Yaani natumika sana na watu wanaokuwa na ukaribu na mimi wakihitaji msaada wa kifedha au kihisia
Kwa sasa naweza sema ukiacha ndugu zangu, watu wote waliobaki wana ji attach kwangu tuu wakiwa na shida. Kuna mmoja yakimkuta kwa siku utapokea simu zaidi ya kumi, kila mara, akishatatua shida yake anapotea.
Wengine pia ndio hivyo, mtu akiwa na shida ndo anakutafuta. Kuwaambia sina wanapoomba ndiyo siwezi
Hii circle ya watu wa aina hii niko nayo mimi tuu au hata nyinyi?
Wewe nakuita wewe!!!
Ndugu zako ni wanao uliozaa!hao ndio ukiugua Hadi kufa watakua pembeni mwa kitanda Hadi dakika ya mwisho!
Haio uliozaliwa nao watakujulia Hali Kwa simu tu!!
Achana na huo ujinga,Jenga familia Yako iwe taasisi Kwa kutengeneza vitega uchumi vya maana!
Saidia watoto waliotelekezwa au yatima au fukara kwenye ukoo Kwa kuwalea yaani daily routine hao ndio wataleta baraka nyumbani kwako!hai wakubwa wapambane na onyesha msimamo wako hapo!
Saidia sana Baba na mama wanakua na shida za maana kama mavazi,njaa na ugonjwa!
Wengine potezea,saidia watoto TU wengine ambao ni mafukara hio ndio sadaka na utakua ukumbusho kwao na Kwa Mungu !na Mungu atakupigania sana!!
Huo mtego utakurudisha nyuma Sana na maendeleo yako kifamilia na kama huna familia Hadi sasa upo kwenye crisis kubwa mno na ni msiba kwako!!!
Mimi ndugu zangu wananijua vema kama ni swala la hela za matumizi Huwa nawaambia "MAMA YETU HAKUZAA MLEMAVU HATA MMOJA ANAEHITAJI HELA YA KULA NA MTAJI KWA KUWA OMBAOMBA ,MTAJI NI VIUNGO ULIVYO NAVYO,PAMBANA!!!
Labda kwa wanafunzi kidogo najali Kwa buku Tano au 20,!!!
Usijifanye Mungu was kubeba misalaba ya watu,Mja ni WA Mungu amuombe yeye afungue njia na sio kuwa Mungu kwao!!