National Interest: Marekani itashindwa na China katika vita juu ya mgogoro wa Taiwan

National Interest: Marekani itashindwa na China katika vita juu ya mgogoro wa Taiwan

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
9,846
Reaction score
20,319
National Interest: Marekani itashindwa na China katika vita juu ya mgogoro wa Taiwan

Jarida la National Interest limewanukuu maafisa wa zamani na wa sasa wa masuala ya ulinzi nchini Marekani wakitahadharisha kwamba, Washington itashindwa na Beijing iwapo kutatokea vita juu ya eneo la Taiwan.

Mivutano baina ya Marekani na China kuhusu kisiwa cha Taiwan ambao ulichochewa na rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump kwa kutuma meli za kivita katika mlango bahari wa Taiwain na kuiuzia silaha seriikali ya kisiwa hicho, umepamba moto zaidi katika kipindi cha sasa cha utawala wa Rais Joe Biden baada ya kiongozi huyo kuahidi kwamba, atailinda Taiwan iwapo itashambuliwa na China.

Graham Allison ambaye ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Harvard ameandika katika jarida la National Interest kwamba uchambuzi wa maafisa wa ulinzi wa zamani na wa sasa nchini Marekani umetahadharisha kuwa, nchi hiyo inapaswa kukubaliana na ukweli wa mambo kwamba si nguvu kubwa tena ya kijeshi katika eneo la Magharibi mwa Oceania.

Allison ameashiria uchambuuzi na tathmini za karibuni za maafisa wa sasa na wa zamani wa ngazi za juu wa Marekani kama mkuu wa zamani wa majeshi ya Marekani, James Winfeld na mkurugenzi wa zamani wa shirika la ujasusi la CIA, Michael Morel juu ya uwezekano wa kutokea vita juu ya kisiwa cha Taiwan ambao wamesisitiza kuwa, jeshi la China linaweza kuchukua hatua dhidi ya Taiwan wakati wowote.
 
Haya mambo Biden hayawezi.

Taliban walimuona kama mdori tu wakachukua nchi fasta.

Sasa China ndio wanamuonaje sijui 😂😂

Mbabe alikuwa ni Trump, huko Afghanistan hakuna aliethubutu kufanya ujinga kipondi chake, Biden mdori kaingia, Taleban wakaona huyu mdori tu
 
Haya mambo Biden hayawezi.

Taliban walimuona kama mdori tu wakachukua nchi fasta.

Sasa China ndio wanamuonaje sijui [emoji23][emoji23]

Mbabe alikuwa ni Trump, huko Afghanistan hakuna aliethubutu kufanya ujinga kipondi chake, Biden mdori kaingia, Taleban wakaona huyu mdori tu
Siku Simba akiacha tabia za kuua wanyama wengine na kuwala nyama huku akishushia na damu ya moto, basi hata kondoo atakuwa anamvimbia Simba. Marekani siyo kuwa nguvu zimepungua au nchi nyingine hazipigiki, ila kuanzia Bush aondoke, maraisi walifuata wamekuwa kama watawa, upole mwingi na mazungumzo.

Marekani anapaswa aongee kwa makombora na drones, lugha hii hueleweka vizuri sana.
 
Ninahakika kikiwaka Marekani atamtelekeza Taiwan kama ilivyo ada yake.
 
IMG_1355.jpg

Ujumbe kutoka Taiwan
 
Haya mambo Biden hayawezi.

Taliban walimuona kama mdori tu wakachukua nchi fasta.

Sasa China ndio wanamuonaje sijui [emoji23][emoji23]

Mbabe alikuwa ni Trump, huko Afghanistan hakuna aliethubutu kufanya ujinga kipondi chake, Biden mdori kaingia, Taleban wakaona huyu mdori tu

Missions za US kwenye ardhi ya waarabu sio mpango wa Rais,
 
Haya mambo Biden hayawezi.

Taliban walimuona kama mdori tu wakachukua nchi fasta.

Sasa China ndio wanamuonaje sijui 😂😂

Mbabe alikuwa ni Trump, huko Afghanistan hakuna aliethubutu kufanya ujinga kipondi chake, Biden mdori kaingia, Taleban wakaona huyu mdori tu
Trump kiboko yake Kiduku tu.

Aliambiwa na Kiduku "jaribu kurusha risasi moja tu Pyongyang halafu uone"

Akasanda.

Trump nyanya tu,alikimbia Syria.
 
Siku Simba akiacha tabia za kuua wanyama wengine na kuwala nyama huku akishushia na damu ya moto, basi hata kondoo atakuwa anamvimbia Simba. Marekani siyo kuwa nguvu zimepungua au nchi nyingine hazipigiki, ila kuanzia Bush aondoke, maraisi walifuata wamekuwa kama watawa, upole mwingi na mazungumzo.
Marekani anapaswa aongee kwa makombora na drones, lugha hii hueleweka vizuri sana.
We unachekesha kweli unafikiri China ni nchi ya kiarabu kwamba inapigika kiraisi

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
 
Siku Simba akiacha tabia za kuua wanyama wengine na kuwala nyama huku akishushia na damu ya moto, basi hata kondoo atakuwa anamvimbia Simba. Marekani siyo kuwa nguvu zimepungua au nchi nyingine hazipigiki, ila kuanzia Bush aondoke, maraisi walifuata wamekuwa kama watawa, upole mwingi na mazungumzo.
Marekani anapaswa aongee kwa makombora na drones, lugha hii hueleweka vizuri sana.
Mmarekani muoga sana kupigana na nchi ambayo anajua nayo inauwezo wa kumtandika kwake. Hizo drones na makombora akimgusa mchina nae anapelekewa moto. Mambo yamebadilika kwa kasi sana sahivi nae kabaki anahubiri tu
 
Mmarekani muoga sana kupigana na nchi ambayo anajua nayo inauwezo wa kumtandika kwake. Hizo drones na makombora akimgusa mchina nae anapelekewa moto. Mambo yamebadilika kwa kasi sana sahivi nae kabaki anahubiri tu
Mchina kashakomaa, vinchi vingine ni kuvikata pembe mapema.
 
Kupigana vita kunahitaji nchi iwe na uchumi imara na thabiti vinginevyo inakuwa yale yaleee ya mwalimu na iid Amin baada ya vita uchumi wa nchi ulidorora mno kama si kuanguka
 
Siku Simba akiacha tabia za kuua wanyama wengine na kuwala nyama huku akishushia na damu ya moto, basi hata kondoo atakuwa anamvimbia Simba. Marekani siyo kuwa nguvu zimepungua au nchi nyingine hazipigiki, ila kuanzia Bush aondoke, maraisi walifuata wamekuwa kama watawa, upole mwingi na mazungumzo.
Marekani anapaswa aongee kwa makombora na drones, lugha hii hueleweka vizuri sana.
Talking is cheap - Merikani zamani sio siku hizi,na akileta ujinga wake aliyo zoea kwa miaka nenda rudi wa kuvamia/shambulia mataifa dhaifu kijeshi (Banana Republics) kama Majenerali wa USA watafanya ujinga wa kuishambulia aidha Uchina au Urusi, basi wajiweke tayari Taifa lao kushambuliwa vilivyo kwa Mara ya kwanza tangu USA ipate Uhuru kwenye miaka ya 1770s.

USA wasitegemee kwamba vita hiyo itapiganwa na kuishia Ulaya na Asia tu, hapana - juzi juzi hapa niliwasikia Waziri wa ulinzi was USA pamoja na maafisa wengine wa kijeshi wakilalamika kwamba Wachina wamefanya majaribio ya glide vehicle zenye uwezo mkubwa wa kubeba thermonuclear bomb si hilo tu makombora hayo yatarushwa kwa kupitia "South Pole" na kwenda kushambulia designated targets ndani ya Merikani kwenyewe, wala Amerika haina kinga dhidi ya makombora kama hayo hatarishi, wao miaka yote wali concentrate kuweka kinga dhidi ya makombora ya ICBM huko Alaska wakasahua kwamba Wachina na Warusi wana uwezo mkubwa wa kurusha makombora kupitia South Pole yakahibukia Mexico na kushambulia Merikani.

Mwaka jana niliwasikia Majenerali wa jeshi la Urusi wakisema wanamiliki makombora ya kupitia mashariki na magharibi na kwenda kushambulia USA, hapo hatuja taja kuhusu hypersonic missiles za Korea Kasikazini - ukweli ni kwamba huko tunako elekea Merikani ijaribu kujitafakari upya kuhusu mwenendo wake wa kutishia tishia Uchina, Urusi na Korea Kasikazini.
 
Back
Top Bottom