Niandike hapa historia ya mgonjwa, huoni naacha vielelezo vya kunitrace na kesho naokotwa kwenye kiroba? Kuna zama huko kwa wenzetu watu walikuwa wanaweka habari kama hizi kwenye chupa na kutupa mbali ili miaka mingi ijayo watu wasome yaliyotokea!Bila shaka hii ni chai ya jioni. Haiwezekani health worker ashindwe hata kuandika historia ya mgonjwa. Na pia haelewi/ameshindwa kusimamia muongozo wa kazi yake. Ameleta contradiction tupu mfano huyo mama alishindwa vipi kuhudhuria clinic kwa miezi yote 9?, alikuwa na mkataba wa aina gani?, alipata uchungu wa ghafla? Maswali ni mengi mengi
Bila shaka itakua ni Epza pale xtenal ubungo ktk kiwanda cha majinsi cha wachinaHebu taja hiko kiwanda asee... Wachina wanakera ila ww utakera zaidi na utakuwa hauna maana! Wahusika wapo humu watachukua hatua toa taarifa kamili hamna anaekujua na ndio lengo la JF
Mkuu ingekuwa Dar ambapo kuna health facilities nyingi ingekuwa nafuu kulinda usalama wangu, hapa nilipo kuna vituo vya kutolea huduma za afya 3 tu, watuhumiwa hao ambao wengi wanatetewa na watanzania wenzetu wenye pesa na madaraka ni rahisi kujua ni kituo gani kilitoa taarifa ya mama huyo, ila pia enzi hizi mh, angalau kuna kipindi watoa taarifa walikuwa wanakabidhiwa kwenye vyombo vya usalama viwalinde!Hicho kiwanda kinaitwaje na kipo wapi? Ukishindwa kukitaja wewe utakuwa ni muongo na mchonganishi.
Hakuna watu wanao tumikisha watanzania kinyanyasaji kama wachina, wachina ni makatili sana na hawajali utu.FUNGUKA MKUUKIWANDA GANI, KIKO WAPI.N.K!..KAMA HUWEZI KWENDA POLISI AMA DAWATI HUSIIKA HATA KUWEKA HAPA KILA KITU UNAOGOPA?
Mkuu mbona ameweka wazi hapo juu kwamba ukijifanya unapenda haki siku zako zinahesabika za kuishi ndiyo maana kaamua kuleta humu yaani katupa jiwe gizaniKuna matatizo ya kimfumo kwenye maswala ya safeguarding; sio kwenye afya sehemu nyingi tu zinazohusika na social services.
Health worker, walimu, ustawi wa jamii na taasisi zingine zinazotoa huduma za jamii hao wafanyakazi ni askari wa mbele kwa serikali kwenye kusimamia sheria, kupambana kupunguza maswala ya unyanyasaji kinyume na sheria na kadhalika.
Nchi za wenzetu frontline workers wana sign mkataba wa duty of care kuripoti mambo ambayo watakayoona ‘ndivyo sivyo’ ni jukumu lao na sehemu zingine unashitakiwa for negligence usipofanya ivyo mtu akapata madhara wakati wewe ulikuwa na information ambazo ukuzitoa watu wachunguze na kuchukua hatua.
Mtu anakutana na mjamzito anaona kabisa process zake za kumpatia huduma hazikuwa sahihi kutokana na restrictions za mwajiri wake ambazo ni kinyume cha sheria badala ya kupeleka concerns kwa wahusika anakuja hapa kulalamika sasa hayo matatizo yataisha vipi kama wenye mamlaka awapelekewi habari na watu wanaoshuhudia ili kuchunguza na kuchukua hatua.
Kipo external ubungo na kinahusika na kutengeneza majinsiHicho kiwanda kinaitwaje na kipo wapi? Ukishindwa kukitaja wewe utakuwa ni muongo na mchonganishi.
Ha ha kile chenye wafanyakazi 4000?Kipo external ubungo na kinahusika na kutengeneza majinsi
PM details za hao manyang'au tusaidiane kulifanyia kazi hilo la wacheiNipo kibaruani mchana wa leo (nimerudi kazini awamu ya sita baada kama nilivyohaidi), nimempokea mama na kichanga chake ambaye amejifungulia kazini kwenye kiwanda cha Mchina (sehemu sitaitaja) ila ni mazingira mabaya kujifungulia binadamu, mama hana kadi ya kliniki na bahati nzuri alikuja kuanza kliniki ijumaa saa kumi akakuta huduma zimeishafungwa (jiulize ilikuwaje mama aanze kliniki na mimba kubwa karibia na kujifungua, hii haihitaji akili kubwa bila shaka hakuna ruhusa kazini) kwahiyo zile huduma kama vipimo vya wingi wadamu, magonjwa ya zinaa na ukimwi nk. na hivyo maisha ya huyu mtoto yapo hatarini!
Jamaa waliomsindikiza kwenye tax huyu mama ni wanaume watatu hakuna jisia ya kike! Walipofika wakahudumiwa wakataka kulipia staff aliyekuwepo akasema huduma za mama na mtoto ni bure, na hapo waksema wanazo 200,000/ mchina kawapa kwa ajili ya matibabu ya huyu mama na wakasema anahitaji risiti, wakauliza kama tunaweza kufanya mbinu ili risiti ipatikane .....kwa ufupi hatukuwapa risiti na badala yake yule mama alipewa sh.40,000 hela iliyobaki wasema wanaenda kutafta namna ya kupata risiti...tuachane na mambo ya pesa maana mimi sio lengo langu la kuleta uzi hapa JF,
Kitendo cha huyu mama kutohudhulia kliniki, kujifungulia kazini, nk kinaleta picha ya kuwepo na manyanyaso kwenye hiki kiwanda, nilitamani huyu mama awe mfano kwa akina mama na watu wote wanaoteswa na kunyimwa haki zao makazini...nilitamani kuripoti unyama huu ila....HII NCHI WAPENDA HAKI HAWATAKIWI KABISA, ukiangalia kesi za wenye pesa kama wale wezi wa mafuta Kigamboni ambapo serikali wapo kimya, nk nikijifanya kuingia anga za hawa wachina wanaoshirikiana na watanzania wenzangu yanaweza kunikuta ya kunikuta na kubaki peke yangu na historia isinikumbuke!
Tuendelee kuangalia pingamizi lililowekwa kwa Diamond Platnumz aondolewe kwenye tuzo za BET maana hiki ndicho waliowengi miongoni mwetu tunaweza sana!
Ndiyo mkuuHa ha kile chenye wafanyakazi 4000?
uchumi wakatiNipo kibaruani mchana wa leo (nimerudi kazini awamu ya sita baada kama nilivyohaidi), nimempokea mama na kichanga chake ambaye amejifungulia kazini kwenye kiwanda cha Mchina (sehemu sitaitaja) ila ni mazingira mabaya kujifungulia binadamu, mama hana kadi ya kliniki na bahati nzuri alikuja kuanza kliniki ijumaa saa kumi akakuta huduma zimeishafungwa (jiulize ilikuwaje mama aanze kliniki na mimba kubwa karibia na kujifungua, hii haihitaji akili kubwa bila shaka hakuna ruhusa kazini) kwahiyo zile huduma kama vipimo vya wingi wadamu, magonjwa ya zinaa na ukimwi nk. na hivyo maisha ya huyu mtoto yapo hatarini!
Jamaa waliomsindikiza kwenye tax huyu mama ni wanaume watatu hakuna jisia ya kike! Walipofika wakahudumiwa wakataka kulipia staff aliyekuwepo akasema huduma za mama na mtoto ni bure, na hapo waksema wanazo 200,000/ mchina kawapa kwa ajili ya matibabu ya huyu mama na wakasema anahitaji risiti, wakauliza kama tunaweza kufanya mbinu ili risiti ipatikane .....kwa ufupi hatukuwapa risiti na badala yake yule mama alipewa sh.40,000 hela iliyobaki wasema wanaenda kutafta namna ya kupata risiti...tuachane na mambo ya pesa maana mimi sio lengo langu la kuleta uzi hapa JF,
Kitendo cha huyu mama kutohudhulia kliniki, kujifungulia kazini, nk kinaleta picha ya kuwepo na manyanyaso kwenye hiki kiwanda, nilitamani huyu mama awe mfano kwa akina mama na watu wote wanaoteswa na kunyimwa haki zao makazini...nilitamani kuripoti unyama huu ila....HII NCHI WAPENDA HAKI HAWATAKIWI KABISA, ukiangalia kesi za wenye pesa kama wale wezi wa mafuta Kigamboni ambapo serikali wapo kimya, nk nikijifanya kuingia anga za hawa wachina wanaoshirikiana na watanzania wenzangu yanaweza kunikuta ya kunikuta na kubaki peke yangu na historia isinikumbuke!
Tuendelee kuangalia pingamizi lililowekwa kwa Diamond Platnumz aondolewe kwenye tuzo za BET maana hiki ndicho waliowengi miongoni mwetu tunaweza sana!
Ulikosea kwenye ku frame story kabla ya kuileta humu... Nenda takukuru au kwa watu wa usalama wape hii ishuMkuu ingekuwa Dar ambapo kuna health facilities nyingi ingekuwa nafuu kulinda usalama wangu, hapa nilipo kuna vituo vya kutolea huduma za afya 3 tu, watuhumiwa hao ambao wengi wanatetewa na watanzania wenzetu wenye pesa na madaraka ni rahisi kujua ni kituo gani kilitoa taarifa ya mama huyo, ila pia enzi hizi mh, angalau kuna kipindi watoa taarifa walikuwa wanakabidhiwa kwenye vyombo vya usalama viwalinde!
Wananchi wakisimama pamoja hata Jeshi linatii, watanzania tumegawanywa kwa mafungu.mno..
Anasema hayupo dar...Bila shaka itakua ni Epza pale xtenal ubungo ktk kiwanda cha majinsi cha wachina
Zamani kidogo wakati nimeajiliwa sijafahamu vizuri kuhusu hii nchi nilikuwa na akili kama zako, mwisho wa mwezi mmoja nikakuta makato kwenye mshahara wangu ambayo sikujua ni ya nini, kuangalia kumbe Chama flani cha wafanyakazi, nikaenda ofisini kwao tena ofisi ya Mkoa nikawauliza kwanini wanakata pesa wakati sikuwahi kuomba uanachama na sikujaza fomu yoyote ya kuridhia makato? boss alijibu kwa kaejeli na dharau kibao hadi nikaamua kwenda Takukuru....hadi leo bado nakatwa hiyo hela na sijawahi kuomba uanachama, ila kila Mei Mosi huwa napewa tisheti na kofia!Ulikosea kwenye ku frame story kabla ya kuileta humu... Nenda takukuru au kwa watu wa usalama wape hii ishu