Naweza kujenga nyumba kwa TZS Milioni 20?


Maliwato vipi au ndio akagonge kwa jirani?
 

Mbona mwasahau maliwato jamani?

 
Mi sidhani kama 20M itatosha kujenga hiyo nyumba ya vyumba4, vifaa vya ujenzi vinapanda kila cku especially nondo na cement. Ni bora akatafuta ramani aende nayo kwa fundi ampe estimates. Je kiwanja chake kiko wapi?ni flat?kama kiwanja kiko sehemu mbaya msingi tu utakuwa zaidi ya 10M.
 
jamani siwezi kujenga nyumba ya vyumba vinne hapo dar kwa milioni 20????niambieni kama siwezi kabla sijaipoteza hii pesa...


thanks,

Hizo zinatosha msingi tu na kupandisha kozi 6
jenga nyumba simple vyumba 3 ujihifadhi
 
OK,
MIMI KAMA MIMI SIJAYATUMIA KWENYE SHUGHULI ZANGU
BUT WATU NINAO DEAL NAO WANAYATUMIA KILA SIKU....
KWA HIYO NIKIPATA DATA KAMILI NITAKUTUMIA..
not neccessarily nifanye mimi hiyo bussiness...

Yanafaa kwa ujenzi Ghorofa?
 
kwa hesabu hii hapa chini kwa haraka haraka anatakiwa aongeze mil 10 zaidi.

 
kiwanja ninacho,nilitaka kujua gharama za ujenzi....thanks..
Millioni Ishirini mkuu haitoshi, labda uniazime hiyo ili niitumie kujenga Fence ya nyumba yangu ili ukiwa tayari kujenga nikurudishie maana kiasi hicho kinatosha kujenga Foundation imara
 
mwone comarederire akupe ramani, kwa maoni yangu jenga ya vutmba vitatu inatosha kwa hiyo hela yako
kwa hela hiyo unaweza kuezeka na madirisha ukaweka nondo na nyavu baadae ukishahamia utafanya finsihing ukabadili aluminium nk
usikate tamaa jenga fasta nunua tofali vibrated tafuta fundi unaemwamini na fanya savei ujue bezi za mafundi na amduka yanaoyouza vifaa
 
jamani siwezi kujenga nyumba ya vyumba vinne hapo dar kwa milioni 20????niambieni kama siwezi kabla sijaipoteza hii pesa...


thanks,

Gharama za ujenzi zinategema vitu vingi. Ili tukusaidie kuona kama hiyo pesa inatosha au haitoshi, yupatie taarifa zifuatazo:

1. Unataka kujenga nyumba ya ukubwa gani (vyumba vingapi vya kulala+sebule+jiko+maliwato)
2. Hiyo nyumba unataka kuijenga maeneo gani hapo Dar es salaam (Kuna maeneo yenye udongo wa mfinyanzi ambayo gharama za ujenzi zinakuwa kubwa kutokana na reinforcements kwenye msingi na kuta ili nyumba isipasuke, tofauti na maeneo kama ya Ukonga ambako ni mchanga mtupu)

Pamoja na hayo, milioni 20 hiyo pesa inatosha tu kujenga nyumba ya kawaida ya chumba kimoja cha kulala + sebule ya kawaida+choo kimoja cha ndani. Kama ni nyumba standard ya vyumba vitatu vya kulala+sebule+jiko+maliwato, hiyo pesa inatosha kujenga msingi peke yake, na labda kunyanyua level tatu za ukuta.

Mahitaji yako ni muhimu ili upate kujua makisio halisi ya gharama za ujenzi.
 
Mkuu hapo namba5, na 7 hivi hizo bati unazoziongelea kwa laki9 ni zipi au madirisha na mirango yepi? Mi binafsi nimeupitia mchakato huo na kwa nyumba ya vyumba vi4 labda twaweza kutofautiana size ya madirisha lakini Magrili zilinitoka M3.4 na Aluminiums M4.3 Total M7.7 na upande wa bati nilitumia zile za versatile bati tuu niliwaachia ALAF kiasi cha M5.2 hapo hujazungumzia misumali wala mbao. Nadhani angeweka wazi nyumba ya aina gani
 

wewe kwa uzoefu wako
nyumba ya kawaida ina cost kiasi gani????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…