Naungana na Rais Samia, ni kweli taifa lilitetereka kwa ubaguzi wa kiitikadi na kikabila kipindi cha nyuma

Naungana na Rais Samia, ni kweli taifa lilitetereka kwa ubaguzi wa kiitikadi na kikabila kipindi cha nyuma

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Rais Samia jana alisema hapo katikati tulitetereka kidogo tukaanza kubaguana kwa itikadi, ukanda na ukabila, hakutaja ni kipindi cha Magufuli, lakini wafuasi wengi wa Magufuli wakasema anamlenga Magufuli

Hili linaashiria kuwa ni kweli Magufuli alikuwa mbaguzi hadi ubaguzi unapokemewa tayari inaonekana Magufuli ndio kaguswa.

Na kama trukitaka kusonga mbele kama taifa lenye umoja na mshikamano ni lazima tuongee kwa uwazi matatizo yetu ili yasije kujitokeza tena, hata kama yamefanywa na kiongozi gani, lazima tuyasema hapa tulikosea na tunatakiwa kujirekebisha

Magufuli alisikika mara nyingi akisema kipindi cha Kikwete na Mkapa taifa hili lilikuwa likinyonywa sana na mafisadi, lengo ni kujua tulikosea wapi ili tujue tunarekebisha vipi, sikuona watu wakimlalamikia Magufuli kuwasema marais hawa wastaafu

Magufuli alisikika mara nyingi tu akisema hawezi kutatua shida za wananchi maeneo ambayo wamechagua upinzani, alisikika pia mara nyingi akiwatishia wananchi waziwazi wakichagua diwani ama mbunge wa upinzani basi serikali yake haitotatua shida zao kabisa..hizi sio kauli za kiungwana na zinafaa kukemewa kama tunataka kujenga taifa pasipo unafiki

Magufuli pia alisikika akiwaambia Tanroads wasiwabomolee watu wa Mwanza kwa kuwa walimpa kura nyingi huku bomoa bomoa ikiwa imefanyika kwa wakazi wa Kimara Dar huku kukiwa na zuio la mahakama, hii haikuwa uungwana hata kidogo kufanywa na kiongozi wa nchi na inafaa ikemewe

Rais pia alisikika akitoa hotuba kwa kilugha cha kwao mara nyingi wakati wa kampeni za uchaguzi hata wakati wa hotuba za kawaida, hii haikuleta picha nzuri, na kama tunataka kujenga taifa lisilo na wanafiki yafaa kukemea mambo haya

Namuunga mkono Rais Samia, amekuwa akirekebisha mabaya ya Magufuli na kuendeleza yale mazuri, na asiogope kusema kuwa sehemu fulani tul;ikosea kwani uwazi na nuaminifu ndio hujenga taifa imara
 
Tupate Katiba Mpya sasa, anaweza kufanya mazuri sana akaja mwingine akavuruga yote kwa sababu ya udhaifu wa katiba.
 
Chadema tangu iundwe inatetereka, makao makuu wamejaa wachaga mpaka madereva, makao makuu ni kama klabu ya mbege kibosho umbwe
 
Chadema tangu iundwe inatetereka, makao makuu wamejaa wachaga mpaka madereva, makao makuu ni kama klabu ya mbege kibosho umbwe
Samia alikua akiizungumzia Chadema?
Mtajificha hadi lini kwenye udhaifu wa Chadema?
 
Rais Samia jana alisema hapo katikati tulitetereka kidogo tukaanza kubaguana kwa itikadi, ukanda na ukabila, hakutaja ni kipindi cha Magufuli, lakini wafuasi wengi wa Magufuli wakasema anamlenga Magufuli
Hili linaashiria kuwa ni kweli Magufuli alikuwa mbaguzi hadi ubaguzi unapokemewa tayari inaonekana Magufuli ndio kaguswa.

Na kama trukitaka kusonga mbele kama taifa lenye umoja na mshikamano ni lazima tuongee kwa uwazi matatizo yetu ili yasije kujitokeza tena, hata kama yamefanywa na kiongozi gani, lazima tuyasema hapa tulikosea na tunatakiwa kujirekebisha

Magufuli alisikika mara nyingi akisema kipindi cha Kikwete na Mkapa taifa hili lilikuwa likinyonywa sana na mafisadi, lengo ni kujua tulikosea wapi ili tujue tunarekebisha vipi, sikuona watu wakimlalamikia Magufuli kuwasema marais hawa wastaafu

Magufuli alisikika mara nyingi tu akisema hawezi kutatua shida za wananchi maeneo ambayo wamechagua upinzani, alisikika pia mara nyingi akiwatishia wananchi waziwazi wakichagua diwani ama mbunge wa upinzani basi serikali yake haitotatua shida zao kabisa..hizi sio kauli za kiungwana na zinafaa kukemewa kama tunataka kujenga taifa pasipo unafiki
Magufuli pia alisikika akiwaambia Tanroads wasiwabomolee watu wa Mwanza kwa kuwa walimpa kura nyingi huku bomoa bomoa ikiwa imefanyika kwa wakazi wa Kimara Dar huku kukiwa na zuio la mahakama, hii haikuwa uungwana hata kidogo kufanywa na kiongozi wa nchi na inafaa ikemewe
Rais pia alisikika akitoa hotuba kwa kilugha cha kwao mara nyingi wakati wa kampeni za uchaguzi hata wakati wa hotuba za kawaida, hii haikuleta picha nzuri, na kama tunataka kujenga taifa lisilo na wanafiki yafaa kukemea mambo haya

Namuunga mkono Rais Samia, amekuwa akirekebisha mabaya ya Magufuli na kuendeleza yale mazuri, na asiogope kusema kuwa sehemu fulani tul;ikosea kwani uwazi na nuaminifu ndio hujenga taifa imara
Sawa
 
Wakuu wa nchi za EAC wakikuwepo hapo Kenya juzi wakizungumzia 'intergration' hii mada ingewakilishwa hapo.
 
Back
Top Bottom