataka kukopa Shilingi milioni 5 nianze biashara

Nataka kukopa Shilingi milioni 5 nianze biashara

Utakatwa mpaka unye awamu hii sio ya kuchukua mikopo eti uanze biashara.HUKU MTAANI HAKUNA BIASHARA INAYOENDA HASWA MPYA. UTAANZA KUPOKEA MSHAHARA KIMINI HADI HAMU YA KAZI IKUTOKE.
Na mm naliofia hilo, japo nilikuwa na mkopo wa miaka miwil ambao nili uwekeza kwenye kilimoo, nilifanikiwa japo sio kama nilivotegemeaa sasa nilitaka nibadilishe biashara kdgo
 
Bisahara ya mahitaji ya nyumban kwa hapo ulipo sema iyunga ni sawa ila unatakiwa utoke uingie njia ya kwenda chuo cha must au njia ya kwenda iyunga secondary haya maeneo bado yanihitaji hiyo huduma kwa wingi

Maana hapo weng wamefungua mitaa ya stand na hapo kwenye soko lao lakini ukitoka nje kidogo huduma hamna

Wekeza hasara ni sehemu ya darasa

Faida ni sehemu ya ukomavu wa ubunifu wako
 
Habari yako.
Kwanza nianze kwa kukupongeza Mwalimu kwa mawazo ya kujikwamua kwenye rat race ambayo yatakupelekea uwe na financially freedom.Unajuwa kuishi kwa kutegemea mshahara tu ni utumwa sana na hakuna aliyefanikiwa na kuishi atakavyo kwa kuangalia chanzo kimoja cha pesa(especially salary)

Nimependa sana akili yako inavyokubali challenge kwa baadhi ya watu kupitia maoni Yao. Wazo lako si baya Kama umelifanyia uchunguzi weka imani,jiamini alafu ingia field uanze kazi/Biashara.
Dunia ya leo Kuna watu wengi sana wana mawazo mazuri ya Biashara ila niwachache wanao ingia Katika ulimwengu wa business,hii maana yake ni nini-Ni kuwa na mawazo mazuri ya Biashara pekee haitoshi inahitaji uwe na boldness (ujasiri) ili uanze Biashara.
Umefanya vizuri kuleta wazo lako hapa ili kulipa challenge lakini Katika Dunia ya leo haupaswi kumwambia kila mtu wazo lako la Biashara ili kuepeka negative mind.

Ngoja nikupe short story kuhusu safari yangu ya Biashara.
Mimi ni kijana nina miaka 27 nilimaliza chuo mwaka 2014.Nakumbuka kipindi bado nipo chuo wakati tumepata boom niliwaza ile pesa nitoa kiasi alafu nianzishe Biashara yoyote ile.Kwa kuwa sikutoka Katika familia ya Biashara hivyo nilikuwa sina uzoefu wa Biashara lakini kitu pekee nilichokuwa nacho ni dream.

One of my friends nilimpa wazo langu kuwa nataka nianzishe Biashara tena Biashara ya kutoa huduma ya saloon ya kiume.Rafiki yangu yule Siwezi kumsahau alianza kunikosoa na kuponda wazo langu la Biashara kuwa si zuri haliwezi ku work katika ulimwengu wa Biashara.
Alinipa sababu nyingi sana kama wanavyokupa wewe baadhi ya wachangiaji hapo juu tena zile sababu ambazo unaona ni muhimu kabisa.
Lakini kwa kuwa nilijiamini Basi nilifungua saloon yangu ya kwanza ya kawaida tu mwaka 2012.

Hadi leo ninapoandaki hapa ni jumla ya saloon 3 za kiume na moja ya kike.
Hakuna Biashara mbaya ndugu kama utakuwa una lenga kutatua changamoto fulani fulani katika jamii unayoishi.Leo yule rafiki zangu ambao walikuwa wanaponda wazo langu ndo wamekuwa wananipongeza kila siku kuhusu mafanikio yangu.

Nataka kusema nini,Uli ufanikiwe katika Biashara inatakiwa kwanza ujiamini.
Fanyia kazi wazo lako naamini utafanikiwa.

Nitakuja kuandika kwanini Biashara nyingi za wafanyakazi hazifanikiwa na kupendeza hatua gani unapaswa kuchukua ili usiwe miongoni mwao.
Asante
Wewe mtoa mada msome huyu hapa.
 
Mkuu nakushauli kopa maana malengo unayo ww tu mwenyewe na uoga wako ndo umasikini wako ,na ukikwama Leo hii Mimi sitakusaidia kabisa chochote kile na ukiendelea ni faida kwako na familia na nchi pia na pia ni kugundua changamoto tunazopitia wafanyabiashara mbalimbali kwa kila siku mkuu , chukua maamuzi sahihi .
 
Kama Kweli Una Nia Ya Mafanikio Wekeza Kwenye Biashara Yangu ( Parnership ) Kwa Kuwa Utakuwa Kwenye Makaratasi Yote Kisheria Na Utajua Kila Kinachoendelea Kwenye Kampuni.

Biashara Ya Mahitaji Ya Majumbani Ni Za Kizamani Na Hazina Mwendeldzo Na Hazifai Kabisa Kwa Kijana Anaefikiria Kwa Karne Ya 21.

Ukiwekeza 10 Milioni Kuna Uwezekano Kabisa Wa Kuzalisha Mpaka Milioni 1 Kwa Mwezi Wakati Kwa Duka La Kawaida Huwezi Kupata.

Kumbuka Ukikopa 10M NMB Utakuwa Ukikatwa 253,000 Kila Mwezi Kwa Miaka 5 Na Kwa Kuwa Mshahara Wako Ni Tsh 353,000 Utcakiwa Na Nini Kwa Kuishi Miaka 5 Ijayo ?

Kama Kweli Una Nia Ya Kutoka Kimaisha, Wekeza Kwangu Na Kampuni Itakuwa Inalipa Mkopo Wako Wakati Wewe Ukiwa Aidha Na Kipato Kile Kile Pamoja Na Umiliki Wa Kampuni Au Zaidi.

Ila Duka La Mazaga Tena Kwa Kumweka Mtu, Utajuta Kwa Miaka 5 Ijayo.
Kuna mtu atatapeliwa hapa
 
Kama Kweli Una Nia Ya Mafanikio Wekeza Kwenye Biashara Yangu ( Parnership ) Kwa Kuwa Utakuwa Kwenye Makaratasi Yote Kisheria Na Utajua Kila Kinachoendelea Kwenye Kampuni.

Biashara Ya Mahitaji Ya Majumbani Ni Za Kizamani Na Hazina Mwendeldzo Na Hazifai Kabisa Kwa Kijana Anaefikiria Kwa Karne Ya 21.

Ukiwekeza 10 Milioni Kuna Uwezekano Kabisa Wa Kuzalisha Mpaka Milioni 1 Kwa Mwezi Wakati Kwa Duka La Kawaida Huwezi Kupata.

Kumbuka Ukikopa 10M NMB Utakuwa Ukikatwa 253,000 Kila Mwezi Kwa Miaka 5 Na Kwa Kuwa Mshahara Wako Ni Tsh 353,000 Utcakiwa Na Nini Kwa Kuishi Miaka 5 Ijayo ?

Kama Kweli Una Nia Ya Kutoka Kimaisha, Wekeza Kwangu Na Kampuni Itakuwa Inalipa Mkopo Wako Wakati Wewe Ukiwa Aidha Na Kipato Kile Kile Pamoja Na Umiliki Wa Kampuni Au Zaidi.

Ila Duka La Mazaga Tena Kwa Kumweka Mtu, Utajuta Kwa Miaka 5 Ijayo.

Mkaruka!! Kampuni yako inaitwaje...? Pertinership?!! Please advise... Nina ka milioni 4 kananisumbua. Sijawahi kufanya biashara yeyote. Nafikiria nifanye nini? Naomba ushauri jinsi ya kuwekeza kwani hii ndio pesa pekee niliyobaki nayo....
 
Mkaruka!! Kampuni yako inaitwaje...? Pertinership?!! Please advise... Nina ka milioni 4 kananisumbua. Sijawahi kufanya biashara yeyote. Nafikiria nifanye nini? Naomba ushauri jinsi ya kuwekeza kwani hii ndio pesa pekee niliyobaki nayo....
Uko Wapi ?
 
Duu, pamoja na riba ntarudisha kama 6.2 mil kwa miaka miwil na nusu,

Nifanyeje sasa mana mshahara naona tu haunitoshi zaid ya kunifanya niwe nasubr sms ya nmb kila mwisho mwez ili nilipe maden
Kulingana na take home yako naona utakua unakatwa hela nyingi kwanini usianze na mtaji mdogo? Ungekua unaendeleza biashara sawa ila kwa kuanza tu na kukopa Tena bank sikushauri sana ni Bora ukaweka kidogo kidogo sakosi au fixed account then Kama ni duka la mahitaji ya nyumbani waweza anza hata na milioni moja ukiona Mambo mazuri waweza kopa sasa uongeze mtaji.In investment usitangulize miguu yote Kwanza nionavyo Mimi
 
Mkuu mwenyew nipo kwenye mchakato Wa kukopa bank ila nakopa ili kuboresha biashara sio kuanza biashara huenda una plan nzur ila biashara kwa sasa ngumu Sana + kodi za mkuu sikushauri ukope utajutia tena ndio wakopa kueka mtu kilio utacholia sio cha nchi hii
 
Kulingana na take home yako naona utakua unakatwa hela nyingi kwanini usianze na mtaji mdogo? Ungekua unaendeleza biashara sawa ila kwa kuanza tu na kukopa Tena bank sikushauri sana ni Bora ukaweka kidogo kidogo sakosi au fixed account then Kama ni duka la mahitaji ya nyumbani waweza anza hata na milioni moja ukiona Mambo mazuri waweza kopa sasa uongeze mtaji.In investment usitangulize miguu yote Kwanza nionavyo Mimi
Nashukuru mkuu nafanyia kaz ushaur wakoo
 
Mkuu mwenyew nipo kwenye mchakato Wa kukopa bank ila nakopa ili kuboresha biashara sio kuanza biashara huenda una plan nzur ila biashara kwa sasa ngumu Sana + kodi za mkuu sikushauri ukope utajutia tena ndio wakopa kueka mtu kilio utacholia sio cha nchi hii
Duu nalo linaniumiza kichwa sana mchagger ngoja niendelee kuchaka akil, na ndo maana nikaomba ushaur kabla ya kuanza kufanya
 
Back
Top Bottom