Naweza kuthibitisha uhalisia wa VISA niliyotumiwa?

Naweza kuthibitisha uhalisia wa VISA niliyotumiwa?

Ni kweli hao majamaa wa Lagos hawafai, japo nimeona nisikurupuke kwanza, niulizie uhalisia naona sasa nimpotezee tu kabla sijalizwa
Huyo Jamaa ni Mjanja sana, Quebec ndo Jimbo pekee Canada ambapo Lugha rasmi ni Kifaransa! Ulivyosema alikutumia Documents zikiwa kwa Lugha ya Kifaransa, nikasema YES...!

Miaka 3 nyuma ilikua kidogo niende Quebec, nina rafiki pale, nilishaanza kujifunza mpaka Kifaransa, coz kwa aina ya Visa ambayo nilikua nataka, ningefanyiwa Interview na Ubalozi kama angalau namudu hata kujielezea kwa Kifaransa, sema safari yenyewe ikaingia Mdudu!

Naona Spirit yako, mimi nna uzoefu na mambo ya safari, ngoja nikupe idea....!

Zipo baadhi ya Nchi ambazo Zinaweza ku issue Visa yako huko huko kwenye hiyo nchi, Canada sio Moja wapo, kwa Canada kama una mwenyeji, yeye anachoweza kusaidia ni kukutumia barua ya Invitation, ambapo anakua amejifunga kukuhudumia wewe kipindi chote ukiwa huko, hasa kwa Visiting Visa, labda kukugharamia ticket ya go and return, na vitu vingine, hiyo barua ndo unaweza ku attach na Documents zako kwenda Ubalozini wewe mwenyewe kuomba Visa!

Ukiacha mipango yako ya kuomba ufadhiri wa masomo, tafuta Marafiki wa kizungu, tokea hapo hapo Quebec, tengeneza urafiki bila kuonyesha lengo lako, urafiki ukikolea, anza kuchomekea kuhusu Dhamira yako, mwambie rafiki yako, huitaji yeye akutumie pesa wala nini, unachoomba na akutumie tu mwaliko, na kwamba kuhusu ticket ya Ndege utagharamika mwenyewe, sidhani kama ticket ya ndege itakushinda, ukiweka nia, ndani ya miezi 3 ushapata rafiki tayari....!
Asante sana kaka [emoji120] ninalifanyia kazi hili
Si lazima kuhangaikia Visa kubwa kubwa kama Resident Visa n.k....!

Hata ukipata Visiting Visa, kimbia haraka, uta renew mbele kwa mbele, na kutimiza ndoto zako.
 
Habari ya wakati huu, wakuu?

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27, na ni ndoto zangu kwenda nchi ya Canada au ughaibuni popote tofauti na bara la Asia kusoma na kutafuta maisha. Nina shahada ya sheria, lakini hata hela ya kwenda pale Law School ni tatizo. Kama kijana nisiye na manung'uniko na kulaumu mzazi kutoniendeleza, nimefanya jitihada kadhaa mpaka sasa, kuomba scholarship na najinoa pia lugha kwa ajili ya mitihani ya IELTS.

Lakini katika mizunguko yangu, kuna mzungu mmoja ambaye hatufahamiani aliniuliza maswali kadhaa, na kwa kuwa anuani yake inaonesha yupo Canada, Jimbo la Quebec, nilimuomba kama kuna namna naweza kwenda nchi yao. Akasema ipo, akanitumia fomu ya VISA ambayo ilikuwa kwa lugha ya Kifaransa. Nikatafuta watu, nikawalipa wakanisaidia kuijaza.

Baadaye, akaniambia nitume hela kwenda huko kwao kwa ajili ya kuthibitisha taarifa zangu, hapo ni baada ya kupokea barua pepe kadhaa zinazoonesha kwamba taarifa zangu zimepokelewa. Nikaamua kwanza elimu yangu inisaidie, maana kusikia cha kike kuingia ni rahisi sana.

Nikadelay kulipia kiasi hicho cha shilingi laki mbili na hamsini, nikamuambia sina, labda next round. Lakini amekuwa mtu anayenisisitiza kuwa ameomba faili langu lihifadhiwe na wamekubali. Nifatilie passport, NIDA, na ripoti ya matibabu, halafu nilipie na pesa.

Kwa kuwa sio mtu tunayefahamiana zaidi ya mitandaoni, naingiwa mashaka, na hili linanileta jinamizi. Ninaomba kujua jinsi ya kuthibitisha taarifa zangu kama kweli zipo Canada. Kwa mwenye ujuzi, naomba anisaidie.
Wee jamaa ni bonge ya nangaa, utafanyaje maombi ya visa ya nchi husika wakati wewe huna pasipoti? Hizo taarifa zako wanazitoa wapi? Halafu unanga wako mwengine hata kitambulisho cha NiDa huna sasa hiyo pasipoti unaipata vp?
 
Hao ni matapeli mi mwenyewe nimeishia apo apo kwenye kulipia pesa tena kwa Bitcoin [emoji28]
 
Habari ya wakati huu, wakuu?

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27, na ni ndoto zangu kwenda nchi ya Canada au ughaibuni popote tofauti na bara la Asia kusoma na kutafuta maisha. Nina shahada ya sheria, lakini hata hela ya kwenda pale Law School ni tatizo. Kama kijana nisiye na manung'uniko na kulaumu mzazi kutoniendeleza, nimefanya jitihada kadhaa mpaka sasa, kuomba scholarship na najinoa pia lugha kwa ajili ya mitihani ya IELTS.

Lakini katika mizunguko yangu, kuna mzungu mmoja ambaye hatufahamiani aliniuliza maswali kadhaa, na kwa kuwa anuani yake inaonesha yupo Canada, Jimbo la Quebec, nilimuomba kama kuna namna naweza kwenda nchi yao. Akasema ipo, akanitumia fomu ya VISA ambayo ilikuwa kwa lugha ya Kifaransa. Nikatafuta watu, nikawalipa wakanisaidia kuijaza.

Baadaye, akaniambia nitume hela kwenda huko kwao kwa ajili ya kuthibitisha taarifa zangu, hapo ni baada ya kupokea barua pepe kadhaa zinazoonesha kwamba taarifa zangu zimepokelewa. Nikaamua kwanza elimu yangu inisaidie, maana kusikia cha kike kuingia ni rahisi sana.

Nikadelay kulipia kiasi hicho cha shilingi laki mbili na hamsini, nikamuambia sina, labda next round. Lakini amekuwa mtu anayenisisitiza kuwa ameomba faili langu lihifadhiwe na wamekubali. Nifatilie passport, NIDA, na ripoti ya matibabu, halafu nilipie na pesa.

Kwa kuwa sio mtu tunayefahamiana zaidi ya mitandaoni, naingiwa mashaka, na hili linanileta jinamizi. Ninaomba kujua jinsi ya kuthibitisha taarifa zangu kama kweli zipo Canada. Kwa mwenye ujuzi, naomba anisaidie.
Chukua hiyo fomu nenda nayo ubalozini
 
Wee jamaa ni bonge ya nangaa, utafanyaje maombi ya visa ya nchi husika wakati wewe huna pasipoti? Hizo taarifa zako wanazitoa wapi? Halafu unanga wako mwengine hata kitambulisho cha NiDa huna sasa hiyo pasipoti unaipata vp?
Nashukuru, ila Kwa muda aliosema nivitafute hivyo vitu nimepata tayari hiyo NIDA na Passport, nangaa Mimi!
 
Back
Top Bottom