National Alliance for Mass Advancement(NEMA), chama kilichonyimwa usajili kwa kuogopwa wanachama wake

National Alliance for Mass Advancement(NEMA), chama kilichonyimwa usajili kwa kuogopwa wanachama wake

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
National Alliance For Mass Advancement(NEMA)

Nimeingia Maktaba na nimekuta picha ambazo nilipiga mimi mweyewe kwa mkono na jicho langu ukumbi wa Arnautoglu miaka 28 iliyopita. Ilikuwa siku ambayo msajili wa vyama anahakiki wanachama wa NEMA. Leo asubuhi naziangalia picha hizi nacheka peke yangu kama mwehu.

Nacheka kwa kuwa picha hizi zimenikumbusha mengi katika ujana wangu na mambo ambayo yalinishughulisha.
Mambo ambayo hivi sasa siwezi kuyafanya tena. Siwezi kuyafanya si kwa kuwa hayana maana, ila ile nguvu ya kwenda huku na kule haiko tena.

Nacheka na kumshukuru Allah kwa kutupa ujasiri wa kupambana na nguvu iliyokuwa na nguvu kubwa, na sisi hatuna chochote ila kule kukataa kudhulumiwa.

NEMA ilipata usajili wa muda tarehe 19 May, 1994. Siku ya usajili asubuhi na mapema wanachama wa NEMA tumeshafika ukumbi wa Arnautoglu tunawasubiri maofisa wa msajili wa vyama vya siasa afike. Ukumbi huu una historia kubwa katika siasa za Tanganyika.

Mle ndani ukumbini tulipokuwa tumekaa ndipo mwaka wa 1953 ulipofanyika uchaguzi wa mwaka wa TAA kumpata rais mpya. Uchaguzi huu ulikuwa baina ya Abdul Sykes na Julius Nyerere, Nyerere akachukua uongozi. Hiki ni kisa nimekieleza mara nyingi na wasomaji wangu naamini wanakijua vyema.

Fikra nyingi zikawa zinanipita kichwani najiambia, hivi wazee wetu waliounda TANU wakifufuka leo na kuja hapa Arnautoglu wakatuuliza imekuwaje mbona mnaunda chama kingine ile TANU tuliyowaundieni iko wapi, hivi tutawapa jibu gani? Majibu sasa yanafuatana na kuongozana moja baada ya lingine.

Lakini nikawa naamini kuwa hawa marehemu wazee wetu waliofufuka watakapo angalia wanachama wa NEMA watashangazwa na kitu kimoja. Wanachama wote tuliokuwa mle ndani ukumbini ni waswahili, kama walivyoanza wao katika ukumbi huu huu mwezi August 1954, TANU ilipoitisha mkutano wake wa kwanza.

Angalia picha hapo chini ya wanachama wa NEMA wakiwa ndani ya ukumbi wakisubiri kuhakikiwa. Fananisha na picha ya pili chini yake ya mkutano wa TANU wa mwaka wa 1955 uliofanyika Gandhi Hall, Hindu Mandal Dar es Salaam. Katika mkutano huo wa TANU wa mwaka wa 1955, kulikuwa na wajumbe wawili kutoka Lindi - Salum Mpunga na Ali Ibrahim Mnjawale.

Hawa walikuja na ujumbe maalum kutoka Southern Province kwa viongozi wa TANU makao makuu, kuwaeleza kuwa TANU inapataka pingazimi kutoka kwa wamishionari wanawazuia waumini wao wasijiuge na TANU kwa kueneza propaganda, kuwa TANU ilikuwa inataka kuanzisha vita vya maji maji dhidi ya waingereza kama walivyofanya akina Abdulraufu Songea Mbano.

Bila shaka maofisa waliokuwa wanahakiki wanachama wa NEMA, hili kuwa kila anaekuja mezani na kadi ya NEMA ni Muislam liliandika alama ya kuuliza vichwani mwao, na hivi ndivyo ilivyokuwa mikoani kote walikopita. Kwa kawaida inawezekana katika vyama vingine ikawa hakuna waislam na walio wengi wakiwa wengine, lakini kwa kawaida ya siasa za Tanzania hili huonekana sawa, tatizo linakuja pale wanapokuwapo waislam wengi.

Moja katika magazeti yaliyokuwa yanachuki kubwa na waislam na uislam Shaba likaandika kuwa, NEMA ni chama cha Waislam (Shaba, 19-25 July, 1994). NEMA ikatoa taarifa kupinga hilo lakini haikusaidia kitu. Msajili wa vyama vya siasa tokea mwanzo alifanya kila juhudi kuhakikisha kuwa NEMA hakipati usajili.

NEMA iliomba usajili kamili na kwa zaidi ya mwaka msajili wa vyama vya siasa hakuchukua hatua yoyote alibakia kimya. Mwishowe NEMA ilinyimwa usajili kwa kile kilichoelezwa kushindwa kutimiza masharti ya sheria ya vyama vya siasa. Lakini ukweli ulikuwa unajulikana wazi kabisa na huu haukuwa mwisho. Wanachama wa NEMA wakahamia kwengine kwenye chama kilichokuwa kimeshapata usajili.

1661401007886.png
1661400870543.png
1661400904130.png
1661401007886.png
 

Attachments

  • 1661401079103.png
    1661401079103.png
    25 KB · Views: 15
Enzi hizo za kina Nyerere ilikuwa ni mpambano wa dhidi ya mkoloni mweupe. Watanzania hatukuwa na udini..

Hivi sasa tunapambana na mkoloni mweusi. Huyu mkoloni mweusi amerithi dini za mwarabu na mzungu...

Mkoloni mweusi ni mwoga sana. Hataki mwarabu na mzungu watengane... Maana Watampa usumbufu wa kutawala.... Anawaweka pamoja ili awatawale vizuri

CCM yajenga nchi
 
Chief...
Hapana katika sheria ya "abbreviations" inaruhusiwa kuandikwa hivyo.
Hapo nikiri kuwa siijui hiyo sheria, lakini kimantiki tu, nadhani abbreviation yoyote inapasa kuakisi uhalisia na ukweli! Unataka kuniambia kuwa CCM wanaweza kuweka abbreviations kama MCC au MCM au CUF waandika CFU au vinginevyo na ikawa sawa!? Sijui hebu tuelimishe bradha Mohamed Said.
 
Hapo nikiri kuwa siijui hiyo sheria, lakini kimantiki tu, nadhani abbreviation yoyote inapasa kuakisi uhalisia na ukweli! Unataka kuniambia kuwa CCM wanaweza kuweka abbreviations kama MCC au MCM au CUF waandika CFU au vinginevyo na ikawa sawa!? Sijui hebu tuelimishe bradha Mohamed Said.
Chief...
CCM herufi zimejipanga kwa hiyo hakuna sababu ya kubadili chochote.

Tayari nimekwisha kukufahamisha.
 
Chief...
CCM herufi zimejipanga kwa hiyo hakuna sababu ya kubadili chochote.

Tayari nimekwisha kukufahamisha.
Kaka Mohamed Said, tangu mwanzo nimekiri kuhusu hiyo sheria ya "abbreviations" na ndiyo maana nikazidi kuuliza ili nielewe zaidi; hata hivyo kwani hizo abbreviations za NAMA hazikujipanga!? Hilo ndio swali ili uweze kupata mpangilio mzuri badala ya NEMA unless mlikuwa mnalenga neema!
 
Kaka Mohamed Said, tangu mwanzo nimekiri kuhusu hiyo sheria ya "abbreviations" na ndiyo maana nikazidi kuuliza ili nielewe zaidi; hata hivyo kwani hizo abbreviations za NAMA hazikujipanga!? Hilo ndio swali ili uweze kupata mpangilio mzuri badala ya NEMA unless mlikuwa mnalenga neema!
Chief...
Nimekupa maelezo yangu sina zaidi.
 
Enzi hizo za kina Nyerere ilikuwa ni mpambano wa dhidi ya mkoloni mweupe. Watanzania hatukuwa na udini..

Hivi sasa tunapambana na mkoloni mweusi. Huyu mkoloni mweusi amerithi dini za mwarabu na mzungu...

Mkoloni mweusi ni mwoga sana. Hataki mwarabu na mzungu watengane... Maana Watampa usumbufu wa kutawala.... Anawaweka pamoja ili awatawale vizuri

CCM yajenga nchi
Sioni umuhimu wa dini kwa waafrika
 
Hii Nchi ina historia tamu sana hasa namna Watawala wa mwanzo walivyoifinyanga ili kuondoa au kuzuia chokochoko za wachache waliotaka kutugawa.

Ilianza na chama cha NRA akiwemo na Kighoma Malima, kulikuwa na harufu kali sana ya 'dini'. Wazalendo kitengoni wakawa wanawafuatilia kwa makini humohumo ndani kwao na hatimaye kikafa bila kuleta athari yeyote ya mgawanyiko. Akaja Mtikila na kelele zake, wakamwangalia na kumuacha wakijua mbio za sakafuni zinaishia ukingoni. Hatimaye Mtikila kaondoka Duniani akiwa na wanachama wasiojaa hata kwenye basi la mkoani.

Wakatokea wachache wakataka kuifanya CUF kama chama cha mlengo flani, lakini matokeo yake kikajitahidi kujijenga Kitaifa na hatimaye leo kimekuwa historia.

Ila nilichojifunza Nchi hii ni kuwa, Watu wengi hawapendi harufu za migawanyiko, ndiyo maana wanapogundua kuna hila flani huwa wanajitenga na hata hawakuambii, kimyakimya.

Mimi nilikuwa msomaji mkubwa wa gazeti la Annur, kwa waliokuwa wanalisoma wakati huo watakubaliana na mimi kuna makala zilikuwa kali sana na zinazochochea mgawanyiko au kuonyesha sisi na wao, na likinunuliwa sana na baadhi ya Ndugu zetu Waislam, lakini nini kilitokea? Sasa lipo hoi bin taabani. 'Wazalendo wangeweza hata kulifungia kama walivyokuwa wanafungia magazeti mengine, lakini wakaliacha wakijua kwa yakini kabisa, wanaonunua watalichoka tu kwa sababu linawapeleka kwenye utamaduni usiokuwa wa kwetu.
 
Hii Nchi ina historia tamu sana hasa namna Watawala wa mwanzo walivyoifinyanga ili kuondoa au kuzuia chokochoko za wachache waliotaka kutugawa.

Ilianza na chama cha NRA akiwemo na Kighoma Malima, kulikuwa na harufu kali sana ya 'dini'. Wazalendo kitengoni wakawa wanawafuatilia kwa makini humohumo ndani kwao na hatimaye kikafa bila kuleta athari yeyote ya mgawanyiko. Akaja Mtikila na kelele zake, wakamwangalia na kumuacha wakijua mbio za sakafuni zinaishia ukingoni. Hatimaye Mtikila kaondoka Duniani akiwa na wanachama wasiojaa hata kwenye basi la mkoani.

Wakatokea wachache wakataka kuifanya CUF kama chama cha mlengo flani, lakini matokeo yake kikajitahidi kujijenga Kitaifa na hatimaye leo kimekuwa historia.

Ila nilichojifunza Nchi hii ni kuwa, Watu wengi hawapendi harufu za migawanyiko, ndiyo maana wanapogundua kuna hila flani huwa wanajitenga na hata hawakuambii, kimyakimya.

Mimi nilikuwa msomaji mkubwa wa gazeti la Annur, kwa waliokuwa wanalisoma wakati huo watakubaliana na mimi kuna makala zilikuwa kali sana na zinazochochea mgawanyiko au kuonyesha sisi na wao, na likinunuliwa sana na baadhi ya Ndugu zetu Waislam, lakini nini kilitokea? Sasa lipo hoi bin taabani. 'Wazalendo wangeweza hata kulifungia kama walivyokuwa wanafungia magazeti mengine, lakini wakaliacha wakijua kwa yakini kabisa, wanaonunua watalichoka tu kwa sababu linawapeleka kwenye utamaduni usiokuwa wa kwetu.
Plato...
Tatizo la udini si jepesi kama ulivyolieleza.
Wala haikuwa Waislam waliosababisha hili tatizo leo kuwapo katika jamii.

Wewe hulijui tatizo la udini wala hajaonja ubaguzi huu wa dini.
Sababu yake ni kuwa wewe uko kwenye kundi la Wengine.

Ikiwa kwa hakika ungependa kulijua tatizo hili unahitaji muda kusoma vitabu vilivyoandikwa kuhusu somo hili.

Wala sitakupa rejea ya mwandishi yeyote Muislam.
Nitakupa rejea za Bergen (1981) na Sivalon (1992).

Lakini ukitaka rejea ya Muislam nakushauri umsome Njozi (2002).

Kwa ajili ya ukweli uliomo mle ndani jinsi Waislam tunavyobaguliwa kitabu, ''Mwembechai Killings...'' kilipigwa marufuku na serikali.

Nakusoma katika post yako jinsi unavyotamba jinsi serikali inavyokabiliana na Waislam wanaotafuta haki zao kwa njia mbalimbali.

Hii si dalili nzuri kwa nchi yetu.

Kuhusu NRA, CUF, Prof. Malima nk.
Hivyo vyama Waislam waliviunga mkono kuonyesha hawaridhishwi na CCM.

Kuhusu Prof. Malima.

Yeye aligundua dhulma waliokuwa wakifanyiwa vijana wa Kiislam katika elimu ndani ya Wizara ya Elimu na aliandika ripoti kamili kumweleza Rais Mwinyi "mchezo," uliokuwa ukichezwa kwenye wizara hiyo.

Hiki ni kisa kirefu siwezi kueleza yote hapa.

Ama kuhusu Annur gazeti lipo na linatoka ''online'' kila Ijumaa na wasomaji sasa ni wengi kuliko wakati ule lilipokuwa linauzwa.

Waislam hawajataka kumgawa yeyote katika nchi hii na laiti Waislam tungekuwa wabaguzi Julius Nyerere asingepata uongozi wa nchi hii.

Kwani hujui Nyerere alipokelewa na nani alipofika Dar es Salaam?
Hivi hujui aliishi nyumba ya nani alipoacha kazi ya Ualimu?

Hujui katika wafadhili wanne wa Mwalimu watatu walikuwa Waislam na wawili ni ndugu mtu na mdogo wake?

Hufahamu kuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa na Nyerere bega kwa bega ndani ya TANU kupigania uhuru wa Tanganyika na akiuza kadi za TANU ndani ya misikiti?

Wengine na Maaskofu ambao walikuwa awala zaidi kuwa ubavuni kwa Nyerere walikuwa wapi?

Ndiyo nakuambia hili la udini inataka usome historia ya Nyerere mwenyewe kabla ya kunyanyua kalamu.

Waislam ndiyo tunaobaguliwa na tatizo hili lilianza baada ya uhuru kupatikana.

Wale walioshika madaraka hawakutaka kugawana madaraka na watu wa dini nyingine.

Yapo mengi ningependa kukusomesha.
Tusimame hapa kwa sasa.

Hiki kitabu hapo chini naogopa kukuambia kinasema nini.
Kilikuwa kinauzwa Cathedral Bookshop.

Ilipofahamika yaliyomo humo ndani kitabu wakakiondoa hapo bookshop kama walivyokiondoa hicho kingine:

1661437064967.jpeg

1661437206624.jpeg
 
Plato...
Tatizo la udini si jepesi kama ulivyolieleza.
Wala haikuwa Waislam waliosababisha hili tatizo leo kuwapo katika jamii.

Wewe hulijui tatizo la udini wala hajaonja ubaguzi huu wa dini.
Sababu yake ni kuwa wewe uko kwenye kundi la Wengine.

Ikiwa kwa hakika ungependa kulijua tatizo hili unahitaji muda kusoma vitabu vilivyoandikwa kuhusu somo hili.

Wala sitakupa rejea ya mwandishi yeyote Muislam.
Nitakupa rejea za Bergen (1981) na Sivalon (1992).

Lakini ukitaka rejea ya Muislam nakushauri umsome Njozi (2002).

Kwa ajili ya ukweli uliomo mle ndani jinsi Waislam tunavyobaguliwa kitabu, ''Mwembechai Killings...'' kilipigwa marufuku na serikali.

Nakusoma katika post yako jinsi unavyotamba jinsi serikali inavyokabiliana na Waislam wanaotafuta haki zao kwa njia mbalimbali.

Hii si dalili nzuri kwa nchi yetu.

Kuhusu NRA, CUF, Prof. Malima nk.
Hivyo vyama Waislam waliviunga mkono kuonyesha hawaridhishwi na CCM.

Kuhusu Prof. Malima.

Yeye aligundua dhulma waliokuwa wakifanyiwa vijana wa Kiislam katika elimu ndani ya Wizara ya Elimu na aliandika ripoti kamili kumweleza Rais Mwinyi "mchezo," uliokuwa ukichezwa kwenye wizara hiyo.

Hiki ni kisa kirefu siwezi kueleza yote hapa.

Ama kuhusu Annur gazeti lipo na linatoka ''online'' kila Ijumaa na wasomaji sasa ni wengi kuliko wakati ule lilipokuwa linauzwa.

Waislam hawajataka kumgawa yeyote katika nchi hii na laiti Waislam tungekuwa wabaguzi Julius Nyerere asingepata uongozi wa nchi hii.

Kwani hujui Nyerere alipokelewa na nani alipofika Dar es Salaam?
Hivi hujui aliishi nyumba ya nani alipoacha kazi ya Ualimu?

Hujui katika wafadhili wanne wa Mwalimu watatu walikuwa Waislam na wawili ni ndugu mtu na mdogo wake?

Hufahamu kuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa na Nyerere bega kwa bega ndani ya TANU kupigania uhuru wa Tanganyika na akiuza kadi za TANU ndani ya misikiti?

Wengine na Maaskofu ambao walikuwa awala zaidi kuwa ubavuni kwa Nyerere walikuwa wapi?

Ndiyo nakuambia hili la udini inataka usome historia ya Nyerere mwenyewe kabla ya kunyanyua kalamu.

Waislam ndiyo tunaobaguliwa na tatizo hili lilianza baada ya uhuru kupatikana.

Wale walioshika madaraka hawakutaka kugawana madaraka na watu wa dini nyingine.

Yapo mengi ningependa kukusomesha.
Tusimame hapa kwa sasa.

Hiki kitabu hapo chini naogopa kukuambia kinasema nini.
Kilikuwa kinauzwa Cathedral Bookshop.

Ilipofahamika yaliyomo humo ndani kitabu wakakiondoa hapo bookshop kama walivyokiondoa hicho kingine:

View attachment 2334600
View attachment 2334601
Nimwelezea mpaka Mtikila.

Hili la kunitaka nimsome Sivalon wala halina sana maana kwangu. Huyo ndiye aliyeandika Baraza zima la mawaziri kumejaa Wakatoliki (uongo wa waziwazi) si Mtu wa kumzingatia.

La msingi na kubwa ambalo nimeeleza ni kuwa mbinu zote za hila zilianguka na zile halali zilifanikiwa. Na hilo ndilo muhimu kwetu kama Watanzania.

Hili la Mwalimu kupokewa Dar es Salaam ndiyo yaleyale yaliyokuwa yakisemwa kuwa Mwalimu kafundishwa kuvaa suti/suruali na Watu wa Dar es Salaam. Msomi ametoka kupiga kitabu UK kwa wenye utamaduni wao wa kuvaa suti aje afundishwe kuvaa suti Dar es Salaam. Na hili la kupokewa Dar narudia kulekule, Msomi amemaliza elimu yake na kapangiwa eneo la kazi Pugu asijue atafikaje kazini kwake, waajiri na wafanyakazi wake ndiyo waliompokea Dar es Salaam.
 
Huyu mzee ni kichwa sana na utulivu sana kwenye maandishi yake na hata umjibu ujeuri vipi huwa hapanik anajibu kwa utulivu na hekima ila maandiko yake mengi yako na dark intentions kiufupi mzee wetu ana nia ovu na umoja wetu wakitaifa
 
Nimwelezea mpaka Mtikila.
Hili la kunitaka nimsome Sivalon wala halina sana maana kwangu. Huyo ndiye aliyeandika Baraza zima la mawaziri kumejaa Wakatoliki (uongo wa waziwazi) si Mtu wa kumzingatia.

La msingi na kubwa ambalo nimeeleza ni kuwa mbinu zote za hila zilianguka na zile halali zilifanikiwa. Na hilo ndilo muhimu kwetu kama Watanzania.

Hili la Mwalimu kupokewa Dar es Salaam ndiyo yaleyale yaliyokuwa yakisemwa kuwa Mwalimu kafundishwa kuvaa suti/suruali na Watu wa Dar es Salaam. Msomi ametoka kupiga kitabu UK kwa wenye utamaduni wao wa kuvaa suti aje afundishwe kuvaa suti Dar es Salaam. Na hili la kupokewa Dar narudia kulekule, Msomi amemaliza elimu yake na kapangiwa eneo la kazi Pugu asijue atafikaje kazini kwake, waajiri na wafanyakazi wake ndiyo waliompokea Dar es Salaam.
Plato...
Mimi si mtu wa kuandika mambo hayo ya suti nk.

Mimi naandika mambo ambayo mtu akiona post yangu atasimama kusoma kwa kuwa kipo atakachojifunza.

Kupokelewa kwa Nyerere Dar es Salaam ni muhimu sana katika historia yake kwani vinginevyo vipi angeweza kukubalika?

Pugu si Dar es Salaam mjini Mtaa wa Stanley na Sikukuu nyumbani kwa Abdul Sykes, Act. President na Secretary wa TAA.

Pugu si Kariakoo Market ambako Abdul Sykes alikuwa Market Master.

Hapo kulikuwa na watu maarufu na wanachama wa TANU kama Mzee Mshume Kiyate na Shariff Abdallah Attas.

Watu wengi walimfahamu Nyerere hapo na nyumbani kwa Abdul Sykes baada ya kuacha kazi ya Ualimu na kuhama Pugu.

Hapa kuna historia ya kusisimua.

Nakuwekea picha ya Mwalimu Nyerere akiwa Uwanja wa Ndege safari ya kwanza UNO 1955 kasindikizwa na mke wa Shariff Attas, Bi. Chiku int Said Kisusa, Bi. Tatu bint Mzee Bi. Titi Mohamed na akina mama wengine wawili sijapata majina yao.

Hawa akina mama ndiyo waliokuwa wanaifanyia kampeni mikutano ya TANU kujaza wanawake viwanja vya Mnazi Mmoja na wakihudhuria mikutano ya ndani nyumbani kwa Abdul Sykes siku moja kabla ya mkutano kuweka mikakati.

Hapo ndipo ninaposema kama mtu haijui historia ya Mwalimu na historia ya TANU atataabika sana.

Kuna kipindi cha TV kitarushwa hivi karibuni.

Picha hiyo watayarishaji wa kipindi hicho wakiwa kazini mimi niko pembeni yao nikieleza jinsi baadhi wanachama wa TANU na baadhi ya viongozi walivyokuwa wakikusanyika ofisi ya TANU, New Street kisha pamoja kwa maandamano wakienda Mnazi Mmoja mbele umetangulia Mganda.

Picha ya mwisho hiyo ipo hapo Mnazi Mmoja watu wanasema imewekwa hapo kama kumbukumbu ya Mganda uliokuwa ukiwaleta TANU mkutanoni Mnazi Mmoja kumsikiliza Mwalimu Nyerere.

1661450160053.png

1661450586105.png

1661451486538.png
 
Huyu mzee ni kichwa sana na utulivu sana kwenye maandishi yake na hata umjibu ujeuri vipi huwa hapanik anajibu kwa utulivu na hekima ila maandiko yake mengi yako na dark intentions kiufupi mzee wetu ana nia ovu na umoja wetu wakitaifa
Ujoka,
Ikiwa wewe fikra yako ni kuwa umoja wa kitaifa utaimarika kwa Waislam kuwa raia daraja la tatu huo moja kamwe hautapatikana.

Unajua kuwa tuko 20:80?
Huu ndiyo umoja unaokupendeza wewe?

Unatarajia hawa 20 waliokuwa mstari wa mbele kuondoa dhulma za wakoloni wanaridhika na hali hii?
 
Back
Top Bottom