Naweza kujenga nyumba kwa TZS Milioni 20?

Naweza kujenga nyumba kwa TZS Milioni 20?

Milioni 20 ni vihela vidogo sana.
sijapenda unavyomkatisha mleta mada ,huyu yuko serious anataka kuachana na mambo ya kupanga wewe kweli unamwambia m 20 ndogo,mshauri kama huwezioita kimya kimya ,kujenga sio lelemama uanhitaji courage
 
Kama Mililioni 20, inajenga dar basi nimeibiwa nimelipa Millioni 24, (kijijini) kuezeka paa tu. Mabati vigae +misumari+mbao(treated) +usafiri 18,000,000; Fundi 4million+2M dharura!
 
Hiyo hela kwa mikoani inatosha kujengea nyumba na inaisha kabisaaa! Kwa nini mng'anganie kujenga Dar peke yake? Njoni muanzie kujenga huku mikoani, nyumba ikiisha inakaa miaka miwili unaiuza unapata hela ya kujenga Dar! Simple like that....

kweli mi siji kujenga dar hata iweje mkoani kwanguu ndo mwake
 
Mil 20/inajenga nyumba ya vyumba 4tena safi kabisa/ unaweza kujenga nyumba mbili za vyumba vitatu kila moja tena safi.../inaweza kujenga nyumba ta vyumba 3,sitting room,car park,geti, alluminium,gypsum full/nimejenga mimi millioni 20 kibongo/bongo kubwa sana mkuu mtu asikudanganye labda mwizi huyoo....lati piga simu hapa tuzungumzee/0657 8/ 0657 740 797............
Hii namba ipo hewani ....
 
Unaweza kabisa; usiogope kujenga kwanza chumba self contained, sehemu ya kupikia, na sebule ndogo - kitu kama a studio flat, huku ukiwa na ramani nzima ambayo utaimalizia taratibu hata ukishahamia humo. lakini siri kubwa ya mafanikio pia ni procurement - simamia kila kitu, kuanzia kufuata kokoto, mpaka kusimamia every step ya ujenzi unaondelea pale;that way uta save cost by half. Kama utasimamia kwa mtindo huu, with 20 million today in Dar, u can build a very nice house with two bedrooms, a bathroom, kitchen and living room.
1506047_297452313786780_9025331958679517089_n.jpg 10574490_282665781932100_2205280872664420402_n.jpg 10703766_281631872035491_4602026831465105371_n.jpg 10801673_289654201233258_8547384014846562766_n.jpg 63936_282600661938612_2856938812978802932_n.jpg 10523339_289654077899937_7253532882885130333_n.jpg 10712863_289024424629569_3094684470529304897_n.jpg
Wazo zuri sana Mchambuzi, mfano mtu akiwa na plan ya nyumba ambayo ramani na mjengo wake unaruhusu kuongeza na ikishakamilika sehemu iliyojengwa kabla haitaonekana kiraka kwa vile ujenzi umefuata ramani. Inafaa kwa utaratibu huu kuchagua mtindo wa ujenzi ambao ni rahisi kufanya extension baadaye kwa awamu.

Picha hapo juu ni mfano wa ramani na picha za nyumba ambazo huwa ni za gharama nafuu na zina nafasi pamoja na vyumba vya kutosha kifamilia pia rahisi kufanya extension siku nafasi itakapokuruhusu.

Ukishaanza kuishi kwenye sehemu ya nyumba unayokusudia rahisi kuimaliza kuliko kusubiria upate mtaji wa kujenga nyumba nzima hadi imalizike.
 
Mimi ningekuwa wewe wala nisingeanza kupanga mipango ya kujenga nyumba. Ningeanza biashara ya kusafirisha nguruwe kwa mchanganuo huu hapa chini
1. Nguruwe 150 wadogo @ 10,000
2.Chakula (mashudu) Tshs 5,000 kwa mwezi kwa nguruwe mmoja
3.Ujenzi wa mabanda Tshs 250,000
4.Mlinzi Tshs 20,000 kwa mwezi
5.Matibabu Tshs 30,000 kwa mwezi.

Nguruwe huchukua miezi 6-8 kwabla ya kuanza kuuzwa. Kwakweli ni biashara nzuri sana na ndani ya miaka miwili unaweza kuwa na hela chafu kiasi cha kugombewa na mademu kama mpira wa kona.

Nguruwe gani wanauzwa elfu kumi
 
kwa kuwa kiwanja unacho millioni 20 mbona unahamia kwenye nyumba lakini finishing hutamaliza. Angalia mgawanyo wa gharama ( i assume uko dar es salaam na nyumba unayojenga ni ya mtu anayejenga nyumba yake ya kwanza):
  1. matofali 5,000 @700=tzs3,500,000
  2. mafundi (kujenga toka msingi mpaka kuezeka)=4,000,000/=
  3. cement mifuko 150 @15,000=2,250,000/=
  4. mbao zote tzs4,000,000/=
  5. bati 60 @ 15,000=900,000/=
  6. fundi umeme na vifaa vyake=5,000,000/=
  7. finishing (madirisha na milango)=5,000,000/=
  8. finishing (plastering + ceiling works)=5,000,000/=

bravoooooooooooooooo
 
Mimi yangu japo nilijenga mwaka 2004 na bado najenga sidhani kama ilifika hiyo mil 20,, kwanza si lazima msingi uwe imara sana yaani wa miaka 100 kwa sisi akina yakhe hulaza matofali tu ya nchi sita na safari ya kupandisha ukuta kwa tofali ya inch 5 huanza .. madirisha ya pale manzese bei rahisi tu mil 20mnaingia ndani then namalizia taratibu...
 
Jestina:

Ni kitambo sasa na watu wengi wameshakujibu. Nami napenda kukupa moyo. Kwa muhibu wa jedwali langu la kukadiria gharama za ujenzi, Shilingi milioni 20 zinaweza kufanya kazi kubwa. Kama umeshajenga msingi, unaweza kumaliza kujenga nyumba nzuri tu. Aidha nashauri ujenge msingi mzuri na imara halafu ujipange tena.

Jedwali hili nimelitolea maelezo marefu hapa: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-vyumba-vitatu-na-sebule-3.html#post11163200

Huko nimeweka mfano kamili ukiwa na ramani na jedwali la makadirio ya ujenzi wa nyumba ya vyumba vitatu vya kulala, sebule na jiko na mabafu matatu. Unachotakiwa ni kubadili takwimu chache tu** kwenye jedwali la MS Excel kwa kulingana na ramani ya nyumba yako.

**(urefu wa kuta zote, upana na urefu wa madirisha na milango yote, eneo la nyumba yote)



Mil 20/inajenga nyumba ya vyumba 4tena safi kabisa/ unaweza kujenga nyumba mbili za vyumba vitatu kila moja tena safi.../inaweza kujenga nyumba ta vyumba 3,sitting room,car park,geti, alluminium,gypsum full/nimejenga mimi millioni 20 kibongo/bongo kubwa sana mkuu mtu asikudanganye labda mwizi huyoo....lati piga simu hapa tuzungumzee/0657 8/ 0657 740 797............
Hii namba ipo hewani ....
 
Karibuni mkoani tabora .
Kiwanja 360000
mchanga trip 30000
fudi kujenga nyumba ya vyumba 6 sh300000
kufyatua tofali@200
cement 18000
nilipata 2 milion..
nimejenga msingi na nina tofali 1200 za block
 
Last edited by a moderator:
Naona watu hawako realistic! Hizo 20ml zinaweza kutosha au zisitoshe kulingana na mahitaji ya mhusika. Kusema tu nyumba ya vyumba 4 ni maelezo yasiyotosheleza. Jestina sema unataka nyumba ya namna gani achilia idadi ya vyumba. Mfano; Aina ya materials [madirisha hapo kuna aluminum au mbao; hata aluminium zina aina hali kadhalika na mbao zina aina; aina ya mbao utakazotumia kutengeneza kenchi pamoja na milango; kuna vifaa vya finishing; yawezekana unahitaji floor tiles na za namna gani; kuezeka zipo roofing materials za kila namna na gharama tofauti. Sema tu Jestina kwani wanaosema inatosha au haitoshi bado hawajakupa mwanga kwa sababu nawewe maelezo yako hayajajitosheleza. Ukweli fedha hizo zinaweza kutosha pale tu ukihitaji bora nyumba siyo nyumba bora! Na hapo lazima usimamie na ukabe mpaka vivuli vya mafundi, vibarua na wauzaji na wasafirishaji wa materials. Asanteni sana
 
Nguruwe gani wanauzwa elfu kumi

Labda mkuu wale kama vifaranga vya bata!? Kwa hawa ninaowafahamu Mimi na Wewe hatujawahi kuwaona kwa bei hiyo!! Kisungura tu chenyewe huwezi kupata kwa bei hiyo seuse kitimoto Mtoto??
 
Thanks wadau wote mliochangia,niko juu ya mawe kwa sasa lol,nitaupitia huu uzi tena nikiwa nazo,ngoja nijipange......Merry Christmas everyone...cheers.
 
Karibuni mkoani tabora .
Kiwanja 360000
mchanga trip 30000
fudi kujenga nyumba ya vyumba 6 sh300000
kufyatua tofali@2000
cement 18000
nilipata 2 milion..
nimejenga msingi na nina tofali 1200 za block

niko tabora na sijawahi kukutana na hivyo viwanja vya laki tatu na sitini elfu.. nipe mchongo mkuu nami nipate
 
Last edited by a moderator:
nakushauri nunua nyumba ,zipo mpaka m18 ukishapata nyumba utaiboresha unavyo penda

 
Kwa kuwa kiwanja unacho millioni 20 mbona unahamia kwenye nyumba lakini finishing hutamaliza. Angalia mgawanyo wa gharama ( I assume uko Dar es Salaam na nyumba unayojenga ni ya mtu anayejenga nyumba yake ya kwanza):
  1. Matofali 5,000 @700=TZS3,500,000
  2. Mafundi (kujenga toka msingi mpaka kuezeka)=4,000,000/=
  3. Cement mifuko 150 @15,000=2,250,000/=
  4. Mbao zote TZS4,000,000/=
  5. Bati 60 @ 15,000=900,000/=
  6. Fundi umeme na vifaa vyake=5,000,000/=
  7. Finishing (madirisha na milango)=5,000,000/=
  8. Finishing (plastering + ceiling works)=5,000,000/=

iyo ndo bei ya cement dar au umeamua kumtisha mwenzio???
 
Back
Top Bottom