Nataka kumpeleka binti yangu(Mkristo) kwenye seminary ya kiislamu iliyopo Dar (wanasoma day). Je, ipi ambayo haina masharti ya kutaka awe muislamu?

Bongotunacheza

JF-Expert Member
Joined
Dec 7, 2018
Posts
983
Reaction score
2,306
Naombeni msaada tafadhali.

Je nitapata seminari ya kiislamu inayo FANYA vizuri ambayo huyu mtoto ataenda kusoma bila kulazimika kuwa muislamu? Mfano kutakiwa kuswali, kujifunza koroani etc.

Mambo mengine yote atafuata kama mavazi na sheria nyinginezo za shule?.ushauri wenu tafadhali. Iwe dsm wilaya ya kinondoni
 
Unapeleka mtoto kwenye shule zinazofanya vibaya kwenye mitihani ya kitaifa kwani huoni shule zisizofungamana na imani za kidini? Shule zenyewe ni kero hata kwa walimu wasioamini itikadi hiyo hutakiwa wavae kiitikadi yao mpaka wengine huacha kazi na kubaki wa itikadi yao wasio na uwezo wa kufundisha. Kuna shule za imani fulani zenyewe hazijali mtu awe wa imani yao au nyingine zinajali uwezo wa mtu tu ndio maana zinafanya vizuri. Hizi zenye ukiritimba wa imani za dini zinatisha
 

Doh! Kwa mara ya kwanza nimesikia mzazi mkristo anapeleka mtoto wake shule ya kiislam!
Samahani najua kuna kinondoni muslim unaweza kumpeleka lakini je nini kimekuvutia?
 
Inaitwaje hiyo seminary tuone matokeo yao?
 
Zinazofanya vizuri kwenye nini hujaweka wazi, kama ni taaluma hamna, labda kama unataka akajifunze elimu ya dini
 
Doh! Kwa mara ya kwanza nimesikia mzazi mkristo anapeleka mtoto wake shule ya kiislam!
Samahani najua kuna kinondoni muslim unaweza kumpeleka lakini je nini kimekuvutia?
Lengo lake siyo shule, Bali matusi yaanze kumiminika.
 
mpeleke lakni ufuate mashariti yao
 
Doh! Kwa mara ya kwanza nimesikia mzazi mkristo anapeleka mtoto wake shule ya kiislam!
Samahani najua kuna kinondoni muslim unaweza kumpeleka lakini je nini kimekuvutia?
hiyo shule ya kinondoni haina ubagazi hata msalba shingoni rukhusa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…