Natamani sana andiko hili la hukumu ya Afande Bageni lisomwe vituo vya Polisi na Makazi yao kwenye Paredi

NImesikia kweli huyu muuaji namba moja yuko Morogoro Mkambarani. Ila nasikia hali yake ni kama zezeta fulani hivi. Afadhali angefungwa jela angekuwa anajitambua ila hapo alipo sasa mmmmmmmm
Akiwa zezeta basi itakuwa afadhali Sana kwa Usalama wa Umma kwa sababu hatakuwa na uwezo tena wa kurudia kufanya uhalifu mbaya kama huo aliofanya kwa hao Wafanyabiashara aliowaua.
 
Polisi wote Tanzania ni majambazi yenye baraka za serikali,, ukweli usemwe,,
 
Naam! Ukifanya ubaya utalipwa ubaya na ukifanya wema utalipwa wema na ziada ya wema.
 
SSP Christopher Bageni atanyongwa hadi kufa. Ndivyo mahakama ya rufaa ilivyoamua. Maamuzi ya leo ni ya mwisho ktk mwenendo wa kesi yake. Hana pengine pa kukata rufaa, pa kukimbilia, wala pa kupinga. Mahakama imeamua anyongwe hadi afe. Jaji Stellah Mugasha amegonga nyundo. Itz over.

Hawezi kukata rufaa tena kwa sababu hukumu ya leo ni review ya hukumu iliyotolewa na mahakama hiyo September 16, 2016, ambapo alihukumiwa kunyongwa hadi kufa na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Benard Luanda. So hakuna mahakama ya kujadili tena shauri lake, labda Rais ampe msamaha.

Kwa wasiokumbuka Bageni alikua Mkuu wa Upelelezi wilaya ya Kinondoni. Mwaka 2006 yeye na wenzie wakiongozwa na aliyekua Kaimu RPC Dar, Abdalah Zombe, walituhumiwa kupanga njama za kuwauwa wafanyabiashara watatu wa Morogoro.

Zombe anadaiwa ndiye aliyeongoza wenzie kwenye mpango huo, baada ya kujulishwa kuwa wana madini na fedha kiasi cha shilingi milioni 200.

Walikamata gari waliyokua wameikodi. Wakamuongoza dereva hadi msitu wa Mabwepande. Wakapora madini pamoja na fedha zote walizokua nazo. Kisha wakawafunga vitambaa vyeusi usoni na pingu mikononi. Kisha wakawapiga risasi za kisogoni na kuwauwa wote akiwemo dereva wa taxi waliyemkodisha.

Kesho yake Zombe akaita media na kusema wameua majambazi yaliyokua yanarushiana risasi na Polisi. Rais Kikwete akaunda tume ya Jaji Kipenka kuchunguza. Ikabainika hawakuwa majambazi. Kilichouma zaidi walikua ndugu wa familia moja. Mama mmoja alipoteza wanae watatu. Watoto wa familia 4 wakapoteza baba zao, na wake wanne wakawa wajane kwa tamaa za polisi.

Zombe alifanikiwa "kuchomoka" kwenye kesi hii baada ya kusota rumande kwa miaka kadhaa. Lakini Bageni alipatikana na hatia akahukumiwa kunyongwa. Akakata rufaa ikafeli, akaomba review ya kesi, na rulling imesomwa leo kuwa ANYONGWE HADI KUFA.

Waliomtuma hawapo nae Segerea, wala hawatanyongwa pamoja nae. Atanyongwa peke yake. Wanaohangaika nae saivi angalau kumfariji ni familia yake. Zombe hayupo, OCD wake hayupo hata IGP wa wakati huo hayupo. Ni yeye mwenyewe, na atanyongwa mwenyewe.

Hii iwe fundisho kwa wote wanaotumwa kufanya maovu leo e.g kuteka, kuua na kupoteza watu. Ipo siku utajikuta peke yako. Anayekutuma hatakuwepo. Utasimama wewe mwenyewe kutoa hesabu ya maovu yako. Kama si hapa duniani basi hata mbinguni, lakini ipo siku utalipa. Kama ambavyo wema ni mbegu, na ubaya pia ni mbegu. Humea, hukomaa, na ni lazima UVUNE.!Na Tumcheni Mungu popote tutakapokuwapo,
 
Mimi huwa siitumii hiyo kauli coz selew maana yake πŸ˜‚
Hata mimi nilikuwa sijui ila nilimwuliza mke wangu maana yake, nilipoielewa ndo nimekuwa mkali kama mbogo kiasi kwamba ningekutana na aliyeiandika ningefanya kitu mbaya.
 
K
Kwa hiyo huyu bageni ana shati hilo hilo tu. Au hii ndiyo ile ile picha ya mwanzo?
 


Siku moja na yaliyomwua Kibao, na kuwapoteza akina soka, nayo yatendewe hivyo hivyo. Hayo ni mashetani yasiyostahili kuonewa huruma. Haya yalitakiwa kuuawa hadharani, tena kwa kuyakata kiungo kimoja kimoja, iwe fundisho kwa mashetani yaliyosalia.
 
Ciciem ni mafπŸ’©πŸ’©πŸ’© na samia buhiri ni takataka kesi hiyo walitakiwa kinyongwa watu kama 10 hivi ...basi hata huyo atapokea msamaha wa mjambiani mipumbavu
 
Anyongwe iwe fundisho,wakivaa magwanda wanadhani wako juu ya sheria
 
Damu Oops
Namuona Mkewe Wakati Mwingine Mo Town
Kwenye Usafiri Lakini Abdala Hoi
 
Baadhi ya Polisi huwa wana akili za ajabu ajabu sana, nina 2 brothers wako huko sioni msaada wao kabisa. Sitaki mazoea kabisa na polisi wa Tanzania

Nilipata wasaa wa kwenda hapo tu jirani Nairobi, aisee polisi wa wenzetu wana maadili ya kwenda mgeni ishu zangu zilikua zinakua sorted bila wenge.

Au issue ya "Fighting For Food Four years" bado ni pending issue kwao na haijapatiwa muarobaini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…