NATO ipo katika wakati mgumu sana kuikoa Ukraine

NATO ipo katika wakati mgumu sana kuikoa Ukraine

100 others

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2017
Posts
4,766
Reaction score
16,191
1940 May ulitokea mvutano mkubwa wa baraza la mawaziri nchini Uingereza baina ya pande mbili, upande mmoja ilikuwa wakiunga mkono kuongea amani na Germany na upande mmoja waliunga mkono kuendelea na vita.

Waziri mkuu wa kipindi hicho Bw Winston Churchill ndiye alikuwa akiongoza ule upande unaunga mkono kuendelea na vita dhidi ya Germany, huku ule upande mmoja wa waliokuwa wanaunga mkono kuongea mazungumzo ya amani na Germany ulikuwa ukiongozwa na Bw Lord Halif ambae alikuwa ni waziri wa mambo ya kigeni.

Ulikuwa ni mvutano wa kukata na shoka, mvutano ulikuwa mkubwa kiasi kwamba ni kama waliingia katika ugomvi huku upande wa Bw Lord Hafix ambao walipendelea kufanya mazungumzo na Hitler walitishia kuondoa uongozi wa Winston Churchill kuwa waziri mkuu.

Mvutano huu ni baada ya viongozi hao kufahamu nguvu aliyokuwa nayo Germany ilkuwa si mchezo, hivyo wasingeweza kukabiliana na Germany, hii ilidhihirika baada ya jeshi la Uingereza na France kuzungukwa na jeshi la Germany katika fukwe na bandari ya Dunkirk ambapo jeshi la Uingereza walifika France kwa ajili ya kuisaidia France dhidi ya uvamizi wa Germany.

main-qimg-12d1a4dd94c53ed33bed6de00be22d1a-lq

Askari wa Belgium, France na British walikuwa wamezungukwa pande zote na jeshi la Germany hapo fukwe na bandari za Dunkirk na sehemu pekee ya kutokea ilikuwa ni kuvuka bahari ya Atlantic kuelekea uingereza kupitia english channel.

Ndipo hapo ilifanyika operation dynamo wakiokolewa askari zaidi ya 338,000, wananchi wa Uingereza walijitolea kwenda kuokoa askari hao. Kuanzia wavuvi waliokuwa na mitumbwi, matajiri waliokuwa na yatchs na meli, watu binafsi, mashirika, meli za kivita n.k walijitoa kwenda kuokoa askari hao, tukio hilo hadi leo linafahamika kama maajabu ya Dunkirk, askari walikuwa wamekata tamaa wakisubiri muda ufike jeshi la Hitler kufika na kuwamaliza kikatili.

Kwa tukio hilo la Dunkirk lilipelekea kwa shemu kubwa baraza hilo kuvutana wakiona hawana uwezo kupambana na Germany.

Bw Lord Halifax ambae alikuwa kiongozi mpingaji wa maamuzi ya Winston Churchill kuhusu kukabiliana na vita na Germany endapo akiivamia Uingereza alipendekeza ni vyema amtumie rafiki wa karibu wa Hitler dictator Mussolini kufanya majadiliano na mazungumzo ya amani kutoingia vitani, hapo ndipo kuna ule msemo maarufu wa Winston ulichukua nafasi yake "Huwezi kujadiliana na tiger wakati kichwa chako kiko kinywani mwake".

Baada ya mvutano wa siku kadhaa walikubaliana maamuzi wanaingia vitani na Germany huku Bw Halifax akikubali mawazo ya Winston.

Kinachoendelea Ukraine ni kama inatukumbusha tukio hilo, nchi za NATO zipo katika mvutano mkubwa wakijadili wafanye nini kuikoa Ukraine toka mikononi mwa Russia, imedhihirika Ukraine hivi sasa licha ya kupewa pesa, kusaidiwa askari, silaha za kila aina ambazo ni superior kutoka west, air defenses, satellite n.k lakini bado game limekuwa gumu sana upande wa NATO.
Ukraine imepoteza pakubwa sana kuliko.

- Askari wa Ukraine wale walio na mafunzo ya hali ya juu, special forces wamekwenda na maji, wamepotezwa vitani kitu kinachoilazimu Ukraine ianze kutumia wananchi wasio na mafunzo, walevi mtaani, mateja, wazee na wagonjwa ndio wanapelekwa front tena kwa ulazima. Hii ni dalili mbaya sana, kama commandos wamelamba mchanga je hawa afya mgogoro wanaweza kukabiliana na jeshi la Russia?

- Vita hii imepoteza vijana wengi sana wadogo wenye nguvu ambao ndio wanategemewa na taifa la Uraine kama nguvu kazi, hii inaonyesha kwamba Ukraine itashuka sana kimapato, kwa sababu ndilo kundi linaloongoza kama walipa kodi wazuri, ina maana pato la taifa litapungua sehemu kubwa sana.

- Vifaa vya kivita, miundo mbinu, viwanda n.k vimeharibiwa sana kufikia point haiwezekani kwa marekebisho, hii itachukua muda mrefu sana kuja kurudisha vitu hivyo, hii ni hasara kubwa.

- Idadi ya watu kwa ujumla imeshuka tokana na madhara ya kivita.

Ndio maana hadi sasa tumeanza kuona viongozi kutoka nchi za NATO wakianza kutumia kuauli kwamba Ukraine ina haki kupiga ndani ya Russia ikitumia silaha zao, huku Russia ikijibu wasithubutu, tumeshuhudia pia Russia kutishia kutumia silaha za nuclear endapo tuusalama wake utakuwa matatani.

Pia tunazidi kusikia nchi za NATO zikidai kutuma vikosi vyao nchini Ukraine kukabiliana na Russia. Hii inaashiria kitu kimoja kwamba msaada wa silaha, pesa na vifaa hauna nafasi tena kuikoa Ukraine.

France imetangaza kupeleka askari wake Ukraine, tukumbuke pia France ndio wa kwanza kwenda kuiokoa Poland dhidi ya Germany WWII, kitu kilichopelekea France kupelekewa moto hadi Paris na Uingereza ilipoingia kati wakapelekewa moto hadi fukwe za Dunkirk walipotorokea na kutokomea kwa ngalawa kurudi nyumbani wakiwa hawaamini kama wamepona na kuiacha Germany ikiitawala France.

Lakini pia tukumbuke Russia ndio walimpelekea moto Germany kutoka mashariki hadi Berlin, huku West akiwepo USA, FRance na England wakiwa wanamkuta Russia tayari amefika ikulu Berlin.

Hii mistake ni kama France anairudia, kumbe history zinajirudia.

Je? Russia itakubali kupigwa mikwara kuacha kuendelea na mipango yake kuitandika Ukraine na kuweka kibaraka wake?

NATO watakubali kuona Ukraine walioishawishi iingie vitani na Russia ikichukuliwa na Russia huku wasifanye lolote?

NATO watakubali kudharaulika na kumponza kibaraka wao Zelensky ambae walimuahidi kuishinda Russia?

Kwa maana Russia ikiacha NATO kushinda hii vita ni kuiruhusu Ukraine kuingia kwenye muungano na NATO, na hili litatokea haraka sana, Je Russia itakubali NATO kukaa karibu na mipaka yake?

Maswali ni mengi. Na situation inaogofya. Tusubiri.
 
Labda matokeo tarajiwa ni tofauti kabisa na jinsi yanavyoonekana kwa sasa.

Inawezekana sana kwamba East, West, North na South wote wana lao jambo moja lilelile.

Haimantikiki wala haiaminiki, ila inawezekana.

Muda utaongea wenyewe.
Jambo lipi mkuu.
 
Tutaenda kusini mashariki na kwingineko hapa duniani MBABE NI URUSI hebu fikiria watu wenye uchumi mkubwa wababe wanakutana wanachangia silaha na pesa lakini bado mchangiwaji kapigwa hadi kugalagazwa yoote tisa lakini kumi ni pale Urusi ilipoitwanga Ujerumani wakati wa WWII na ndo ikawa mwisho wa Hitler jambo hili siyo jepesi hata kidogo nchi za ulaya zilipitia untold story wanaokolewa na Urusi halafu leo kuna watoto umri wa 18 hadi 30 ambao wameishia kumeza notisi za historia mwenemutapa, the U shaped Chaka's military tactics hawajui lolote kuhusu hii dunia
 
Lakini pia tukumbuke Russia ndio walimpelekea moto Germany kutoka mashariki hadi Berlin, huku West akiwepo USA, FRance na England wakiwa wanamkuta Russia tayari amefika ikulu Berlin.
Misaada inayotolewa na wanachama wa NATO kwa Ukraine haina tofauti na misaada iliyotolewa na Marekani na washirika wengine kwa USSR ilipokuwa ikipambana na uvamizi wa Adolf Hitler kipindi cha Vita ya Pili ya Dunia. Soma Lend-Lease Act ya mwaka 1941.

Bila msaada wa Marekani na allies wengine, Muscovites wangekuwa wanazungumza kijerumani hivi sasa kama ambavyo Wabrazil wanazungumza kireno.
 
Tutaenda kusini mashariki na kwingineko hapa duniani MBABE NI URUSI hebu fikiria watu wenye uchumi mkubwa wababe wanakutana wanachangia silaha na pesa lakini bado mchangiwaji kapigwa hadi kugalagazwa yoote tisa lakini kumi ni pale Urusi ilipoitwanga Ujerumani wakati wa WWII na ndo ikawa mwisho wa Hitler jambo hili siyo jepesi hata kidogo nchi za ulaya zilipitia untold story wanaokolewa na Urusi halafu leo kuna watoto umri wa 18 hadi 30 ambao wameishia kumeza notisi za historia mwenemutapa, the U shaped Chaka's military tactics hawajui lolote kuhusu hii dunia
Maneno ya kiongozi wa zamani wa Soviet Union (Russia):

Lend-Lease 1.png
 
Misaada inayotolewa na wanachama wa NATO kwa Ukraine haina tofauti na misaada iliyotolewa na Marekani na washirika wengine kwa USSR ilipokuwa ikipambana na uvamizi wa Adolf Hitler kipindi cha Vita ya Pili ya Dunia. Soma Lend-Lease Act ya mwaka 1941.

Bila msaada wa Marekani na allies wengine, Muscovites wangekuwa wanazungumza kijerumani hivi sasa kama ambavyo Wabrazil wanazungumza kireno.
Hata hivi sasa unaweza kusema pasipo Iran kumpatia silaha Russia basi Russia haiwezi kushinda vita.
Russia aliwaambia mapema sana west tusipoungana kumkabili Hitler itakuwa ngumu, west walimtenga na kukataa mawazo yake kisa ana sera za kijamaa, baada ya Germany kumvamia Soviet ndipo vita ikaanza kati ya Germany na Russia.

Hapo unaona kabisa USA na wenzake walishamkataa Soviet kama ally mwenzao kumkabili Germany.

Kuhusu hio lend lease programme mnufaika mkubwa alikuwa ni Great Britain, je aliishinda Germany?

Sasa hivi NATO inamsaidia Ukraine pesa na silaha za kutosha je wamemshinda Russia?

Stalin alishasema Soviet imelipa damu kwenye vita, USA imelipa pesa, GB imelipa muda, nadhani umeelewa maana yake.
Soviet asingejihusisha na hio vita USA asingeweza ishinda Germany.
 
Maneno ya kiongozi wa zamani wa Soviet Union (Russia):

View attachment 3010234
Aliyekwenda kuomba msaada USA wa pesa na silaha ni Great Britain, mwishoni mwa 1940 Great Britain juhudi zake kupambana na Germany zilifikia sehemu mbaya, hawakuwa na pesa, akiba waliyokuwa wanategemea ilikuwa inakwenda kuisha.
Mwaka huo ndipo balozi wa Uingereza nchini USA akaenda kufanya press na waandishi akiwaambia Uingereza ipo kwenye hali mbaya kiuchumi na vita inakuwa ngumu hivyo wanahitaji pesa, baadae Winston mwenyewe waziri mkuu wa Uingereza alituma barua kwenda kwa Roosevelt rais wa US, akiomba msaada hapo ni 1940.

Nilishakuambia toka mwanzo Russia walipigana kimpango wao baada ya west kujikuta wanamtenga kwa sababu ni wajamaa, wakidhani atakuja kuwapigia magoti, lakini wao ndio walifahamu wanahitaji msaada wa Soviet, na hapo ndipo wakaanza kutoa hio misaada pasipo kuombwa.
Lend lease programme US waliiweka Soviet mwishoni mwa mwaka 1942, kuanzia 1941 Russia inapigana peke yake na Germany baada ya Germany kuanzisha Operation Barbarossa kuivamia Soviet.

USA anaingia vitani mwishoni mwa 1942 december, muda huo pia ndipo anatambua maneno ya Stalin kabla ya vita kuanza kwamba wanahitaji ushikiano kumkabili Germany.
US ilikuwa bado ina pesa, kuanzia 1939 USA haikujihusisha na vita.

Programme hio ilisaidia nchi nyingi tu ikiwemo China, Australia, New Zealand n.k je walishinda vitadhidi ya Germany?

USA anaanza kumtabua Soviet kama ally baadae sana.

Stalin alizungumza kutoa credits, kwa kauli y umoja kama allies.

Askari wengi wa Germany walifia mashariki ambapo ndipo Russia alikuwa akipambana unafamu hilo? Askari wengi wafungwa wa kivita walifia magerezani kwa USSR, nikikuletea takwimu hapa utashangaa.

Tazama hapo chini
main-qimg-f7610c291496f54cdc10e8e869fc3c7b-lq

main-qimg-42d482347523929061fa302467a6abe1-lq


Soviet ilikua ni mashine ya mauaji.

We endelea kukaa hapo kwenye kahawa mkidanganyana.
 
Aliyekwenda kuomba msaada USA wa pesa na silaha ni Great Britain, mwishoni mwa 1940 Great Britain juhudi zake kupambana na Germany zilifikia sehemu mbaya, hawakuwa na pesa, akiba waliyokuwa wanategemea ilikuwa inakwenda kuisha.
Mwaka huo ndipo balozi wa Uingereza nchini USA akaenda kufanya press na waandishi akiwaambia Uingereza ipo kwenye hali mbaya kiuchumi na vita inakuwa ngumu hivyo wanahitaji pesa, baadae Winston mwenyewe waziri mkuu wa Uingereza alituma barua kwenda kwa Roosevelt rais wa US, akiomba msaada hapo ni 1940.

Nilishakuambia toka mwanzo Russia walipigana kimpango wao baada ya west kujikuta wanamtenga kwa sababu ni wajamaa, wakidhani atakuja kuwapigia magoti, lakini wao ndio walifahamu wanahitaji msaada wa Soviet, na hapo ndipo wakaanza kutoa hio misaada pasipo kuombwa.
Lend lease programme US waliiweka Soviet mwishoni mwa mwaka 1942, kuanzia 1941 Russia inapigana peke yake na Germany baada ya Germany kuanzisha Operation Barbarossa kuivamia Soviet.

USA anaingia vitani mwishoni mwa 1942 december, muda huo pia ndipo anatambua maneno ya Stalin kabla ya vita kuanza kwamba wanahitaji ushikiano kumkabili Germany.
US ilikuwa bado ina pesa, kuanzia 1939 USA haikujihusisha na vita.

Programme hio ilisaidia nchi nyingi tu ikiwemo China, Australia, New Zealand n.k je walishinda vitadhidi ya Germany?

USA anaanza kumtabua Soviet kama ally baadae sana.

Stalin alizungumza kutoa credits, kwa kauli y umoja kama allies.

Askari wengi wa Germany walifia mashariki ambapo ndipo Russia alikuwa akipambana unafamu hilo? Askari wengi wafungwa wa kivita walifia magerezani kwa USSR, nikikuletea takwimu hapa utashangaa.

Tazama hapo chini
main-qimg-f7610c291496f54cdc10e8e869fc3c7b-lq

main-qimg-42d482347523929061fa302467a6abe1-lq


Soviet ilikua ni mashine ya mauaji.

We endelea kukaa hapo kwenye kahawa mkidanganyana.
Nilidhani unatoa hoja bila kuegemea upande wowote kumbe unayo majibu tayari. Unaweza kupima nguvu ya Ujerumani na USSR kwa wakati huo na nguvu Urusi na Ukraine kwa wakati huu?
Tupunguze ushabiki ili tuwe objective.
Swali dogo tu, ni sehemu gani inaonesha kuwa NATO walimshawishi Ukraine kuingia vitani na Russia kama ulivyoandika kwenye andiko lako la kwanza.
 
Hata hivi sasa unaweza kusema pasipo Iran kumpatia silaha Russia basi Russia haiwezi kushinda vita.
Russia aliwaambia mapema sana west tusipoungana kumkabili Hitler itakuwa ngumu, west walimtenga na kukataa mawazo yake kisa ana sera za kijamaa, baada ya Germany kumvamia Soviet ndipo vita ikaanza kati ya Germany na Russia.

Hapo unaona kabisa USA na wenzake walishamkataa Soviet kama ally mwenzao kumkabili Germany.

Kuhusu hio lend lease programme mnufaika mkubwa alikuwa ni Great Britain, je aliishinda Germany?

Sasa hivi NATO inamsaidia Ukraine pesa na silaha za kutosha je wamemshinda Russia?

Stalin alishasema Soviet imelipa damu kwenye vita, USA imelipa pesa, GB imelipa muda, nadhani umeelewa maana yake.
Soviet asingejihusisha na hio vita USA asingeweza ishinda Germany.
Great Britain iliishinda Germany mapema kabla hata ya uvamizi wa Hitler dhidi ya USSR. Soma kile kilichoikumba Luftwaffe (Nazi Germany air force) kwenye Battle of Britain. Ushindi wa allies kwenye Vita ya Pili ya Dunia ulipatikana kwa namna nyingi na Great Britain ilipambana zaidi vita ya kujilinda (defensive war) dhidi ya Hitler.

Wanazuoni na wanahistoria wengi wanakubaliana kuwa anguko la kwanza la Nazi Germany ni baada ya kushindwa vita ya anga dhidi ya Great Britain mwaka 1940.

Wakati Great Britain inapambana na Hitler, USSR ilikuwa imeingia kwenye makubaliano na Hitler (1939) ya kutovamiana (non-aggression pact). Mara baada ya makubaliano, USSR ilishirikiana na Hitler kuigawa Ulaya ya Mashariki kupitia vita za upanuzi wa mipaka (expansionism). Soma Molotov-Ribbentrop Pact.

Hiyo Russia unayosema iliwaambia "West" waungane kumkabili Hitler ndiyo Russia (USSR) hiyohiyo iliyoungana na Hitler kuivamia na kuigawa Poland mwaka 1939 bila kujua kuwa Hitler alikuwa na mipango na malengo yake mengine tofauti na makubaliano yao.

Baada ya USSR "kuzidiwa kete" na Hitler (Operation Barbarossa) ndipo USSR ikavunja uhusiano na Nazi Germany kisha ikaungana na Great Britain, USA n.k. dhidi ya Hitler.
 
Aliyekwenda kuomba msaada USA wa pesa na silaha ni Great Britain, mwishoni mwa 1940 Great Britain juhudi zake kupambana na Germany zilifikia sehemu mbaya, hawakuwa na pesa, akiba waliyokuwa wanategemea ilikuwa inakwenda kuisha.
Mwaka huo ndipo balozi wa Uingereza nchini USA akaenda kufanya press na waandishi akiwaambia Uingereza ipo kwenye hali mbaya kiuchumi na vita inakuwa ngumu hivyo wanahitaji pesa, baadae Winston mwenyewe waziri mkuu wa Uingereza alituma barua kwenda kwa Roosevelt rais wa US, akiomba msaada hapo ni 1940.

Nilishakuambia toka mwanzo Russia walipigana kimpango wao baada ya west kujikuta wanamtenga kwa sababu ni wajamaa, wakidhani atakuja kuwapigia magoti, lakini wao ndio walifahamu wanahitaji msaada wa Soviet, na hapo ndipo wakaanza kutoa hio misaada pasipo kuombwa.
Lend lease programme US waliiweka Soviet mwishoni mwa mwaka 1942, kuanzia 1941 Russia inapigana peke yake na Germany baada ya Germany kuanzisha Operation Barbarossa kuivamia Soviet.

USA anaingia vitani mwishoni mwa 1942 december, muda huo pia ndipo anatambua maneno ya Stalin kabla ya vita kuanza kwamba wanahitaji ushikiano kumkabili Germany.
US ilikuwa bado ina pesa, kuanzia 1939 USA haikujihusisha na vita.

Programme hio ilisaidia nchi nyingi tu ikiwemo China, Australia, New Zealand n.k je walishinda vitadhidi ya Germany?

USA anaanza kumtabua Soviet kama ally baadae sana.

Stalin alizungumza kutoa credits, kwa kauli y umoja kama allies.

Askari wengi wa Germany walifia mashariki ambapo ndipo Russia alikuwa akipambana unafamu hilo? Askari wengi wafungwa wa kivita walifia magerezani kwa USSR, nikikuletea takwimu hapa utashangaa.

Tazama hapo chini
main-qimg-f7610c291496f54cdc10e8e869fc3c7b-lq

main-qimg-42d482347523929061fa302467a6abe1-lq


Soviet ilikua ni mashine ya mauaji.

We endelea kukaa hapo kwenye kahawa mkidanganyana.
Soviet Union (Russia) ilitengwa kwa sababu ya sera zake za kujiongezea mipaka (expansionism). Na ilishirikiana na Hitler kuigawa Central na Eastern Europe kabla ya uvamizi wa Hitler dhidi ya Soviet Union.

Marekani iliona haja ya kuisaidia Soviet Union baada ya uhusiano wa Soviet Union na Nazi Germany kuvunjika ukichochewa na uvamizi wa Hitler dhidi ya Soviet Union.

"The enemy of my enemy is my friend".
 
Nilidhani unatoa hoja bila kuegemea upande wowote kumbe unayo majibu tayari. Unaweza kupima nguvu ya Ujerumani na USSR kwa wakati huo na nguvu Urusi na Ukraine kwa wakati huu?
Tupunguze ushabiki ili tuwe objective.
Swali dogo tu, ni sehemu gani inaonesha kuwa NATO walimshawishi Ukraine kuingia vitani na Russia kama ulivyoandika kwenye andiko lako la kwanza.
Kama historia ndivyo ilivyo isisemwe?

Kwani Urusi imewafanyaje? Mbona ikiweka historia ya kuonekana yeye ni mshindi wengine mnaghadhibika?
 
Great Britain iliishinda Germany mapema kabla hata ya uvamizi wa Hitler dhidi ya USSR. Soma kile kilichoikumba Luftwaffe (Nazi Germany air force) kwenye Battle of Britain. Ushindi wa allies kwenye Vita ya Pili ya Dunia ulipatikana kwa namna nyingi na Great Britain ilipambana zaidi vita ya kujilinda (defensive war) dhidi ya Hitler.

Wanazuoni na wanahistoria wengi wanakubaliana kuwa anguko la kwanza la Nazi Germany ni baada ya kushindwa vita ya anga dhidi ya Great Britain mwaka 1940.

Wakati Great Britain inapambana na Hitler, USSR ilikuwa imeingia kwenye makubaliano na Hitler (1939) ya kutovamiana (non-aggression pact). Mara baada ya makubaliano, USSR ilishirikiana na Hitler kuigawa Ulaya ya Mashariki kupitia vita za upanuzi wa mipaka (expansionism). Soma Molotov-Ribbentrop Pact.

Hiyo Russia unayosema iliwaambia "West" waungane kumkabili Hitler ndiyo Russia (USSR) hiyohiyo iliyoungana na Hitler kuivamia na kuigawa Poland mwaka 1939 bila kujua kuwa Hitler alikuwa na mipango na malengo yake mengine tofauti na makubaliano yao.

Baada ya USSR "kuzidiwa kete" na Hitler (Operation Barbarossa) ndipo USSR ikavunja uhusiano na Nazi Germany kisha ikaungana na Great Britain, USA n.k. dhidi ya Hitler.
USSR iliamua kuwa ally na Germany baada ya kuona west wanamkataa, akaamua kusaini huo mkataba Molotov–Ribbentrop Pact ya kwamba wasivamiane kijeshi. Alitumia akili, lakini Hitler alipoavunja makubaliano ilibidi aingie nae vitani kumbuka kwamba USSR hawakutaka vita na Germany, walifahamu jeshi la Germany lina nguvu kiasi gani, hata USA hakuingia vitani mpaka pale ally wa Germany ambae ni Japan alipoivamia Pearl Harbor.

USA haikuthubutu kuingia na kutangaza vita dhidi ya wanazi mpaka pale aliposhambuliwa kwenye ardhi yake na Japan. USSR pia haikuona sababu ya kuingia vitani na Germany hadi pale Germany alipoishambulia USSR.

Kuhusu Britain tayari ilikuwa na hali mbaya, ndipo wakatuma balozi yao USA kuomba msaada wa fedha na silaha, baadae WInston mwenyewe alimtumia barua Roosevelt kwamba anahitaji msaada, haikupita muda ndipo Japan anaishambulia USA na kusababisha USA aungane na Britain iliyokuwa imechoka mbaya wanakaribia kukata roho kwenda kumuokoa France ambae tayari alikuwa chini ya Germany.

Hapo Britain alishatuma askari wake kwenda France kukabiliana na Germany na nchi washirika kama Belgium n.k lakini hawakufua dafu mbele ya Germany walitandikwa hadi kuzungukwa Dunkirk.

Sasa hio nguvu ya Britain sielewi inatokea wapi.

Wachambuzi wa kivita wanasema Germany ilikuwa inakwenda kummaliza Britain, ndipo Germany akageuka kwenda kupambana na USSR akijua Britain amejiishia.
Nakubaliana na wewe Air Royal Force ilijitahidi kupambana na kupeleka mashambulizi Germany japo ni ukweli usiopingika Britain ilikuwa kidogo inakata roho endapo tu USA (i) asingetoa msaada wa silaha (ii) USSR na USA kuingia vitani.
 
Soviet Union (Russia) ilitengwa kwa sababu ya sera zake za kujiongezea mipaka (expansionism). Na ilishirikiana na Hitler kuigawa Central na Eastern Europe kabla ya uvamizi wa Hitler dhidi ya Soviet Union.

Marekani iliona haja ya kuisaidia Soviet Union baada ya uhusiano wa Soviet Union na Nazi Germany kuvunjika ukichochewa na uvamizi wa Hitler dhidi ya Soviet Union.

"The enemy of my enemy is my friend".
Dah basi tumesoma vitabu tofauti kwa maana west walimtenga USSR kwa sababu moja kuu, sera za kijamaa, huko kujiongezea mipaka nadhani itakua ziada.


Elewa pia Stalin alikuwa anafahamu fika Hitler si mtu wa kuamini, hivyo alikwenda kuomba kusaini mkataba wa Molotov-Ribbentrop Pact akiwa na nia ya kununua muda kujijenga kijeshi, alimfahamu vyema Hitler, rejea Hitler alipovunja makubaliano ya Munich, soma Munich Agreement.

Hitler pia alivunja Anglo-German Naval Agreement na Chamberlain 1935, akavunja 1939.

Stalin hakuwa mjinga, licha ya makubaliano apewe sehemu Czech baadae akasem anaitaka na Poland ndipo France kujikuta Super power kuingili vita kutandikwa hadi aibu.
 
Dah basi tumesoma vitabu tofauti kwa maana west walimtenga USSR kwa sababu moja kuu, sera za kijamaa, huko kujiongezea mipaka nadhani itakua ziada.


Elewa pia Stalin alikuwa anafahamu fika Hitler si mtu wa kuamini, hivyo alikwenda kuomba kusaini mkataba wa Molotov-Ribbentrop Pact akiwa na nia ya kununua muda kujijenga kijeshi, alimfahamu vyema Hitler, rejea Hitler alipovunja makubaliano ya Munich, soma Munich Agreement.

Hitler pia alivunja Anglo-German Naval Agreement na Chamberlain 1935, akavunja 1939.

Stalin hakuwa mjinga, licha ya makubaliano apewe sehemu Czech baadae akasem anaitaka na Poland ndipo France kujikuta Super power kuingili vita kutandikwa hadi aibu.
Mkuu upo vizuri
Wengi history ya vita ya kwanza na ya pili wanalishwa Matango pori na west.
West kwenye propaganda wapo vizuri hata ukifuatilia hii vita ya Ukrein wanaongopa bila aibu.
Mwanaume Rusia yeye anatwanga tu kimyakimya.
Mara ooh hana silaha. Mara hana uchumi. Yeye ni mwendo wa kugonga tu
 
1940 May ulitokea mvutano mkubwa wa baraza la mawaziri nchini Uingereza baina ya pande mbili, upande mmoja ilikuwa wakiunga mkono kuongea amani na Germany na upande mmoja waliunga mkono kuendelea na vita.

Waziri mkuu wa kipindi hicho Bw Winston Churchill ndiye alikuwa akiongoza ule upande unaunga mkono kuendelea na vita dhidi ya Germany, huku ule upande mmoja wa waliokuwa wanaunga mkono kuongea mazungumzo ya amani na Germany ulikuwa ukiongozwa na Bw Lord Halif ambae alikuwa ni waziri wa mambo ya kigeni.

Ulikuwa ni mvutano wa kukata na shoka, mvutano ulikuwa mkubwa kiasi kwamba ni kama waliingia katika ugomvi huku upande wa Bw Lord Hafix ambao walipendelea kufanya mazungumzo na Hitler walitishia kuondoa uongozi wa Winston Churchill kuwa waziri mkuu.

Mvutano huu ni baada ya viongozi hao kufahamu nguvu aliyokuwa nayo Germany ilkuwa si mchezo, hivyo wasingeweza kukabiliana na Germany, hii ilidhihirika baada ya jeshi la Uingereza na France kuzungukwa na jeshi la Germany katika fukwe na bandari ya Dunkirk ambapo jeshi la Uingereza walifika France kwa ajili ya kuisaidia France dhidi ya uvamizi wa Germany.

main-qimg-12d1a4dd94c53ed33bed6de00be22d1a-lq

Askari wa Belgium, France na British walikuwa wamezungukwa pande zote na jeshi la Germany hapo fukwe na bandari za Dunkirk na sehemu pekee ya kutokea ilikuwa ni kuvuka bahari ya Atlantic kuelekea uingereza kupitia english channel.

Ndipo hapo ilifanyika operation dynamo wakiokolewa askari zaidi ya 338,000, wananchi wa Uingereza walijitolea kwenda kuokoa askari hao. Kuanzia wavuvi waliokuwa na mitumbwi, matajiri waliokuwa na yatchs na meli, watu binafsi, mashirika, meli za kivita n.k walijitoa kwenda kuokoa askari hao, tukio hilo hadi leo linafahamika kama maajabu ya Dunkirk, askari walikuwa wamekata tamaa wakisubiri muda ufike jeshi la Hitler kufika na kuwamaliza kikatili.

Kwa tukio hilo la Dunkirk lilipelekea kwa shemu kubwa baraza hilo kuvutana wakiona hawana uwezo kupambana na Germany.

Bw Lord Halifax ambae alikuwa kiongozi mpingaji wa maamuzi ya Winston Churchill kuhusu kukabiliana na vita na Germany endapo akiivamia Uingereza alipendekeza ni vyema amtumie rafiki wa karibu wa Hitler dictator Mussolini kufanya majadiliano na mazungumzo ya amani kutoingia vitani, hapo ndipo kuna ule msemo maarufu wa Winston ulichukua nafasi yake "Huwezi kujadiliana na tiger wakati kichwa chako kiko kinywani mwake".

Baada ya mvutano wa siku kadhaa walikubaliana maamuzi wanaingia vitani na Germany huku Bw Halifax akikubali mawazo ya Winston.

Kinachoendelea Ukraine ni kama inatukumbusha tukio hilo, nchi za NATO zipo katika mvutano mkubwa wakijadili wafanye nini kuikoa Ukraine toka mikononi mwa Russia, imedhihirika Ukraine hivi sasa licha ya kupewa pesa, kusaidiwa askari, silaha za kila aina ambazo ni superior kutoka west, air defenses, satellite n.k lakini bado game limekuwa gumu sana upande wa NATO.
Ukraine imepoteza pakubwa sana kuliko.

- Askari wa Ukraine wale walio na mafunzo ya hali ya juu, special forces wamekwenda na maji, wamepotezwa vitani kitu kinachoilazimu Ukraine ianze kutumia wananchi wasio na mafunzo, walevi mtaani, mateja, wazee na wagonjwa ndio wanapelekwa front tena kwa ulazima. Hii ni dalili mbaya sana, kama commandos wamelamba mchanga je hawa afya mgogoro wanaweza kukabiliana na jeshi la Russia?

- Vita hii imepoteza vijana wengi sana wadogo wenye nguvu ambao ndio wanategemewa na taifa la Uraine kama nguvu kazi, hii inaonyesha kwamba Ukraine itashuka sana kimapato, kwa sababu ndilo kundi linaloongoza kama walipa kodi wazuri, ina maana pato la taifa litapungua sehemu kubwa sana.

- Vifaa vya kivita, miundo mbinu, viwanda n.k vimeharibiwa sana kufikia point haiwezekani kwa marekebisho, hii itachukua muda mrefu sana kuja kurudisha vitu hivyo, hii ni hasara kubwa.

- Idadi ya watu kwa ujumla imeshuka tokana na madhara ya kivita.

Ndio maana hadi sasa tumeanza kuona viongozi kutoka nchi za NATO wakianza kutumia kuauli kwamba Ukraine ina haki kupiga ndani ya Russia ikitumia silaha zao, huku Russia ikijibu wasithubutu, tumeshuhudia pia Russia kutishia kutumia silaha za nuclear endapo tuusalama wake utakuwa matatani.

Pia tunazidi kusikia nchi za NATO zikidai kutuma vikosi vyao nchini Ukraine kukabiliana na Russia. Hii inaashiria kitu kimoja kwamba msaada wa silaha, pesa na vifaa hauna nafasi tena kuikoa Ukraine.

France imetangaza kupeleka askari wake Ukraine, tukumbuke pia France ndio wa kwanza kwenda kuiokoa Poland dhidi ya Germany WWII, kitu kilichopelekea France kupelekewa moto hadi Paris na Uingereza ilipoingia kati wakapelekewa moto hadi fukwe za Dunkirk walipotorokea na kutokomea kwa ngalawa kurudi nyumbani wakiwa hawaamini kama wamepona na kuiacha Germany ikiitawala France.

Lakini pia tukumbuke Russia ndio walimpelekea moto Germany kutoka mashariki hadi Berlin, huku West akiwepo USA, FRance na England wakiwa wanamkuta Russia tayari amefika ikulu Berlin.

Hii mistake ni kama France anairudia, kumbe history zinajirudia.

Je? Russia itakubali kupigwa mikwara kuacha kuendelea na mipango yake kuitandika Ukraine na kuweka kibaraka wake?

NATO watakubali kuona Ukraine walioishawishi iingie vitani na Russia ikichukuliwa na Russia huku wasifanye lolote?

NATO watakubali kudharaulika na kumponza kibaraka wao Zelensky ambae walimuahidi kuishinda Russia?

Kwa maana Russia ikiacha NATO kushinda hii vita ni kuiruhusu Ukraine kuingia kwenye muungano na NATO, na hili litatokea haraka sana, Je Russia itakubali NATO kukaa karibu na mipaka yake?

Maswali ni mengi. Na situation inaogofya. Tusubiri.
Hii habari yako ni ya kuunga unga sana. Unasema Ukraine kapoteza wakati unakumbuka Kyiv ilizungukwa na jeshi la Urusi ila sasa vita vipo mpakani. Askari wengi wa Ukraine wamefariki kama walivyofariki wa Urusi. Urusi ni kubwa kwa Ukraine na sio rahisi Ukraine kushinda. Njia ya vita kuisha ni askari wa Urusi kufariki kwa winging zaidi, ikijumuisha mamluki wa India, Nepal na nchi za Central Asia.
 
Back
Top Bottom