Lord Delamere in Kenya
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,988
- 8,021
Uliwahi kupita shuleni? Basi ufafanuzi wa swali lako uko hivi; YANGA ni sawa na mwanafunzi anayeongoza darasani kwenye mitihani ya ndani ya shule (mfano midterm, terminal na annual examinations) ila anafeli vibaya kwenye mitihani ya nje (mfano Mock na Necta Examinations). SIMBA yenyewe ni sawa na mwanafunzi mwenye ufaulu wa wastani kwenye mitihani ya ndani ya shule ila kwenye mitihani ya nje ya shule yuko 🔥 Ile mbaya kumzidi anayeongoza darasani kwao. Hapo nani mjanja?Wadau naomba Ufafanuzi kidogo juu ya hiyo kwanini YANGA ambao ndio Bingwa wa Ligi Kuu anacheza Shirikisho Kombe la Washindwa na SIMBA ambao Sio Bingwa wa Ligi anacheza KOMBE la MABINGWA kwani YANGA nini KILIWAPATA?
Naomba Majibu yasiwe ya HASIRA na CHUKI
Huyu mwanafunzi anayefaulu internal examinations pekee (YANGA) walakini sana. Ukimchunguza sana utagundua anafaulu sana mitihani ya ndani kwa sababu zifuatazo:
1.Huwa anaotea au anajua style ya utungaji mitihani wa Mwalimu wake hapo shuleni, akikutana na mitihani ya Walimu wa shule nyinginezo lazima achemke. Hapa namaanisha YANGA ameizoea ligi ya ndani na rhythm yake.
2.Mwanafunzi huyu inawezekana huwa anaiba paper au anaonyeshwa paper na Mwalimu wake, akikaziwa kwenye paper za Mock au Necta lazime ahesabu mabati. Hapa namaanisha YANGA huwa anapenyeza bahasha kwa waamuzi ili abebwe. Sasa kule CAFCL na hata CAFCC hakunaga mambo ya bahasha, ni uwezo wako ndo utakubeba.
Mwisho wa siku mwanafunzi huyu hufeli ila wenzake alikuwa anawapita darasani (Simba SC) husonga mbele kwenye levels nyingine za elimu na kumwacha akisema ''Mimi nilikuwa na akili kumzidi fulani (Simba), darasani alikuwa ananijua!". Ehee,halafu ikawaje?
Majibu mwengine wataongezea wadau.