Nataka kuwa "Dalali" Nipeni Mbinu!

Usimzingue chalii yangu Aisee πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Principles
1. Chagua udalali unaotaka kuufanyia kazi ila ili upate kazi nyingi usichague sector piga kote kote i.e usafirishaji mizigo, kukodi mashine za ujenzi, uuzaji wa vitu mbali mbali etc

2. Pata information za kutosha juu ya kitu unacho dalalia

3. Usiweke cha juu kikubwa sana

4.ukipata namba ya mteja wa kwanza usifute

5. Uwe na mtaji ili mishe ikibuma fedha unarejesha itakujengea heshima

6. Sometimes ingia gharama zako kama itafaa ili kujenga trust

7. Simu zako mda wote ziwe zinasalio na bundle na chaji

8. Jitangaze kwenye mitandao ya jamii

9.usiwe mdhulumaji, madalali ni ndugu mwenzio akiwa na shida msaidie

10. Kuzungukana kwenye michongo sio ujanja

11.usiwe mkali kuwa na lugha ya tamu yenye matumaini

12.uwe mvumilivu

13. Ukipata hela fanyia kitu cha maana maana sometimes ishu huwa zinagoma hadi miezi 6

14. Kila la kheri
 
Dalali ni sawa na mwanasiasa! Jiandae kuwa muongo wa kiwango cha Phd afu tengeneza urafiki na police na andaa watu wa kuwa wanakudhamini mahakamani!
Madalali wachache sana waaminifu na ukiwa mwaminifu utafanikiwa sana maana mtaji ni mdomo tu na pesa inaingia kiulaini kabisa
 
utakuwa umejika ktk nafasi nzuri ya utapeli,angalizo uwe na kumbukumbu imara
 
mbinu ya kwanza madalali huwa hajakubali kushindwa, mteja akijileta ataoneshwa kila sehem ata kama hapamvutii kwa kuona, atavutiwa kwa maneno yako hadi atoe hela.
 
Udalali bahna ukijifanya una mshipa wa aibu hutoiweza hiyo kazi. udalali upo dizaini mbili, kutafutwa na wateja ama kutafuta wateja. Udalali upi labda unaotaka wewe [emoji52]
 
Kuna dalali wa magari
Kuna madalali wa nyumba,mashamba na viwanja
Kuna madalali wa kkoo,wao wanakaa mbele ya maduka mteja akikosa kitu wao wanakipata popote ndani ya dk chache tu
Kuna dalali wa madem
 
Asante sana Mkuu, Nimekuelewa sana ila Hapo Penye wekundu nieleweshe zaidi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…