Nawatakia Wakenya wote uchaguzi mwema, wenye amani na wa haki

Nawatakia Wakenya wote uchaguzi mwema, wenye amani na wa haki

Nadhani issue isiwe kukataa kujifunza hata vitu vizuri kutoka kwa wengine.

Kama mpango huo wa kuwapima wagombea wetu vizuri na kuamua uwezo wao na dira zao, ni kitu kizuri sana cha kujifunza, na sioni aibu kusema kuwa ni vema KUIGA.

A wise man changes his mind sometimes, a fool never.

Kwa hili hata mimi sikatai hata kidogo. Achilia mbali nchi, binadamu kila kukicha tunajifunza na ndiyo njia ya kupambana na changamoto za kimaisha. Lakini vile vile, kama jamii, tuna miiko na taratibu na sheria zetu tulizojiwekea kama taifa.
Kitu ambacho kwangu ninakiona ni absurb, ni hii kasumba ya kuona kama sisi hakuna kitu ambacho tumesimama na wengine wanataka kuwa kama sisi. Ukiangalia comment za Watanzania wengi hapa, utagundua wako negative kwa kila kitu nchini kitu ambazo kiuhalisia siyo kweli hata kidogo.
ni kweli, kuna kitu tunaweza tukajifunza kutoka Kenya lakini siyo vyote na Wakenya nayo wana kitu wanaweza kujifunza kutoka kwetu.
Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini ulitanguliwa na mdahalo wa wagombea Urais, kutokufanyika mdahalo kwenye last election isiwe ndiyo nyongwa. Hili ni jambo la utaratibu wa kisiasa kati ya chama na chama.
 
Kwa hili hata mimi sikatai hata kidogo. Achilia mbali nchi, binadamu kila kukicha tunajifunza na ndiyo njia ya kupambana na changamoto za kimaisha. Lakini vile vile, kama jamii, tuna miiko na taratibu na sheria zetu tulizojiwekea kama taifa.
Kitu ambacho kwangu ninakiona ni absurb, ni hii kasumba ya kuona kama sisi hakuna kitu ambacho tumesimama na wengine wanataka kuwa kama sisi. Ukiangalia comment za Watanzania wengi hapa, utagundua wako negative kwa kila kitu nchini kitu ambazo kiuhalisia siyo kweli hata kidogo.
ni kweli, kuna kitu tunaweza tukajifunza kutoka Kenya lakini siyo vyote na Wakenya nayo wana kitu wanaweza kujifunza kutoka kwetu.
Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini ulitanguliwa na mdahalo wa wagombea Urais, kutokufanyika mdahalo kwenye last election isiwe ndiyo nyongwa. Hili ni jambo la utaratibu wa kisiasa kati ya chama na chama.
Sioni shida na ukosoaji endapo ukosoaji huo umejikita katika UKWELI.

Ukipenda sana kupigiwa makofi tuu, wakati fulani utapigiwa makofi na wapumbavu au utapigiwa makofi ya kejeli. Halafu mambo yanaendelea kuharibika.
 
Dodoki hufyonza lakini hutakatisha likakupa muonekano mzuri. Linaweza likakung'arisha ukapendeza ama likakuchubua, lakini mwisho wa siku litakuwa limekutakatisha!!!!!!
Kwa hiyo una maana tunapofyonza uchafu wote wa kidunia unaokuja mbele yetu tunafanya hivyo ili tumtakatishe nani?. Hatuwezi kuishi kama dodoki, ni muhimu kuchambua na kuchukua yale ambayo yanatufaa katika jamii yetu kulingana na utamaduni, taratibu na sheria tulizojiwekea katika jamii.
 
Sioni shida na ukosoaji endapo ukosoaji huo umejikita katika UKWELI.

Ukipenda sana kupigiwa makofi tuu, wakati fulani utapigiwa makofi na wapumbavu au utapigiwa makofi ya kejeli. Halafu mambo yanaendelea kuharibika.

Yes, kama ukosoaji umejikita katika ukweli basi hata huyo anayepinga atakuwa ni mjinga. Kinachotokea kwa sasa katika jamii ya kitanzania, ukosoaji mwingi unakuwa wa kinafiki na mara nyingi unachagizwa na fikra kinzani za kiitikadi zaidi au kufunga goli la kisiasa.
 
Kwani kukopa ni dhambi?. Kwa taarifa yako, hata USA ina madeni kibao na bado inakopa pesa kutoka CHINA. Open your eyes.

Nilijibu post yako kwa maana ya neno uliotumia. yaani jiwe la pembeni. kwa msingi ipi TZ ikawa jiwe la pembeni.
 
Acha kusifu vitu usivyovielewa, Wakenya wana kesi ya kujibu huko Mahakama ya kimataifa ya Hague, na hao hao wahandishi wa Habari wa Kenya unaowasifu ndio walio sababisha watu zaidi ya 1000 kuchinjwa live kama wanyama, sasa hata kama wahandishi wetu hawako kama wa CNN lkn hawachochei watu kuchinjana na wala hawana kesi za mauaji!
Are you a graduate? I would like to know before I comment anything on your thread...!!!!
 
Yes, kama ukosoaji umejikita katika ukweli basi hata huyo anayepinga atakuwa ni mjinga. Kinachotokea kwa sasa katika jamii ya kitanzania, ukosoaji mwingi unakuwa wa kinafiki na mara nyingi unachagizwa na fikra kinzani za kiitikadi zaidi au kufunga goli la kisiasa.
Mie naona mengi yanayokosolewa yamejikita katika ukweli. Na ninaona pia WATAWALA hawapendi mawazo mbadala hata yenye maslahi kwa umma.

Labda wewe utuoneshe lipi linalopingwa ambalo linapingwa kiitikadi tu na kupinga huko hakuzingatii ukweli wala maslahi ya nchi.
 
Vyombo vya habari Kenya siyo vya kuviamini sana na wakati mwingine hujisahau maana kama nukuu hapo juu waandaaji wa Mdahalo walikuwa hao hao vyombo vya habari lakini walitaka kutowapa nafasi wagombea 'wadogo' kama Mwanasheria Paul Muite na Mwalimu Abduba Diba mpaka jamaa wakaenda kortini kudai haki yao kikatiba kuweza kushirikishwa katika mdahalo wa wagombea urais Kenya.

Hivyo katiba katika makaratasi na wino inaweza kuonekana nzuri lakini katika utekelezaji huwa inapindishwa na kuwabagua baadhi wa wananchi wa Kenya na ni hivyo katika nchi zingine za barani Afrika.

Lugha fasaha ya Kiingereza inawapiga chenga wapiga kura walio wengi Kenya lakini vyombo vya media ya Kenya vinarusha matangazo ya kampeni, midahalo na uchambuzi kwa lugha ya Kiingereza badala ya Kiswahili na huu si mfano wa kuigwa au kupongezwa.

Masuala mzito kwa mwananchi wa kawaida wa Kenya kama ardhi, elimu, afya, ajira inakuwa vipi yachambuliwe au kuahidiwa kwa wananchi waKenya kupitia vyombo vya media kwa lugha ya Kiingereza bila kutilia maanani kuwa wasikilizaji au watazamaji wa televisheni ufahasa wa lugha ya Kiingereza hawana! Hii ni sawa na sera za mkoloni wa Kiingereza ambaye alikuwa na sheria kuwa ukiwa na elimu ndogo basi waachie walio na elimu kupiga kura na kukuamulia mustakabali wa maisha yako kisiasa.

Tukitumia mfano , mdahalo wa uraisi Kenya hauna lolote la ziada zaidi ya Tanzania au nchi yoyote ya kiafrika katika kufuata katiba nzuri iliyo katika makaratasi kwa vitendo iwe kwa vyombo vya media, tume za uchaguzi, vyombo vya dola vya usalama na ulinzi n.k ambavyo ama kwa kufahamu au mazowea au kuburuzwa au kushurutishwa hupendelea baadhi ya watu walio na 'uwezo' katika jamii.

Mfano mwingine Vyama vya siasa vya msimu Kenya/miungano ya chap-chap Jubilee au CORD au Ukabila havichambuliwi kwa kina na media ya Kenya. Vyama vya siasa Tanzania siyo vya msimu CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI, MAGAMBA a.k.a CCM n.k vyote vimedumu miaka ishirini (20) na zaidi, ''ukabila'' na 'udini'' unachambuliwa kwa kina na media za Tanzania na mitandao ya kijamii kutukumbusha athari- hasi (negative impact) katika juhudi zetu za kuujenga utaifa wa Mtanzania.

KASS- FM Kenya inamilikiwa na Wakalejin na K24TV ni ya GEMA association wakati Tanzania vituo vya media vya kikabila vinapigwa kwa majadiliano chanya katika media na mitandao ya jamii Tanzania ili kuzuia kuwepo vituo vya media vyenye muelekeo wa kikabila.
Kaka hebu read between the lines, Katiba hiyo hiyo imetenganisha mihimili 3 ya dola ndio maana walikwenda mahakamani ambako hakuna upendeleo hata kwa chama tawala ndiyo maana wakashinda na wakashiriki kwenye mdahalo huo!! Isitoshe lugha ya Kiingereza kwa Kenya inaongewa na wengi kama Kiswahili kinavyo ongewa Tanzania!! Kama ambavyo watanzania wengi hawaelewi mambo kwa lugha ya Kiingereza vivyo hivyo, wakenya wengi hawaelewi mambo mengi kwa lugha ya Kiswahili!! Wenzetu hawakuvuruga misingi ya Elimu na hususani lugha ya Kiingereza kama lugha ya kufundishia! Watanzania Just blame the first government for politicizing everything in this country such that we have nothing to be proud of! Badala ya somo la CIVICS mkapewa somo la ELIMU YA SIASA na nyote mmekuwa wanasiasa mnaopenda kuongea wakati hata utafiti hamna muda wa kufanya mnategemea maneno mengi na FITNA mkidhani mtafanikiwa... ANGALIENI mlipo sasa!! mnadhania kama nyie kiingereza hakipandi basi ni kwa wananchi wa nchi zote za East Africa kwa wale waliotawaliwa na waingereza!!
 
TBC tunajua ni TBCCM
sijui magamba wakianguka 2015 itakuwa inasifia upande gani.
wanaonekana wazi hawasomi habari za vyama vingine au kuwapa kipaumbele vyama vingine
huku wakitumia kodi zetu. TIDO alijitahidi kubalance lakini tuliona mwisho wake.

Ndiyo maana ya kampeni, kwani TBC huwa ni aje?
 
Mie naona mengi yanayokosolewa yamejikita katika ukweli. Na ninaona pia WATAWALA hawapendi mawazo mbadala hata yenye maslahi kwa umma.

Labda wewe utuoneshe lipi linalopingwa ambalo linapingwa kiitikadi tu na kupinga huko hakuzingatii ukweli wala maslahi ya nchi.
Kwenye swala la siasa jinsi zinavyoendeshwa Kenya ukilinganisha na Tanzania. Inashangaza kusikia wengi hapa wanasema siasa za Kenya ni better ukilinganisha na za kwetu. Ukiangalia kampeni zao za ubunge, governors na senetor hazina ustaraabu na zimejaa ukabila wa hali ya juu.
Kwenye matangazo pamoja na kwamba katika tekinologi wao wako mbele yetu, TV nyingi ziko mikononi mwa wagombea kwa hiyo bias zipo nyingi tu. Kuna mengi tu ambayo tunafikiri kama ni bora kuliko ya kwetu wakati sivyo pamoja na kwamba mwaka huu wameingia kwenye kampeni kwa kutumia Katiba ya nchi mpya.
 
Vyombo vya habari Kenya siyo vya kuviamini sana na wakati mwingine hujisahau maana kama nukuu hapo juu waandaaji wa Mdahalo walikuwa hao hao vyombo vya habari lakini walitaka kutowapa nafasi wagombea 'wadogo' kama Mwanasheria Paul Muite na Mwalimu Abduba Diba mpaka jamaa wakaenda kortini kudai haki yao kikatiba kuweza kushirikishwa katika mdahalo wa wagombea urais Kenya.

Hivyo katiba katika makaratasi na wino inaweza kuonekana nzuri lakini katika utekelezaji huwa inapindishwa na kuwabagua baadhi wa wananchi wa Kenya na ni hivyo katika nchi zingine za barani Afrika.

Lugha fasaha ya Kiingereza inawapiga chenga wapiga kura walio wengi Kenya lakini vyombo vya media ya Kenya vinarusha matangazo ya kampeni, midahalo na uchambuzi kwa lugha ya Kiingereza badala ya Kiswahili na huu si mfano wa kuigwa au kupongezwa.

Masuala mzito kwa mwananchi wa kawaida wa Kenya kama ardhi, elimu, afya, ajira inakuwa vipi yachambuliwe au kuahidiwa kwa wananchi waKenya kupitia vyombo vya media kwa lugha ya Kiingereza bila kutilia maanani kuwa wasikilizaji au watazamaji wa televisheni ufahasa wa lugha ya Kiingereza hawana! Hii ni sawa na sera za mkoloni wa Kiingereza ambaye alikuwa na sheria kuwa ukiwa na elimu ndogo basi waachie walio na elimu kupiga kura na kukuamulia mustakabali wa maisha yako kisiasa.

Tukitumia mfano , mdahalo wa uraisi Kenya hauna lolote la ziada zaidi ya Tanzania au nchi yoyote ya kiafrika katika kufuata katiba nzuri iliyo katika makaratasi kwa vitendo iwe kwa vyombo vya media, tume za uchaguzi, vyombo vya dola vya usalama na ulinzi n.k ambavyo ama kwa kufahamu au mazowea au kuburuzwa au kushurutishwa hupendelea baadhi ya watu walio na 'uwezo' katika jamii.

Mfano mwingine Vyama vya siasa vya msimu Kenya/miungano ya chap-chap Jubilee au CORD au Ukabilahavichambuliwi kwa kina na media ya Kenya. Vyama vya siasa Tanzania siyo vya msimu CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI, MAGAMBA a.k.a CCM n.k vyote vimedumu miaka ishirini (20) na zaidi, ''ukabila'' na 'udini'' unachambuliwa kwa kina na media za Tanzania na mitandao ya kijamii kutukumbusha athari- hasi (negative impact) katika juhudi zetu za kuujenga utaifa wa Mtanzania.

KASS- FM Kenya inamilikiwa na Wakalejin na K24TV ni ya GEMA association wakati Tanzania vituo vya media vya kikabila vinapigwa kwa majadiliano chanya katika media na mitandao ya jamii Tanzania ili kuzuia kuwepo vituo vya media vyenye muelekeo wa kikabila.

Post zako nyingi huwa biased licha ya kuwa unaweza kuwa na hoja mwafaka. KASS- FM ni moja ya stesheni za royal media ambayo ina zingine zaidi ya kumi zinazotangaza kwa lugha tofauti. Mijadala iliopita yalikosa kuangazia kwa kina hoja za uchumi elimu, uchimbaji na utengenazaji nishati nk. Midahalo yalipangiwa kumvamia mtu moja kwa misingi ya ICC na ardhi na hazikutaka kujadili mambo ya msingi.

Pia Odinga alipoulizwa mbinu atakayotumia kuboresha matumizi za fedha na uchumi kwa ujumla, alisema atapunguza matumizi ya fedha/government expenditure. Mara nyingi maendeleo na miradi nyingi kenya huwezeshwa kwa kutumia fedha. badala aeleze njia mbadala ya kupata pesa za kutimiza miradi ya maendeleo, alikwama kwa kupunguza matumizi ya fedha. Mara nyingi wanaotafuta kiti hukosa weledi wa mambo wanayotarajia kutekeleza.

kueleza wtz katiba mpya ya kenya haina faida, ni uongo mtupu. vyombo vya habari kenya havijavamiwa kama vya TZ na zina huru wa kupeperusha habari. halafu kwasababu wewe ni mbumbumbu wa mwanasiasa unafikili watu ni vipofu kama wewe. Huenda huna familia unaoshughulikia ndiposa unasifia uongozi mbovu ulioko tanzania katika kundi la upinzani. Sera mbovu serikalini huaribu utekelezaji wa kazi. Baadhi ya waTZ kama wewe hawapendi mageuzi ya katiba bora ili vyombo vya habari vizid kupeperushe habari kwa kuwekewa vikwazo na wafisadi serikalini. Kwako imesalia majigambo kuwa Tz ina amani na uweledi katika lugha ya kiswahili. Sasa hivi idadi ya vyombo vya habari imeongezeka nchini ukilinganisha na hapo awali.

Ni rahisi kwa mwanasiasa anayepoteza umaarufu kuburuza vyombo vya habari, afisi za serikali, vyombo vya usalama, tume za uchaguzi nk katika tetesi kuleta sokomoko nchini na kwingineko ikiwa njia au mbinu mpya ya kisiasa amabayo wanasiasa wanatumia kujiuza kisiasa. Shirika na tume hizi nyingi zimeteuliwa na kamati na sio watu binafsi. Ikiwa mtu yeyote ana hofu anatakiwa kutumia mahakama kutatua utata.

Kuisifu tu lugha ya kiswahili haitoshelezi, ujue ni dhahiri watu wenye asili za kigeni huelewa kingereza. Kwa sababu mkoloni anatumia kingereza kama lugha ya asili haileti picha wanaozungumza kingereza wanamtukuza mwingereza. Nyie pia mna mengi mumekopa na kuchukua kutoka kwa mzungu hasa kwenye taaluma za kingereza sayansi sheria, nk amabo zimefanywa kutafsiriwa na sio uvumbuzi wa akili ya mwafrika. na kuiga kwenu taaluma hizi hamaanishi munatukuza muingereza!

Vyama za kenya ni vya msimu na ndio maana tunajivunia mengi kwa sasa kama kuibuni demokrasia katika anga za siasa za kenya. pengine vyama vya kutenda kazi kwa midomo CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI, MAGAMBA a.k.a CCM vikiondolewa, wtz watapata mabadiliko na maendeleo na sio kuenea kwa kazi za midomo bila vitendo ambao humnyima mwananchi nafasi ya maendeleo.
 
Kwenye swala la siasa jinsi zinavyoendeshwa Kenya ukilinganisha na Tanzania. Inashangaza kusikia wengi hapa wanasema siasa za Kenya ni better ukilinganisha na za kwetu. Ukiangalia kampeni zao za ubunge, governors na senetor hazina ustaraabu na zimejaa ukabila wa hali ya juu.
Kwenye matangazo pamoja na kwamba katika tekinologi wao wako mbele yetu, TV nyingi ziko mikononi mwa wagombea kwa hiyo bias zipo nyingi tu. Kuna mengi tu ambayo tunafikiri kama ni bora kuliko ya kwetu wakati sivyo pamoja na kwamba mwaka huu wameingia kwenye kampeni kwa kutumia Katiba ya nchi mpya.
Mimi naona wewe ndiwe uko negative. Watu wanapotazama mifano ya wengine wanatafuta mazuri ya kuiga, yasiyo mazuri wanawaachia wenyewe.

Bado na wewe una nafasi ya kuanzisha thread za kusifia hayo mema unayoyasema, ambayo nayaona kama yameanza kuwa mema ya kihistoria. Mfano: kampeni za kina Nape, haziachi kutaja Uchaga katika Chadema, na mbaya zaidi wameanza kutumia udini pia. Sasa utasifia nini hapo? Siasa za kujipigia debe kwa udini na ukabila tayari zimo humu Tanzania.

Naona bado tuna mema tunayoweza kujifunza, mabaya yao tutawaachia wao. Debates walizofanya ni jambo zuri kubwa sana la kujifunza na ikiwezekana kuiga.
 
I am very confident that this election will be very different and that we will all learn lessons from our Kenyan Brothers. Yesterday when supporters of Uhuru and Raila met, they hugged and chanted peace and nationalist slogans as a sign of peace. THEY HUGGED!!!
Even in countries where there has never been post electoral violence, I have never heard of supporters hugging. This is a very good "omen" and I believe that the election will be peaceful. Even if we have some discomfort at the second run, it will not be "post electoral conflict. All my expatriate friends in Kenya did not leave, they are confident that Kenyan's will agreeably surprise all skeptical and defeat predator journalist who thrive for sensational reports.
 
Ndugu wanaJF! Wengi tunaelewa kwamba jirani zetu na marafiki zetu wa Jamhuri ya Kenya wanelekea kufanya uchaguzi wao kesho tarehe 3.3.2013. Tunajua jinsi chaguzi nyingi hasa za Afrika hufuatiwa na vurugu kubwa ambazo husababisa upotevu wa mali na maisha. Nawaomba wanaJF wote, tuungane kwa pamoja kuwaombea hawa ndugu zetu wawe na uchaguzi mwema hapo kesho. Amani ya Kenya ni Amani ya Tanzania, Rwanda, Uganda, DRC na Afrika kwa ujumla. Kila la kheri kwa wagombeaji wote katika uchaguzi wa Kenya. Kila la kheri wapiga kura wote katika uchaguzi wa Kenya. Kila la kheri kwa Wakenya Wote. Harambeeeee! Nyayooo!

Nyayo mbona alishatoka madarakani!
 
Kwa kupitia mtandao huu wa JF, rafiki yangu Ab-Titchaz , ningependa kukutakia uchaguzi mwema, wa haki, na wa amani.

Tukiwa Tz tunatazama jinsi mtakavyo tetea demokrasia na kukubali matokeo.
Kwa kawaida yale yanayotokea katika nchi hizi zetu za Afrika Mashariki kwa njia moja au nyingine sisi wote tunahusika na matokeo yake.

Kwa dhati kabisa Mwenyezi Mungu awe nanyi.
 
page.jpg
Machi 4,2013
 
Let peace prevail


8525095951_286364245e_b.jpg



Kenya: Kenyans today troop in their millions to voting stations to elect leaders of their choice.

This is a pivotal General Election. It is the first under the new constitution and the first since the country almost disintegrated after the disputed election of 2007.

However, we must see things in perspective. This is not Kenya's first national vote, it is the tenth since Independence in 1963. There will be many more in future so long as we recognise that the country is more important than a single instance of balloting.

In one sense this is not a do-or-die affair, but a periodic event where Kenyans exercise their democratic right to choose their own leaders. But given the events of 2007, the elections are the last opportunity for us as a country to get our politics right. If we bungle today's election or go back to killing each other, not only will the world give up on us as a civilised nation but Kenyans too could lose faith in their own country.

Every Kenyan with a vote must go out and cast it. But after the voting, the law requires that you resume your normal activities until the next election. You must not remain at the polling station nor join agitating groups creating tension in the country.

Whatever the outcome of this election, normal life continues for the Kenyan family.

The world will not stop because of the electoral outcome, and that applies to voters as much as to the candidates. Ultimately, the fate of this country depends on the conduct of the politicians running in this election and the efficiency of the electoral authorities. It has been said many times before but it bears repeating: the losers must accept defeat with grace. There is no dignity in being a sore loser and it poses a grave danger to 40 million Kenyans.

As to the winner, you must not behave as if you have been granted a title to Kenya. Be magnanimous in victory. You and your supporters must respect those whom you have defeated.

You have a duty of national healing to reach out to your rivals and behave like the President of everyone, not just your supporters. Revenge and political score settling are primitive and unworthy. Excluding supporters of your rivals from the political mainstream is destructive and divides the country even more. This moment calls for statesmanship.

The Kenyan nation has invested heavily in reforming its institutions, such as the police, the Judiciary and the Independent Electoral and Boundaries Commission. These institutions must be allowed to do their job. Have faith in them.

Any calls for street protests that could lead to violence must be completely rejected. The Kenyan people must not allow themselves to be defined by one bungled election. We can and must move on.

Prove them wrong

When the winner is finally declared by the chairman of the IEBC, all political camps and institutions of government must obey the law and the transition mechanisms. Your constitutional duty is not to facilitate the assumption of power of your preferred person but to obey the will of the people.

With the new order, the ignominy of a departing president being booed and pelted with mud must never be repeated. The nightmarish scenes of Kenyans tearing down the pillars of their economy must be consigned to the dustbins of history.

Images of brother turning on brother are best deleted from the collective memory.


Here is our opportunity to shame the skeptics, naysayers and doomsday theorists. We must prove wrong those who are addicted to the image of Africa as a continent of bloodshed and suffering, such as the makers of the CNN story showing militia preparing for war in the Rift Valley.

As a nation we must show that we learnt our lesson from 2007.

It is a chance to demonstrate that we have come of age and are fully prepared to take our rightful place among the community of safe and secure democracies.

The last time we descended into anarchy and bloodshed, more than 1,000 Kenyans were butchered and 600,000 evicted from their homes. Our country was the scene of the most shocking atrocities, such as the burning of people inside a church and buildings. Even today, there are Kenyans who are refugees in their own country. In that season of madness, the economy lost at least Sh25 billion.

The future of this beloved country is today in our hands once again. By all going out to vote, respecting the outcome and ensuring law and order we will be united in sending out a firm message to the world: Never again.

Standard Digital News - Kenya : Opinion : Let peace prevail
 
Back
Top Bottom