Nawakumbusha tu: Miaka hiyo tuliimba tu kama kujifurahisha wala hatukujua maana yake

Nawakumbusha tu: Miaka hiyo tuliimba tu kama kujifurahisha wala hatukujua maana yake

Ila huyu Mzee alikuwa jau sana,ukiangalia ubeti wa nne Mzee anajinadi anakufa maskini Hana Mali,Sasa Kwa Nini enzi za Uhai wake hakuenda huko shambani kulima Ili apate mali[emoji1751]?
Kuna mawili nayaona kwa huyu mzee
1.eidha alijua mapema kuwa mali ipo shambani lkn yy akapotezea akajikita kutafuta rupia za mjerumani namambo mengine kama hayo mpaka mauti unamkaribia akaona awaase wanae kua mali ipo shambani wasije wakapoteza muda tena kama yy.
2 .safari atokayo ndio iliyomfumbua macho kuwa kulimo kinalipa, sema ndo ivo too late akaona sio mbaya akiwasanua vijana wake
 
Sadiki na Chitemo walifanyaje,?labda ni story tofauti
Mmoja alikuwa mvivu mwingine mchapa kazi.. chitemo aliamua kutoroka baada ya kuona kama ananyanyaswa kwenda kwenye gari akashushwa kwa sababu hana nauli hapo ndo akaanza kuimba hilo shairi

Sijajua kama mwanzo ilikuwa Ni sikiri na sadiki ila version ambayo nimekutana nayo ni hiyo ya juu
 
Inawezekana upo sahihi, kwani baadaye, vitabu vikawa vinatumika tofauti, kati ya shule na shule, tofauti na huko nyuma, ambako, Nchi nzima, shule zote zilikuwa zinatumia vitabu vya aina moja!
Yeap na hii kiasi fulani imeathiri sana elimu. Vitabu vilivyokuwa vinachapwa na TIE vilikuwa na quality content ukilinganisha na vile vya macmillan . Sasa sijui chenga ilitokea wapi.
 
Mmoja alikuwa mvivu mwingine mchapa kazi.. chitemo aliamua kutoroka baada ya kuona kama ananyanyaswa kwenda kwenye gari akashushwa kwa sababu hana nauli hapo ndo akaanza kuimba hilo shairi

Sijajua kama mwanzo ilikuwa Ni sikiri na sadiki ila version ambayo nimekutana nayo ni hiyo ya juu
hata mimi ndio ivyo hivyo . Kisa cha sadiki na chitemo
 
Yeap na hii kiasi fulani imeathiri sana elimu. Vitabu vilivyokuwa vinachapwa na TIE vilikuwa na quality content ukilinganisha na vile vya macmillan . Sasa sijui chenga ilitokea wapi.
Iliingia biashara! Watu wengi wakawa wanatoa vitabu, na kufanya biashara na shule moja moja. Ikawa, watoaji wanatoa rushwa kwa mwalimu mkuu, basi unapewa tenda.
 
Sikiri mi maskini,uvivu wangu nyumbani,
Nikiwa hapa njiani nakufa hapa Kwa Nini?
Sadiki Sasa ashiba,chakula kingi Kwa baba
Nikiwa hapa njiani nakufa hapa Kwa Nini?
Ni chitemo siyo sikiri.....
Ama vitabu ni tofauti?
 
Iliingia biashara! Watu wengi wakawa wanatoa vitabu, na kufanya biashara na shule moja moja. Ikawa, watoaji wanatoa rushwa kwa mwalimu mkuu, basi unapewa tenda.
Upo sahihi nadhani kama nakumbuka vizuri nikiwa chalii mdogo sana ilianza kushamiri miaka kuanzia 2004 , 2005 na 2006. Maana ndio vitabu vya logo ya BEN, Pamoja na macmillan aidan vinaanza huku vikiwa na picha. Michoro na vielelezo vya colored na sio vile vya black n white
 
Hadithi ya juma na uredi

I missed those days[emoji1][emoji1][emoji1]
 
Umetisha sana.Haya mashairi yataishi miaka yote.
 
View attachment 2769079
NAWAKUMBUSHA TU
1. Karudi baba mmoja,
toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja,
na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja,
ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli iwafae maishani.

2. Akatamka mgonjwa,
ninaumwa kwelikweli,
Hata kama nikichanjwa,
haitoki homa kali,
Roho naona yachinjwa,
kifo kimenikabili,
Semeni niseme nini,
kiwafae maishani.

3. Yakawatoka kinywani,
maneno yenye akili,
Baba yetu wa thamani,
sisi tunataka mali,
Urithi tunatamani,
mali yetu ya halali,
Sema iko wapi mali,
itufae maishani

4. Baba aliye kufani,
akajibu lile swali,
Ninakufa maskini,
baba yenu sina hali,
Neno moja lishikeni,
kama mnataka mali,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

5. Wakazidi kumchimba,
baba mwenye homa kali,
Baba yetu watufumba,
hatujui fumbo hili,
akili zetu nyembamba,
hazijajua methali,
Kama tunataka mali,
tutapataje shambani?

6. Kwanza shirikianeni,
nawapa hiyo kauli,
Fanyeni kazi shambani,
mwisho mtapata mali,
haya sasa buriani,
kifo kimeniwasili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

7. Alipokwisha kutaja,
fumbo hili la akili,
Mauti nayo yakaja,
roho ikaacha mwili,
Na watoto kwa umoja,
wakakumbuka kauli,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

8. Fumbo wakatafakari,
watoto wale wawili,
wakakata na shauri,
baada ya siku mbili,
wote wakawa tayari,
pori nene kukabili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

9. Wakazipanda shambani,
mbegu nyingi mbalimbali,
tangu zile za mibuni,
hadi zitupazo wali,
na mvua ikaja chini,
wakaona na dalili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

10. Shamba wakapalilia,
bila kupata ajali,
Mavuno yakawajia,
wakafaidi ugali,
Wote wakashangilia,
wakakumbuka kauli,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

11. Wakanunua na ng'ombe,
majike kwa mafahali,
wakapata na vikombe,
mashine na baiskeli,
Hawakuitaka pombe,
sababu pombe si mali,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.

2. Wakaongeza mazao,
na nyumba za matofali,
Pale penye shamba lao,
wakaihubiri mali,
Wakakiweka kibao,
wakaandika kauli...

"KAMA MNATAKA MALI
MTAIPATA SHAMBANI"
.
[emoji124]
[emoji124]
[emoji124]
[emoji124]
[emoji124]
[emoji124]

Miaka hiyo tuliimba tu kama kujifurahisha wala hatukujua maana yake, leo twatambua nini maana yake
Nawakumbusha tu
[emoji1493]
Miaka hiyo tuliimba tu kama kujifurahisha wala hatukujua maana yake, leo twatambua nini maana yake[emoji419][emoji375]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna lile shaili la silitaki mbichi hizi,nalo ni[emoji91]
 
Back in those days, when education was education
Mmmh Kwa hiyo Elimu ya siku hizi sio elimu!watoto wa darasa la tatu siku hizi wanasoma reproduction we ulisoma form three😁😁
 
Huu ndio ulipuaji Sasa kwa kivuli Cha competency based
90% Lasaba wa miaka yetu walikua smart kuliko form 4 wanaomaliza mwez ujao
Hamna lolote....Sie ndio wale tuliojua binadamu alikuwa nyani watoto wa siku hizi waulize uone uelewa wao,enzi hizo utasikia mtu wa form two hajui hata mtoto anazaliwaje eti kaokotwa sijui kanunuliwa uliza watoto wa siku hizi,hao watoto wasio smart ni hao wanaosoma shule zisizo na walimu, Serikali ipeleke walimu uone,darasa Moja watoto 158 mwalimu mmoja wataelewa Nini Sasa?
 
Hamna lolote....Sie ndio wale tuliojua binadamu alikuwa nyani watoto wa siku hizi waulize uone uelewa wao,enzi hizo utasikia mtu wa form two hajui hata mtoto anazaliwaje eti kaokotwa sijui kanunuliwa uliza watoto wa siku hizi,hao watoto wasio smart ni hao wanaosoma shule zisizo na walimu, Serikali ipeleke walimu uone,darasa Moja watoto 158 mwalimu mmoja wataelewa Nini Sasa?
Madam umeamua kuni-challange au upo serious

Level of content, coverage na scope of study was far better kuliko Hawa wa Sasa hivi

Level of performance ilikua sahihi na yakibabe. Ukifaulu umefaulu kweli
Sio Sasa hivi, siasa ipo mtu Kati kwenye ku-balance ili interest zao ziende sawa

Wanafunzi wa Sasa hivi wengi wao ni weupe Sana kichwani. Zaidi ya kujua matusi kwa marefu na mapana
 
Madam umeamua kuni-challange au upo serious

Level of content, coverage na scope of study was far better kuliko Hawa wa Sasa hivi

Level of performance ilikua sahihi na yakibabe. Ukifaulu umefaulu kweli
Sio Sasa hivi, siasa ipo mtu Kati kwenye ku-balance ili interest zao ziende sawa

Wanafunzi wa Sasa hivi wengi wao ni weupe Sana kichwani. Zaidi ya kujua matusi kwa marefu na mapana
Wala siku-challange!mwamko wa elimu zamani ulikuwa mdogo,hivyo number ya watoto ilibalance na mwalimu,siku hizi Elimu imepanuliwa,mitaala imeboreshwa,shule za kata zimejengwa kila Kona,wazazi wamehamasishwa wapeleke watoto shuleni Kwa wingi na wamefanya hivyo siku hizi hata kupata house dada ni kisanga,Cha ajabu walimu hamna...Sasa kusema elimu mbovu sio kweli sema tuna uhaba wa waelimishaji
 
Kuna mawili nayaona kwa huyu mzee
1.eidha alijua mapema kuwa mali ipo shambani lkn yy akapotezea akajikita kutafuta rupia za mjerumani namambo mengine kama hayo mpaka mauti unamkaribia akaona awaase wanae kua mali ipo shambani wasije wakapoteza muda tena kama yy.
2 .safari atokayo ndio iliyomfumbua macho kuwa kulimo kinalipa, sema ndo ivo too late akaona sio mbaya akiwasanua vijana wake
🤣🤣🤣🤣Kazururaaa wewe rupia zenyewe asipate akambulia kuvimba mapaja,,, akaona Bora angebaki zake shambani alime angepata mali
 
Back
Top Bottom