Nataka nichukue mkopo ninunue mabasi ya mikoani

Mbona milioni 500 ni kidogo sio lazima Bank kuu hata CRDB wanatoa ilimradi umekamilisha vigezo, ila pia kiasi hicho cha pesa labda ununue TATA sio basi la mkoani maana mpaka linaanza safari sio chini ya milioni 580 huko na hilo ni moja....zaidi ya basi moja fikiria kuomba zaidi ya billion moja
 
Tafuta mashine ya kudarizi ata vichwa viwili.
Wewe dili na kudarizi tisheti za vikundi na tasisi za kidini tu

Au unaongeza shule za privet tu.
 
Mkuu Biashara ya Mabasi Ina Stress nyingi ni DM nikwambie nko kwenye hyo Industry 😄😄😄Cha msingi sio kwamba nakutania nakwambia nachokiona kwa miakaZaid ya7
 
Hongera kwanza mkuu kwa kua na mawazo chanya
Ila nikukatishe tamaa ya kua hapa hutoweza kamwe kupata msaada wa kimawazo ambao utaleta tija katika maamuz utakayoamua kuchukua, platform hii sio kama zamani, wakat huu naona asilimia kubwa labda 80% kuna wahuni na wagonjwa wengi wa akili, maskini na wenye elimu ndogo na utawapata wengi kwenye mada zao za kipuuzi. Hizo 20% labda ndio watu walio na maarifa mengi ila sio waandikaji sana na hua wanapita tu kusoma na wakichangia ni mara chache sana, wewe tafufa wataalam zaid wanaoweza kukupa maarifa ama nenda katika hizo taasisi utafute appointment ya kuonana na wahusika naamin utasaidika kama una nia.
 
Duu kumbe elimu yako haijakusaidia nilitegemea hilo wazo lako ungelifanyia utafiti ili uligeuze liwe biashara, (market research analysis), baada ya kufanya utafiti uliandikie mpango wa biashara.

Mpango wa biashara unafanya makosa kwenye makaratasi badala ya kwenye eneo la biashara, kwakifupi mpango wa biashara, (business plan), unatafsiri wazo lako la biashara baada ya kuliangalia soko likoje kwa kuelewa wapinzani wako wanafanyaje biashara kwa maana hiyo biashara siyo mpya

Please write a competitive business plan,

Tafadhali andika mpango wa biashara ambao ni shindani kwa elimu uliyo nayo nitakushangaa kama huwezi kuandika mpango wa biashara
 
Hata bei ya mabasi hajui
 
Harafu ana degree ya bussness information
Anashindwa kupata information, (anashindwa kupata taarifa sahihi), huyu jamaa anatatizo amebobea kuhusu taarifa lakini hawezi kupata taarifa pia kasoma kuhusu biashara halafu hawezi kupata taarifa za biashara
 
Anashindwa kupata information, (anashindwa kupata taarifa sahihi)
Ili aweze kufanya biashara lazima apate taarifa na awe na uwezo mzuri wa kutafsiri taarifa, kwa maana anaweza akapata taarifa sahihi lakini akawa hana uwezo wa kutafsiri taarifa kwa usahihi, kwakifupi huyu jamaa hawezi kufanya biashara
 
Hakikisha unaenda kuyazindika vizuri HANDENI la sivyo ndani ya mwezi mmoja utaugua
 

Okay naona umendika na hii post ukiwa bado usingizini.ukiamka utaifuta.mkopo BOT?
 
Khaaaaa......nakushauri tafuta kazi utaacha kuota ndoto za ndotoni...safari ndefu sana....sio rahisi hivyo anza na boda boda kwanza....baada kupata kazi jichange nunua boda kwanza....
 
Sera ya bank zetu hasa commercial bank iko Ivi ili ukopesheke kuna vigezo wanavyozingatia, moja ya kigezo ni muombaji wa mkopo kuwa na “collateral” (dhamana) hii inaweza kuwa ardhi, nyumba n.k.

Baadhi ya nchi zilizoendelea mkopo unaweza kutolewa kwa kutazama na kupima wazo lako yani (business idea) kama kweli italeta output inayokusudiwa.

Aidha, binafsi ninakushauri utembelee tawi lolote la bank iliyo karibu na wewe ili uweze kuzungumza nao juu ya hutaji lako, ninaamini watakupa maelezo mazuri zaidi.

Pia kwa nature ya biashara zetu za kibongo kama una Dream ya kua mfanyabiashara mkubwa na unajua hauna inventory capital ya kutosha ANZA na kiasi ulicho nacho kwenye biashara unayo iweza kwa wakati huo kisha jipambanie kukua kibiashara ili badae utimize ile ndoto yako kubwa uliyo nayo ambayo kwa namna moja ama nyingine inahitaji mtaji mkubwa.

Mimi nitakuandikia business plan nzuri utani Dm.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…