Nawatakia wana JamiiForums wote heri ya mwaka mpya 2025

Nawatakia wana JamiiForums wote heri ya mwaka mpya 2025

Tate Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2019
Posts
33,092
Reaction score
96,127
Kwa heshima na taadhima, nichukue nafasi hii ya kipekee kuushukuru uongozi mzima wa jamii forums, wafanyakazi wake wote, na pia wana JamiiForums wenzangu kwa kuwa pamoja kwa mwaka wote huu wa 2024.

Natambua fika tumepitia mengi ndani ya mwaka wote huu. Wako ndugu na jamaa zetu wengi kwa namna moja au nyingine wameshindwa kuifikia hii siku ya leo. Lakini kwa upande wetu tunashukuru kufika salama pamoja na changamoto zetu mbalimbali za kiuchumi, kimaisha, kijamii, nk. zinazotukabili.

Lengo la huu uzi ndugu zangu, ni kutaka tu kuwatakia Wana jamii forums wote Heri ya Mwaka Mpya wa 2025! Natambua fika kuna baadhi yenu niliwakosea kwa namna moja au nyingine! Lakini pia kuna wachache wenu mlinikosea kwa kunikejeli, kunitukana, kuutweza utu wangu, nk. Binafsi napenda kusema nimewasamehe.
Hivyo na nyinyi nawashauri mfanye hivyo hivyo, ili maisha nayo yaendelee.

Mwisho kabisa napenda kuupongeza uongozi wa jamii forums kwa kufanikiwa kuufanya huu mtandao kuwa sauti ya wananchi walio wengi. Na uwepo wa viongozi waandamizi wa serikali, uwepo wa taasisi mbalimbali za serikali, nk. humu jukwaani, ni ushahidi tosha jamii forums ni chombo makini cha kupashana habari.

NB: Rai yangu ni kwa sisi wajumbe tuliomo humu jukwaani! Tujitahidi ndugu zangu kutoa maoni yetu kwa staha. Matusi, kejeli, nk. Ndiyo baadhi ya vitu vinavyoweza kutuweka matatani.

Lakini pia ninaomba ndugu zangu muwe mnanichukulia wakati fulani kutokana na ukweli kwamba mimi ni mtu ambaye huwa ninapenda kuchekesha kadamnasi, kuuliza maswali ya hapa na pale ya kufikirisha, nk. Therefore, don't take each and everything in a serious way, ok?

All in all, tukutane 👉 2025 panapo majaliwa. InshaAllah!
Wenu Tate Mkuu... Kutoka Lushoto Tanga.✍️
🙏
 
"so what are your plans for december 31?"
me:
FB_IMG_1735623774824.jpg
 
Kwa heshima na taadhima, nichukue nafasi hii ya kipekee kuushukuru uongozi mzima wa jamii forums, wafanyakazi wake wote, na pia wana JamiiForums wenzangu kwa kuwa pamoja kwa mwaka wote huu wa 2024.

Natambua fika tumepitia mengi ndani ya mwaka wote huu. Wako ndugu na jamaa zetu wengi kwa namna moja au nyingine wameshindwa kuifikia hii siku ya leo. Lakini kwa upande wetu tunashukuru kufika salama pamoja na changamoto zetu mbalimbali za kiuchumi, kimaisha, kijamii, nk. zinazotukabili.

Lengo la huu uzi ndugu zangu, ni kutaka tu kuwatakia Wana jamii forums wote Heri ya Mwaka Mpya wa 2025! Natambua fika kuna baadhi yenu niliwakosea kwa namna moja au nyingine! Lakini pia kuna wachache wenu mlinikosea kwa kunikejeli, kunitukana, kuutweza utu wangu, nk. Binafsi napenda kusema nimewasamehe.
Hivyo na nyinyi nawashauri mfanye hivyo hivyo, ili maisha nayo yaendelee.

Mwisho kabisa napenda kuupongeza uongozi wa jamii forums kwa kufanikiwa kuufanya huu mtandao kuwa sauti ya wananchi walio wengi. Na uwepo wa viongozi waandamizi wa serikali, uwepo wa taasisi mbalimbali za serikali, nk. humu jukwaani, ni ushahidi tosha jamii forums ni chombo makini cha kupashana habari.

NB: Rai yangu ni kwa sisi wajumbe tuliomo humu jukwaani! Tujitahidi ndugu zangu kutoa maoni yetu kwa staha. Matusi, kejeli, nk. Ndiyo baadhi ya vitu vinavyoweza kutuweka matatani.

Lakini pia ninaomba ndugu zangu muwe mnanichukulia wakati fulani kutokana na ukweli kwamba mimi ni mtu ambaye huwa ninapenda kuchekesha kadamnasi, kuuliza maswali ya hapa na pale ya kufikirisha, nk. Therefore, don't take each and everything in a serious way, ok?

All in all, tukutane 👉 2025 panapo majaliwa. InshaAllh!
Wenu Tate Mkuu...✍️
🙏
Na kwako pia mkuu❤❤❤📌💪🏿🔨.. Asante sana kwa upendo
 
Kwa heshima na taadhima, nichukue nafasi hii ya kipekee kuushukuru uongozi mzima wa jamii forums, wafanyakazi wake wote, na pia wana JamiiForums wenzangu kwa kuwa pamoja kwa mwaka wote huu wa 2024.

Natambua fika tumepitia mengi ndani ya mwaka wote huu. Wako ndugu na jamaa zetu wengi kwa namna moja au nyingine wameshindwa kuifikia hii siku ya leo. Lakini kwa upande wetu tunashukuru kufika salama pamoja na changamoto zetu mbalimbali za kiuchumi, kimaisha, kijamii, nk. zinazotukabili.

Lengo la huu uzi ndugu zangu, ni kutaka tu kuwatakia Wana jamii forums wote Heri ya Mwaka Mpya wa 2025! Natambua fika kuna baadhi yenu niliwakosea kwa namna moja au nyingine! Lakini pia kuna wachache wenu mlinikosea kwa kunikejeli, kunitukana, kuutweza utu wangu, nk. Binafsi napenda kusema nimewasamehe.
Hivyo na nyinyi nawashauri mfanye hivyo hivyo, ili maisha nayo yaendelee.

Mwisho kabisa napenda kuupongeza uongozi wa jamii forums kwa kufanikiwa kuufanya huu mtandao kuwa sauti ya wananchi walio wengi. Na uwepo wa viongozi waandamizi wa serikali, uwepo wa taasisi mbalimbali za serikali, nk. humu jukwaani, ni ushahidi tosha jamii forums ni chombo makini cha kupashana habari.

NB: Rai yangu ni kwa sisi wajumbe tuliomo humu jukwaani! Tujitahidi ndugu zangu kutoa maoni yetu kwa staha. Matusi, kejeli, nk. Ndiyo baadhi ya vitu vinavyoweza kutuweka matatani.

Lakini pia ninaomba ndugu zangu muwe mnanichukulia wakati fulani kutokana na ukweli kwamba mimi ni mtu ambaye huwa ninapenda kuchekesha kadamnasi, kuuliza maswali ya hapa na pale ya kufikirisha, nk. Therefore, don't take each and everything in a serious way, ok?

All in all, tukutane 👉 2025 panapo majaliwa. InshaAllah!
Wenu Tate Mkuu... Kutoka Lushoto Tanga.✍️
🙏
Bado hatujauona , tutajibu tukiuona. Siku ndefu
 
Mwaka mpya bado sana kuna watu watakufa masaa machache yajayo na hawataiona 2025. Tuendelee kuomba uzima tuvuke salama.
Uko sahihi. Ila kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, InshaAllah tutavuka salama.
 
insha'Allah Zumbe tutavuka salama, Leo naenda kuuza maji Kwenye mkesha wa Mwamposa, nayachanganya na Nyagi kidogo ili waumini wasije wakachoka sana
Dah!! Ukifanya hii kitu itasababisha mapepo kupiga makelele yasiyo kawaida wakati yanatolewa na Mtimishi wa Mungu Askofu, Nabii na Mtume Mwamposa!!
 
Back
Top Bottom