Nataka nimchome kwa ndugu zake

Nataka nimchome kwa ndugu zake

Nina mchumba angu ambae sasa tuna miaka mitatu nikiwa nae ila mienendo yake inaanza kunitia wasiwasi sana na kuna vitu nimeshabaini kwake.

1. Kuna shemeji yake ambaye kamuoa dada yake mkubwa anamtaka na wana mawasiliano ya karibu hadi kamtumia kiasi cha pesa mara kadhaa jumla haiwezi kupungua laki mbili na wanakutana mara kadhaa na huwa haniambii mpaka nijue kwa jitihada zangu au mpaka dada yake amtukane kuhusu swala la kukutana na mme wake bila taarifa yeye kupata maana nahisi kama kahack simu ya mumewe.

2. Mara zote nikimuuliza kuhusu ili jambo anakua mkali sana na kufanya kama vile mimi simuamini ilihali anasema ukweli na mambo mengine mengi ambayo yananifanya nimchome kwa ndugu zake.

NB: Kuna mambo ambayo mimi nayajua mengi na nikimwambia dada yake lazima tu apo litokee jambo kubwa sasa nawaza apa nimchome ili kila mtu akose kila kitu maana mimi hilo nilikua nalisamehe ila bado kuna la ex wake kwaio nataka nimchome naombeni ushauri wenu wakuu.
Sasa mchumba wako analiwa na ww unachekelea? Au na wewe unataka kuukalia
 
Usiwe sababu ya kuvunja undugu wa watu, dhima yake ni kubwa sana kwa Mungu. Huyo binti si mkeo, usimuonee uchungu kiasi hicho. Shukuru Mungu umejua tabia zake mapema kabla kumfanya mke. Kama anaweza kulala na mume wa dada yake hatoshindwa kulala na kaka yako. Piga chini.

Kumbuka ukisanua unachojua athari haitokuwa kwake tu. Utavunja udugu wake na dada yake, utavunja ndoa ya dada yake na mumewe na pengine kuleta mtafaruku katika familia nzima. Sasa huoni kuwa utakuwa unaadhibu wasiokuwa na hatia.

Za mwizi daima ni 40, kama dada yake anajua kuna kukutana baina yake na shemeji yake basi ni swala la muda tu atawakamata na hapo hutokuwa na lawama yeyote hata wakiuana.
 
Back
Top Bottom