Nataka kukopa trekta kwa kilimo na kazi ndogo

Nataka kukopa trekta kwa kilimo na kazi ndogo

ushauri wangu kwako na kwenu wote mnaotaka kununua au kukopa tractor based on my experience, msichukue trekta kwa minajili ya kukodisha au kufanyia kaz za watu haijakaa vzr utalichosha mapema na inaweza isikulipe zaid ya kukupa unnecessary stress. Sbb wakulima wengi wanamiliki mashamba chini ya eka 3. Mara nyingi utajikuta ili ulime eka nyingi lazima utembee na tractor umbali mrefu na muda mwingi utajikuta unalitembeza trekta kwny njia mbovu ambayo nayo yana udongo/ardhi tofauti tofauti ngumu, laini, yenye mawe nk. Lkn pia trekta ni mashine haijatengenezwa kutembea tembea barabarani tena mbovu. Haya yote kwa ujumla wake yanalichosha trekta ila kama unashamba kubwa chukua trekta tumia kwa kazi zako. Na amini with proper management unaweza kukopa ilo trekta kama una 30 acres
Asante kwa ushauri.Niliambiwa hili pia na akashauri nilime eneo langu la kutosha na labda kubeba Mizigo
 
Utafilisika unless uwe unatumia kwa kazi zako binafsi za shamba ili kuongeza productivity yako. Na hivi utakuwa mbali ndiyo kabisa, wabongo hawaogopi mambo za GPS etc.
Noted...kuna mtu alinitahadharisha pia
 
Mkuu wajaribu na bank ya kilimo nasikia wana mikopo rafiki sana kwa wakulima serious

Kuhusu mradi wako kuna changamoto mbili

Mosi, Hakikisha trekta linazalisha zaidi shambani kwako na kukodisha iwe ni ziada na sio kukodisha ndio msingi na shamba lako ziada

Pili, Kuwa mbali na mradi nayo ni changamoto sana aisee
Wabongo sijui nani katuroga, uaminifu kwetu ni sifuri
Trekta litapigishwa kazi balaa za kukodi mwaka tu limechoka
Ni vizuri ukawepo mwenyewe au mtu wa kuaminika sana sana sana
 
Juzi juzi nilisikia watu wanalia wamekopa trekta feki baada ya mwezi spana mkononi na deni bado bichi. Kesi iko mahakamani sijui kwa mkuu wa mkoa
 
Wadau nafikiria nikope trekta la HP 35 ambalo talitumia kulima ekari zangu 50 na chache za majirani.Baada ya hapo nitakutumia kubebea mazao na vifaa vya ujenzi kwa maana ya kulikodisha.

Nitalifunga GPS maana nitakuwa nalo mbali.

Trekta na tela lake ni TZS 33m ambapo nitalipa kama 13m za kuanzia na zilizobakia nitarejesha kwa miezi 18.

Nataraji nikiuza mazao nitakayolima na makusanyo nimalize deni. Kadi watabaki nayo benki na nitakata bima kubwa.
Kama huna mpango WA kukaa nalo karibu sikushauri.. Kuna kuiba mafuta, Kuna kuiba spea Kwa kifupi binadamu wengi uaminifu Ni zeroooooo utalia mkuu labda dereva awe mwanao[emoji55]‍[emoji2418]
 
Hiyo mosi ndio msingi.Ifakara wakulima wakubwa wakimaliza wanayafungia ndani
 
Wadau nafikiria nikope trekta la HP 35 ambalo talitumia kulima ekari zangu 50 na chache za majirani.Baada ya hapo nitakutumia kubebea mazao na vifaa vya ujenzi kwa maana ya kulikodisha.

Nitalifunga GPS maana nitakuwa nalo mbali.

Trekta na tela lake ni TZS 33m ambapo nitalipa kama 13m za kuanzia na zilizobakia nitarejesha kwa miezi 18.

Nataraji nikiuza mazao nitakayolima na makusanyo nimalize deni. Kadi watabaki nayo benki na nitakata bima kubwa.
Tena sasa hivi kwa BBT, unapewa kwa mkopo laini sana. Nenda benki zilizo kwenye mpango wa BBT.

Kuna namba wameweka wizara ya kilimo ya kutowa msaada.
.siku hizi wizara ya kilimo kuna customer care, mambo ya Bashe na mama Samia hayo.
 
Jipya sh ngapi? Na used sh ngapi Kwa new Holland
 
Tena sasa hivi kwa BBT, unapewa kwa mkopo laini sana. Nenda benki zilizo kwenye mpango wa BBT.

Kuna namba wameweka wizara ya kilimo ya kutowa msaada.
.siku hizi wizara ya kilimo kuna customer care, mambo ya Bashe na mama Samia hayo.

BBT ndio nini ?
 
Mkuu hiyo aina gani ya trekta na unachukulia wapi?, nami ni ishu ambayo inanisumpua kichwa changu sana, lakini watu wananitisha kwamba trekta litakupa hasara tu.
Of course hawakuambii uongo. Kitu chochote kama huja-plan kwa umakini unapata hasara tupu. Kama unatishika na maneno ya watu inaonekana kabisa hujafanya research ya kutosha kuhusu hilo suala.
 
Jipya sh ngapi? Na used sh ngapi Kwa new Holland
New holland tt75 4wd mpya ni milioni karibia 59 bila jembe.

Used new holland tt75 4wd ambayo ipo katika hali nzuri ya kupiga kazi bila service kubwa ni kati ya milioni 24 na kuendelea huko
 
Mkuu angalia trekta linalotengenezeka, kuna trekta kupata spea ni ishu.
 
New holland tt75 4wd mpya ni milioni karibia 59 bila jembe.

Used new holland tt75 4wd ambayo ipo katika hali nzuri ya kupiga kazi bila service kubwa ni kati ya milioni 24 na kuendelea huko
Je tt 55 zinakuwa na bei gani kwa used na kwa mpya.
 
Waheshimiwa kwenye trekta used bei sio kigezo cha kuzingatia sana. Jambo la msingi kabisa la kuzingatia ni uzima wa hilo trekta. Unaweza ukauziwa trekta kubwa lenye 4wd hp kuanzia 75 na kuendelea kwa mteremko ukadhani umeokota dodo.

Kumbe lina matatizo kuliko hata neno matatizo lenyewe. Lazima trekta used ulikague saana. Kama huna uzoefu wa kukagua, tafuta fundi mzuri mwaminifu na mlipe posho nzuri akukagulie chuma. Pia zingatia sana maamuzi binafsi, ukiona chuma hujaridhika nalo achana nalo na uendelee kutafuta.
 
Mkuu shukurani sana kwa maelezo yako, naomba kuuliza tena, je ni vitu gani ambavyo fundi anatakiwa kuvizingatia wakati wa ukaguzi wa tractor used?
 
Mkuu hiyo aina gani ya trekta na unachukulia wapi?, nami ni ishu ambayo inanisumpua kichwa changu sana, lakini watu wananitisha kwamba trekta litakupa hasara tu.
Trekta ukiiweka sehemu yenye uhitaji utapasua labda uwe mbali
 
Back
Top Bottom