National Intelligence and State Intelligence

National Intelligence and State Intelligence

Uongo gani ambao Yericko kausema au kusema kuna tofauti kati ya National na State Intelligence, na mbona unayemsifia kazunguka mlemle alimopita Yericko.
Sidhani kama umesoma vitu vizuri na kuvielewa. Halafu ni kushauri tu unapotaka kufanya analysis ya kitu chochote jibidiishe kujielimisha mwenyewe from other sources thn ndo uje humu utajua wapi unalishwa matango pori wp unaambiwa ukweli.

Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
 
Karai jingine lililoamua kuja na stori za alfulelaulela...unapiga stori za vikosi unavyodai ktk nchi wanaweza kuwa wanavifahamu watu wawili then unatoa maelezo as if na wewe ni miongoni mwa hao watano...Makarai acheni kutuongopea tuna akilii
 
SAD ni kitengo cha CIA,
operation nyingi za siri wanafana hawa ikiwemo mauaji,na sio lazima iwe ni amri ya rais ama rais ajue nini wamefanya,
anaweza akajua director wa CIA,
ama hata yeye anaweza asijue,
mfano boss wa kawaida ndani ya CIA anaweza ku authorise operation na hawa SAD wakafanya,na inaweza isiwe kwa maslahi ya rais au nchi,
inaweza ikawa kwa maslahi ya kikundi cha watu ndani ya CIA,ama ndani ya uongozi wa marekani,mfano senator fulani,au pengine labda foreign secretary etc,
rais wa marekani haidhinishi operation zote zinazofanywa na CIA,nyingi hupewa taarifa baada ya operation,
ama hata asipewe taarifa
 
strugo BOMBERDIER INAMSAIDIA NINI MAMA LISHE? USILAZMISHE WATU NAMNA YA KUFKIRI WAKAT HATA WEW UWEZO WAKO WA KUFKIRI NI 0.1%
 
Oii UMESEMA WATU WA SERIKALI WANGETUMWA KUUA LISU ASINGEPONA, KWA HYO KUMBE WATU WA SERIKALI HUWA WANATUMWA KTK MISHENI ZA KUUA? EBU TUPE MIFANO

MWSHO, HATMA YA ROHO YA BNADAMU ANAIJUA MUNGU, HATA DR. ULIMBOKA ALISEMA WALIOMTESA WALIJIHAKIKISHIA AMEKUFA LAKN AKAWA HAI.

MUNGU NDYE KASHKILIA UHAI WA MTU NA NDIYO MAANA WEWE UNAWEZA PGWA RISAS YA TUMBO UKAFA MWINGNE AKAPONA.
 
Uongo gani ambao Yericko kausema au kusema kuna tofauti kati ya National na State Intelligence, na mbona unayemsifia kazunguka mlemle alimopita Yericko.
tofauti ya msingi ni kuviweka hivyo vikosi katika category ya 'vizivyo kisheria'. mathalan Kidon ipo kisheria, Soma kitabu cha By way of deception au Gideon spies utajua kuhusu Mossad na matawi yake.
 
Samahani kwa kukukosoa. Naamini kuwa uongo usiporekebishwa unaweza kuonekana ukweli.

Ni rahisi sana kuwadanganya Watanzania wengi. Na sababu kuu ni wengi wao kutojihangaisha japo ku-Google vitu mbalimbali wanavyokutana navyo mitandaoni au hata katika maongezi.

Unfortunately, tuna wenzetu ambao ni mahiri sana katika kutumia udhaifu huo, ambapo huzusha habari huku wakijua bayana hakuna atakayejihangaisha ku-countercheck. Kibaya zaidi, hata mtu aki-volunteer kuweka rekodi sawa, chances are ataonekana kama hater flani.

Situation could become even worse katika zama hizi za fake news, maana hiki ni kipindi ambacho mlaji wa habari/taarifa shurti afanye jitihada za ziada kusaka ukweli, kwa vile hata baadhi taasisi za habari za rekodi nazo zaweza kujiingiza katika mkumbo wa fake news.

Back to kwako Bwana Yericko. Sijui ulidanganywa, au umeamua tu kudanganya, lakini tafsiri ya ulichokiita "national intelligence" ni mgawanyiko tu wa majukumu ya kiintelijensia ndani ya taifa husika, ilhali ulichokiita "state intelligence" ni ujumla wa intelijensia kwa taifa husika, mara nyingi kwa kulinganisha na taifa jingine. Maelezo yako kuhusu maneno hayo sio sahihi.

Umeandika "National Intelligence huwa ipo kisheria (Legal), na State Intelligence huwa haipo kisheria (illegal). Wanaweza kufanya kazi moja, mahali pamoja, nk Tofauti yao nikuwa kimoja Natinal Intelligence kinafanya kazi chini ya miiko na taratibu za kisheria kwa nchi husika, na State Intelligence hakitambuliwi na sheria yoyote zaidi ya (decree) na mara nyingi huwa hakifahamiki na wengi katika serikali, huenda katika nchi kikafahamika na watu watano au sita tu." Nani aliyekudanganya? Or rather kwanini unadanganya?

Labda kwa kukusaidia tu, ni vema ukajielimisha kuhusu tofauti/mfanano kati ya" nation" na "state" na maana ya "intelligence" kisha ulete hiyo nonexistent dichotomy kati ya "national intelligence" vs "state intelligence." Sio siri, upotoshaji wa aina hii unakera hasa ikizingatiwa kuwa haya ni masuala nyeti.

Bila aibu unaandika "Special Activites Division (SAD)... huendesha shughuli zenye maslahi ya rais, chafu, mbaya na pia dhalili zenye maslahi kwa nchi na muda mwingine kwa maslahi ya wakuu katika nchi au katika vikosi husika. Uwepo wacho hautambuliwi na katiba wala sheria yoyote." Urais Marekani ni taasisi, na tofauti na akina sie ambapo kimsingi Rais ndio mkuu" halisi" wa Idara ya Usalama wa Taifa, kwa wenzetu uhusiano kati ya Rais na taasisi za intelijensia ni wa kitaasisi kuliko matakwa binafsi.

Special Activities Division ya CIA ni moja tu ya vitengo kadhaa vya Idara hiyo ya ujasusi. Ipo kisheria na uwepo wake unafahamika. Kwa wenye uhusiano mzuri na Google, fanya kuuliza, kisha linganisha na hicho anachodai Bwana Yericko.

Kwa kifupi, Special Activities Division ni kitengo kinachohusika na "covert operations." Na kimegawanyika sehemu mbili, "Special Operations Group" (SAD/SOG) kwa ajili ya operesheni zenye ujeshi ndani yake (tactical paramilitary operations) na "Political Action Group" (SAD/PAG) kwa ajili ya operesheni za siri za kishushushu kuhusiana na siasa (covert political action). Kama ilivyo nature ya CIA, yaani taasisi ya ujasusi, shughuli hizi hulenga mataifa mengine. Special Activities Division humpatia Rais wa Marekani option mbadala pindi njia za kidiplomasia zinapoonekana hazina ufanisi.

Kwa wenye uhusiano mzuri na Google, bonyeza hapa https://www.google.co.uk/search?biw....64.mobile-gws-serp..1.0.0....248.aG24GvAxhbo

Kuhusu Kidon ya Israeli, Bwana Yericko umefanya kile Waingereza wanaita "telling tall stories," tuseme "changa la macho" kwa lugha ya mtaani. Kufupisha maelezo, Kidon ni kitengo cha Mossad kama ilivyo Special Activities Division ya CIA, kinachofanya shughuli zake (mostly mauaji) kwa usiri mkubwa kupindukia. Na hiyo "usiri mkubwa kupindukia" ni kama utani katika ushushushu, kwa sababu taaluma yenyewe nzima ni ya "usiri mkubwa kupindukia."

Kidon hufahamika kama "Mossad ndani ya Mossad" kwani ipo "compartmentalised" kwa kiwango cha juu kiasi kwamba hata ofisi zake hazipo katika makao makuu ya Mossad. Na ni nadra kwa maafisa wa Kidon, wanaojulikana kama "The Team" kwenda katika ofisi za Mossad. I hope Bwana Yericko utawaeleza "raia" maana ya "compartmentalisation."

Kidon - neno la Kiyahudi lenye maana ya singe (bayonet) - imebobea katika "infiltration" (kujipenyeza) katika nchi mahasimu wa Israel kwa lengo la kuuwa bila kuacha alama.

Moja ya faida kubwa kwa Mossad ni asili ya uhamiaji wa Waisraeli, kwa maana kwamba wengi wao wana asili pia ya nchi mbalimbali duniani, na hiyo inawapa faida moja muhimu majasusi wa nchi hiyo: uwezo wa hali ya juu kumudu lugha na tamaduni za nchi nyingine. Na maafisa wa Kidon ni wanufaika wa faida hiyo.

Again, kwa mwenye muda, au mwenye kiu ya kujua zaidi kuhusu Kidon, link ya kusaka taarifa zao mbalimbali ni hii https://www.google.co.uk/search?q=k...j0l2.2964j0j4&sourceid=chrome-mobile&ie=UTF-8

Kuhusu Spetsnaz, Bwana Yericko umeongopa kwamba "Nchini Urusi nako ikulu ya Kremlin chini ya Vladimir Vladimirovich Putin ina kikosi ndani ya jeshi kitwacho Spetsnaz ambacho kazi yake kubwa ni kudhibiti wapinzani wa kisiasa na wanaharakati nchini Urusi, kikosi hiki kipo ndani ya shirika la Ujasusi la nchi hiyo la FSB japo kinaundwa zaidi na wanajeshi wa Red Army na hakitambuliwi kwa sheria yoyote ndani na nje ya Urusi." Uzuri wako Bwana Yericko ni kwamba unajua kuupamba uongo hadi unaonekana kama ukweli.

Kwa kifupi, tofauti na "tall story" yako Bwana Yericko, neno "spetsnaz" ni neno la jumla (umbrella term) lenye maana ya "special forces" kwa Kirusi, na linatumika sio Russia pekee bali pia katika mataifa mengine ya Ulaya Mashariki hasa yale ambayo zamani yalikuwa sehemu ya USSR.

Tofauti na porojo zako Bwana Yericko kwamba "spetsnaz" (special force) ipo chini ya FSB, ukweli ni kwamba ipo chini ya GRU na hujulikana kama "Spetsnaz GRU." Kwa ufafanuzi, GRU ni idara ya intelijensia ya kijeshi (military intelligence) na FSB ni Idara ya intelijensia ya ndani ya Russia, ilhali Idara ya ujasusi ya nchi hiyo ni SVR.

Again, mengi kuhusu Spestnaz, kiungo hiki hapa www.google.co.uk/search?q=spetsnaz&oq=sp&aqs=chrome.0.69i59l2j69i57j69i61j0j69i61.2434j0j9&sourceid=chrome-mobile&ie=UTF-8

Kuhusu Zanzibar, anachoongelea Bwana Yericko ni matumizi fyongo ya Idara ya Usalama wa Taifa, na wala si uwepo wa "Idara ya Usalama wa taifa ya Zanzibar." Modern equivalent ni hicho kinachosemekana kuongozwa na Bashite hivi sasa.

Kwanini Bwana Yericko unamuua kupotosha umma makusudi? Jibu unalo mwenyewe. Nakuheshimu kama mtu unayejibidiisha sana kusaka uelewa, lakini huwa nashindwa kuelewa kwanini at times anaamua kuhatarisha reputation yake kwa "tall stories." Yatendee haki maeneo usioyaelewa.

Nikusaidie kwa ufahamu huu wa traits tatu za very intelligent people
bd8cd6ce1df6d62f021e8c412f227807.jpg
Jaribu kuzingatia hiyo ya tatu

Samahani Bwana Yericko kama nitakuwa nimekukwaza lakini ni vema kuweka rekodi sawia, maana uongo usipopingwa waweza kuwa ukweli. Otherwise, hongera kwa mapenzi yako kwenye taaluma ya intelijensia.
Kuna bwana mmoja ni mkimbizi anaishi ughaibuni, naamini atachangia huko mbeleni, yeye amejipa umiliki wa mambo ya aina hii, hivyo hata siku moja hawezi kukubaliana na alichoandika mwingine, atakipinga na kuja na majibu yaleyale ya aliyempinga lakini atazunguka weeee mpaka mwisho anarudi palepale....


Anyway, bwana Kulikoni Ughaibuni, maprofesa wanaposoma tasnifu za wafunzwa wao huzingatia mambo mawili tu, nayo huitwa "dhanna" na "mantiki". Kama mwanafunzi ataweza kushawishi jopo la maprofesa hawa katika mambo hayo mawili basi huyo hujihesabu kuwa ni mzamivu.

Yasome maandishi yako kisha chambua dhanna na mantiki ya andiko langu, kwahakika ungeikosa sifa ya uzamivu.

Wewe ni msomi na ninafahamu umepata Phd hapo ya siasa, kibaya zaidi kwenye andiko langu umeachana kabisa na matumizi ya uwanda wako na kujivika hasira za mkizi...


Shukrani sana kwa mchango wako mkuu, mpaka tarehe 15 mwezi huu nitamaliza kusoma kitabu cha Shushushu kilichoandikwa na kada mtiifu wa ccm aitwaye Evarist Chahali. Ni kizuri japo kina makosa ya kimantiki na kidhanna.
 
tofauti ya msingi ni kuviweka hivyo vikosi katika category ya 'vizivyo kisheria'. mathalan Kidon ipo kisheria, Soma kitabu cha By way of deception au Gideon spies utajua kuhusu Mossad na matawi yake.
Kuna hitajika tafsiri mpya ya kiswahili ili kukubaliana na hoja, kusema kisicho cha kisheria hakuna maana kwamba anayekiongoza hayupo kisheria...

Mfano Idara ya Usalama Tanzania (TISS) tangu baada na kabla ya Uhuru haikuwa kisheria, lakini ilifanya kazi zote kama idara ya ujasusi tu. Miaka yote ilikuwa ni kitengo ndani ya Jeshi la Polisi ikiitwa Tawi Maalumu (Special Branch SB) mpaka Mzee Mkapa alipokuja kuiweka kisheria na kuiita Tanzania Intelligence and Security Service (TISS).

Sasa watu kama akina Chahali ukiwambia TISS iliendesha shughuli zake in black space yaani kiharamu, watakukatalia na kukuletea maandishi mareeeefu na milinks ya Google kujihalalishia kile wakisemacho....
 
Kuna hitajika tafsiri mpya ya kiswahili ili kukubaliana na hoja, kusema kisicho cha kisheria hakuna maana kwamba anayekiongoza hayupo kisheria...

Mfano Idara ya Usalama Tanzania (TISS) tangu baada na kabla ya Uhuru haikuwa kisheria, lakini ilifanya kazi zote kama idara ya ujasusi tu. Miaka yote ilikuwa ni kitengo ndani ya Jeshi la Polisi ikiitwa Tawi Maalumu (Special Branch SB) mpaka Mzee Mkapa alipokuja kuiweka kisheria na kuiita Tanzania Intelligence and Security Service (TISS).

Sasa watu kama akina Chahali ukiwambia TISS iliendesha shughuli zake in black space yaani kiharamu, watakukatalia na kukuletea maandishi mareeeefu na milinks ya Google kujihalalishia kile wakisemacho....

Surprise me na kitu kipya, Bwana Yericko. Mie sintochoka kukurekebisha kila utapowalisha watu matango pori, na hata ukikimbilia kwenye kashfa au matusi, hayatozidi yale uliyotoa dhidi yangu wakati wa kampeni za mwaka 2015.

Mie japo sijasoma kitabu ukichoandika, siwezi kufanya utoto kama wako kukikebehi. Afterall, sikuandika kitabu changu kwa minajili ya kusaka sifa au kuwathibitishia watu kitu flani bali ulikuwa mchango wangu katika body of knowledge.

Kuna kijana mmoja alijipa uhuru kama wako kule Facebook. Nikamsihi kistaarabu kuwa hoja hujibiwa na hoja na si kebehi au matusi dhidi ya mtoa hoja...mie yangu macho! [emoji4]
 
Surprise me na kitu kipya, Bwana Yericko. Mie sintochoka kukurekebisha kila utapowalisha watu matango pori, na hata ukikimbilia kwenye kashfa au matusi, hayatozidi yale uliyotoa dhidi yangu wakati wa kampeni za mwaka 2015.

Mie japo sijasoma kitabu ukichoandika, siwezi kufanya utoto kama wako kukikebehi. Afterall, sikuandika kitabu changu kwa minajili ya kusaka sifa au kuwathibitishia watu kitu flani bali ulikuwa mchango wangu katika body of knowledge.

Kuna kijana mmoja alijipa uhuru kama wako kule Facebook. Nikamsihi kistaarabu kuwa hoja hujibiwa na hoja na si kebehi au matusi dhidi ya mtoa hoja...mie yangu macho! [emoji4]
Hakuna ulichosahihisha ndugu, nilichofanya nimekurejesha kwenye mstari uache kijicho na ujenge hoja za kisomi tu.......

Kwani wewe ndio yule Chahali mwandishi wa kitabu cha Shushushu? Basi tumia jina lako halisi ili tujadiliana kwa hekima na taadhima....

Kubwa zaidi Yericko hajawahi kukutukana kama unavyojitanabaisha... Kama siasa za maji taka huziwezi nakuasa usirudie tena kukaa kwenye ulingo wa siasa katika chaguzi zingine zijazo 2020, siasa ni kuchafuka hasaaa na kama una moyo wa nailoni kama wako utaungua tu....

Hahahaaa ati vijineno na vijembe vya uchaguzi 2015 bado umevikumbatia moyoni... Rudi bongo uishi tukufundishe aina ya siasa ngumu sio hizo za kwenye makaratasi hapo Uskochi...
 
Sioni tofauti kubwa ya alichoandika Yericko na alichoandika wewe, hakuna uongo bali ulichofanya ni kuliboresha andiko la Yericko au tuseme umejazia nyama kwa sababu alimopita Yericko nawewe ndimo ulimopitia.
Soma vizuri alichokiandika Yeriko ,yeriko kapotosha kuhusu hizo taasisi kuanzia muundo na namna zibavyotekeleza majukumu yake
 
Kuna bwana mmoja ni mkimbizi anaishi ughaibuni, naamini atachangia huko mbeleni, yeye amejipa umiliki wa mambo ya aina hii, hivyo hata siku moja hawezi kukubaliana na alichoandika mwingine, atakipinga na kuja na majibu yaleyale ya aliyempinga lakini atazunguka weeee mpaka mwisho anarudi palepale....


Anyway, bwana Kulikoni Ughaibuni, maprofesa wanaposoma tasnifu za wafunzwa wao huzingatia mambo mawili tu, nayo huitwa "dhanna" na "mantiki". Kama mwanafunzi ataweza kushawishi jopo la maprofesa hawa katika mambo hayo mawili basi huyo hujihesabu kuwa ni mzamivu.

Yasome maandishi yako kisha chambua dhanna na mantiki ya andiko langu, kwahakika ungeikosa sifa ya uzamivu.

Wewe ni msomi na ninafahamu umepata Phd hapo ya siasa, kibaya zaidi kwenye andiko langu umeachana kabisa na matumizi ya uwanda wako na kujivika hasira za mkizi...


Shukrani sana kwa mchango wako mkuu, mpaka tarehe 15 mwezi huu nitamaliza kusoma kitabu cha Shushushu kilichoandikwa na kada mtiifu wa ccm aitwaye Evarist Chahali. Ni kizuri japo kina makosa ya kimantiki na kidhanna.
Kukubali makosa sio dhambi ,maelezo uliyotoa kuhusu hizo taasisi hayakua sawa ,et inaweza kuwa na watu watano tu na wanaweza kuwa ndugu au rafiki wa kiongozi .Yeriko kwenye hilo bandiko hukuwa sahihi
 
Kuna hitajika tafsiri mpya ya kiswahili ili kukubaliana na hoja, kusema kisicho cha kisheria hakuna maana kwamba anayekiongoza hayupo kisheria...

Mfano Idara ya Usalama Tanzania (TISS) tangu baada na kabla ya Uhuru haikuwa kisheria, lakini ilifanya kazi zote kama idara ya ujasusi tu. Miaka yote ilikuwa ni kitengo ndani ya Jeshi la Polisi ikiitwa Tawi Maalumu (Special Branch SB) mpaka Mzee Mkapa alipokuja kuiweka kisheria na kuiita Tanzania Intelligence and Security Service (TISS).

Sasa watu kama akina Chahali ukiwambia TISS iliendesha shughuli zake in black space yaani kiharamu, watakukatalia na kukuletea maandishi mareeeefu na milinks ya Google kujihalalishia kile wakisemacho....

taasis kutokuwepo kisheria maana yake haitambuliwi na sheria yoyote au haijawa attached kwenye taasis inayotambuliwa kisheria. Lakini administratively zinaundwa taasis ndani ya taasis like hzo SAD na KIDON.

Chukua mf afrika kusini wakati wa Mbeki alikua na 'baraza la mawaziri' lisilo rasmi. Hili liliundwa na watu mashuhuri na madon wa S.A na walikua na maamuz ambayo serikali iliyatekeleza.
 
Leo kuna ubatizo wa majasusi stay tuned.
 
Mnakimbilia sana utamaduni wa magharibi tujenge nchi yetu na maneno mepesi ya kueleweka Kwa hadhira pana

Yericko wew ni mwandishi mzuri sana tabia yako ya kuipenda sana marekani na kuitolea mifana huo ni utumwa wa fikira

Kule twitter umepost habari za kitabu cha fire and fury sasa nikuulize tu maudhui ya kitabu hicho yanamsaidia nn mkulima wa korosho au wananchi wa kawaida wanaoishi Kwa mlo mmoja na pengine Kwa kutegemea ruzuku kutoka Kwa wahisani ndugu na jamaa

Badilikeni

Kijana msomi kama wewe unapaswa kumulika matatizo ya taifa lako na kuyasemea wazi Kwa hadhira bila kumung' unya maneno

Mossad inamsaidia nn mamantilie anaehangaishwa na mgambo wa jiji ?


Bila katiba mpya iliyopendekezwa na wananchi hakuna jambo lolote la maana unaweza kuongea likapata mashiko.
 
Back
Top Bottom