Nataka kuoa wapendwa

Nataka kuoa wapendwa

Bin Shaib

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2019
Posts
1,346
Reaction score
1,221
Habari wapendwa mimi kijana ambaye ni mwenye umri wa miaka 25 kwa sasa,si mtu ambae nilipenda kudinya dinya katika maisha yangu,,kwa sasa nataka nioe lakini bado sijapata mtu sahihi wa kuingia nae kwenye ndoa,japo kuna wasichana kama wawili hivi ambao wanataka ndoa na mimi.

Kati ya hao nimemchunguza mmoja mwenendo wake kama nahisi anafaa lakini sijamuamini sana maana wanawake hawajulikani wanataka nini, unashangaa anaingia ndoani anabadilika unaanza kujuta.

Maana huyu kipindi nipo nae kwenye mahusiano nilikuwa simpi hela yaani hadi nipende mimi alivumilia nakuniaminisha kuwa ananipenda nakunambia nikiwa sina hela ya kumpa njsiwaze ,,namimi sio kwamba hela ndogo ndogo sikuwa nazo,ila nilifanya kumpima,

lakini baadae kidogo nilianza kuona ameanza mabadiliko,dharau zikaanza hata ukimwita kimazungumzo anachukulia poa, akaanza visa mara mimi natembea na msichana ambae alikuwepo pale mtaani, baada yakuona dharau zimezidi nikamuita kisitaarabu tu nikamwambia naomba kila mtu ajue maisha yake.

Kwa sasa unaelekea mwezi sasa toka tumeachana na huyu ambae nilimdhania atakuwa wife wangu maana hadi kufanya mapenzi alikataa hadi tuingie ndoani.

Naona aninyemelae full kunichangamkia mara aniambie nikamtembelee kwao wakati zamani alikuwa akanizuia nisiende kwao.

kipindi cha nyuma alituma mtu ili kuniomba msamaha ili nimsamehe japo hizo taarifa sikuzipata kiundan.

Nahsi nikimurudia huyu labda naweza juta baadae? Maana nisha move on.

Jamani wapendwa muniombee nipo natafuta mke ambae atakuwa wakunana na mimi atakae nivumilia kwa hali zote katika mapito ya dunia na japo mapenzi ya sasa ni magumu mimi naomba nimpate mwenye mapenzi ya dhati.

Umri wa kuoa umefika nataka nioe na majukumu magetoni yamenizidia nahitaji msaidizi,natoka mishe zangu nimechoka hadi nalala bila kula hata kuoga pia naamini kama kuna msaidizi mambo yanakuwa poa.

NB:Mimi ni mkiristo nimemwamini Yesu nakumpa maisha yangu, nimlokole halisi.

Asanteni kwa kusoma uzi wangu,, nawatakia ushauri mwema juu ya maamzi yangu ya kuoa..

Bin Shaib Classic 2020.
 
Kila la heri kwenye jambo unalotaka kufanya ila hautomlaza mtoto wa watu njaa kweli? Unalalaje bila kula na kazi unafanya kisa tu huna wa kukupikia, mkuu hapa unatafuta wa kukupikia.

Asante, Kulala njaa kwangu ni ile hali yakufika nimechoka nashindwa kupika,, maana nafika muda mwingine saa 4 usiku,,unakuta kila kitu kipo ila uvivu wa kupika huwa naamua kula matunda tu nalala.
 
Hizi ndoa huwa mnazichukuliaje kwani? Mbona limefanywa kuwa jambo rahisi rahisi hivi?


Let's meet at the top, cheers 🍻
 
Hizi ndoa huwa mnazichukuliaje kwani? Mbona limefanywa kuwa jambo rahisi rahisi hivi?


Let's meet at the top, cheers 🍻

Kwani ni jambo gumu kivipi, maana ndoa iliyo na Mungu hakuna lisilo wezekana.
 
Njoo DM Kuna bint anAjielewa sana mtaan nazn utawezan nae ila uwe mkristo.
 
Njoo DM Kuna bint anAjielewa sana mtaan nazn utawezan nae ila uwe mkristo.
Mpaka sasa mi ni mlokole nasali kanisa la (T.A.G Tanzania Assemblies of God)
 
Back
Top Bottom