Naweza vipi kuishi Pasina kuyatilia sana Maanani haya Maisha?

Naweza vipi kuishi Pasina kuyatilia sana Maanani haya Maisha?

Ishi kama utakufa kesho, hii itakufanya uishi kwa hofu ya MUNGU na utafanya ibada zaidi. Pia ishi kama hautakufa hii itakufanya ufanye bidii kujijenga kiuchumi zaidi.
Kumbuka kusambaza furaha ndani ya familia yako na jamii iliyo karibu nawe, usisahau kujipa furaha mwenyewe.
sawa, ila sasa hapo kwenye kusambaza furaha ndio changamoto. Furaha ni tunda la Roho Mtakatifu. huzaliwa kutoka ndani ya mtu. (moyoni).

kumpa mtu furaha, haiwezekani. ni ngumu sana kumridhisha mtu mwingine, haiwezekani.

YESU KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI
 
Ivi Umewahi kufikiria hili?

Katika miaka mia ijayo, mwaka 2124, sisi sote hatutakawapo hata jamaa na marafiki zetu pia.

Watu wasiojulikana wataishi katika nyumba zetu ambazo tumejenga kwa jitihada kubwa na kwa Majaribu mengi. Watakuwa na vitu vyote tulivyo navyo au Vingine kuvitupa majalalani.

Hata gari, ambalo tumetumia Gharama kubwa, litakuwa mahala fulani kwenye dampo.

Wazawa wetu hawatatukumbuka sisi, na wachache pekee watajua kama tulikwepo.

Ni nani kati yetu anayemjua baba wa Babu wa babu yake?
View attachment 2868732

Baada ya kifo, watatukumbuka kwa miaka michache zaidi, kisha picha zetu zitahifadhiwa kwenye shelf za kabati za Vitabu.

Miaka michache baadaye, picha zetu na matendo zitasahaulika. Hatutakuwa tena katika kumbukumbu za yeyote.

Kama siku moja ungekaa kufikiria hili , unaweza kuelewa jinsi isivyokuwa na maana kutembea na kuhangaika kwa muda mrefu kwa nguvu kubwa .

Tukifikiri na kuelewa kuwa sisi ni kidoti tu katika historia ya binadamu, Tutaiacha dunia au ulimwengu kama ulivyo , Tutaishi Maisha yetu kwa jinsi ya utofauti zaidi

HUWENDA BADO MNA MASWALI MENGI KWANINI NAANDIKA HAYA

Wakuu ni kwamba leo imenichukua takribani siku nzima ndani ya chumba changu kukaa pasina kutoka nje na pasina kula, nikiwaza na kujaribu kutafuta hasa maana na dhima kuu ya haya maisha Yangu.

Ni hivi wadau, Binafsi nimetokea kwenye Familia yenye maisha Duni kidogo, na kwa kiasi hakuna Yeyote ndani ya Familia au koo kwa ujumla , ambae naweza kujivunia kapiga hatua tofauti ya kimaendeleo.

Binafsi ni wa kwanza kuzaliwa katika familia yangu, Na kipekee nimebahatika kusoma kwa Shida sana,

Wazazi wangu wamepambana sana, Mama yangu kwa kuuza Vitumbua na Maandazi na pia akishilikiana na Baba yangu kwenye kilimo cha Jembe la mkono.

Nachoweza kusema Wazazi waliwekeza kwangu, wakiamini mimi kama mzawa wa kwanza nitafanya kitu na kwa wadogo zangu.

Mara kadhaa nilikua nikisikia Mama akisema "Unajua Babako jana usiku kucha hajalala alikua amekaa tu kitandani akifikiri kwa jinsi gani atakulipia ada ya shule "

Au mara nyingine pia utasikia Mama akisema Unajua siku fulani tulivyokutumia ile hela ya matumizi , tulibaki mikono mitupu kabisa pasina chochote na wadogo zako, na Mara nyingine pia walikosa hata chakula

Na nukuu maneno ya mama
"Mwanangu najua sipaswi kusema haya yote kwako na Baba yako pia hapendi nizungumze haya yote kwako, ila Ukumbuke mwanangu Maisha yetu na ya wadogo zako, yako kwenye misingi yako, Katika kila unalolifanya Kumbuka tuko nyuma yako Mwanangu, kwa Gharama yoyote utasoma.

Hujawahi kutuona mimi au Babako tukienda Kulewa pombe au starehe zozote. Mawazo yetu yote ni kwako mwanangu. Mchana na Kila ifikapo usiku tunakuombea Mwanangu na wewe jiombee daima,

Kuanguka ni sehemu ya maisha ila Chunga usijidondoshe mwenyewe tupo nyuma yako mwanangu"

Haya maneno ya Mama siku zote hayaachi kujiludia kwenye fikra zangu na mara zote yakinijia najihisi machozi .

Kwakua ni dhahiri niliona Juhudi za wazazi wangu. Asubuhi hadi jioni Shambani, Mvua na jua vyao.

Nimefanikiwa kumaliza chuo miaka takribani kadhaa iliyopita, bado sijaajiliwa licha ya kutembeza bahasha isivyokua kawaida,

Kwenye makundi ya Whatsapp nashuhudia shuhuda za wenzangu niliosoma nao jinsi wakielezea walivyopata kazi kwenye kampuni fulani au serikalini, lakini mimi milango bado ni migumu.

nimeenda nje ya boksi pia kwa kuweka kisomo changu pembeni na kuingia shambani na kuzamia huko vilivyo na kwa nguvu zote, lakini shughuli bado ni tete na mtaji ni issue nyingine pasua kichwa.

Toka nikiwa mdogo nimeona na nimefunzwa na Wazazi, katika kila ninalolifanya, na katika kila nyakati yani shida, raha , Njaa au Shibe MUNGU kwanza(nisiache kuomba)
Lakini bado maombi yangu hayazai matunda. Kadili mda uendavyo najiona kukosa nguvu ya kuomba tena😢


Wazazi nawaona wakizidi kuchoka na kuzeeka ilihali bado ile ndoto yao bado sijaitimiza.

Kwakweli natumia mda mwingi kuwaza hasa majira ya usiku pasina kupata usingizi hali ambayo sasa inanipelekea kupata maradhi ya presha na Vidonda vya Tumbo.

Hii hali ndio iliyopelekea leo nijifungie ndani na kutathimini Nilipotoka na mwafaka mzima wa maisha yangu.

Ni ivi wadau naenda kuhitimisha ;

Kama nilivyotangulia awali kwa hoja ya jinsi nilivyong'amua mzunguko wa mwanadamu ni mfupi sana na hupita kama upepo,

Sasa kuna maana gani kuwa na mfululizo wa nyakati za majonzi, Huzuni na misongo ya mawazo ambayo ni chanzo cha maradhi kwangu ilihali nafukuzia upepo na maisha haya ni mpito na mwisho kila kitu na kila historia itaenda kufutika na kusahaulika kabisa

Ni hivi;
Kwa huu mda sasa nitafurahia matembezi ambayo kamwe sikupata muda kabla.

Na haswa nataka nitumie nyakati hizi zinazohesabika na ambazo hazikawii kuisha, kwa kuwa karibu na kujenga upendo mkubwa na familia yangu,

Kwa kushikana mikono ya faraja, kufurahia hizi nyakati bora na nzuri ambazo zitajenga kumbukumbu na kuchora alama ndani yetu kwa kina.
( Those would certainly be the most beautiful and best moments to remember and imprinted deep within ourselves. )

Mapambano ya utafutaji yataendelea( With no regrets). Nitakalopata nitashukuru, nitakalopoteza nitaliacha liende pasina majuto, na nitalokosa sitaki liniumizi (no much expectation)

HUU MDA NITATUMIA KUISHI NA KU ENJOY HIZI NYAKATI FUPI NILIZONAZO NA NDUGU,JAMAA NA MARAFIKI WAKATI WA MUNGU UKIFIKA NITAUPOKEA. Hii dunia sio yetu, tumejiegesha
Pole na Asante kwa mada fikirishi, binafsi baada ya kusoma nimejikuta nikiyatafakari maisha kwa angle nyingine. Kadri miaka inavyosonga ndivyo inavyokua ngumu kwetu kuyaishi maisha. Chuki, visasi, unafiki, tamaa, ubinafsi, majivuno vimekuwa vikiyatawala maisha ya kisasa.

Dhambi inatutafuna wanadamu bila ya sisi wenyewe kujua ni kiasi gani maisha yetu yanaathirika. Jiulize tuu nini kinaweza tokea kwa watu wa chini kiongozi anapokuwa mbinafsi, tujiulize ni athari ipi tunaipata kama jamii tunapokuwa na vijana wenye kuwaza anasa na zinaa siku nzima.

Zama hizi mtu akipata cheo ama pesa kidogo basi majivuno huibuka, wazee si wenye hekima tena. Kila mmoja anawaza namna kutimiza ndoto zake bila ya kujali kama njia inayoitumia inaweza leta athari kwa wengine. "What goes around comes back around" now days ni wangapi tunawaona machoni mwetu kuwa wamefanikiwa lakini hawana raha na maisha wanayoishi.

Mungu anatutaka kuishi kwa upendo, upendo na kumtegemea Mungu ndio njia pekee ya kuyapa thamani na maana maisha yetu apa duniani. Upendo unapotawala baina yetu majivuno, chuki, wivu, ubinafsi na tamaa hujitenga hivyo kuyapa udhati matendo yetu. Fikiria maisha yangekuwaje kama tungekuwa na jamii ambayo misingi yake imejengwa katika upendo na mshikamano.

Si jambo baya kujiwekea malengo, jambo la kuangalia ni malengo tunayojiwekea maana hayo yanaweza kuwa gereza katika maisha yetu hapa duani. Yana maana gani maisha yetu kama uwepo wetu apa duniani hautakuwa na baraka kwa wengine?
 
Ni hivi;
Kwa huu mda sasa nitafurahia matembezi ambayo kamwe sikupata muda kabla.

Na haswa nataka nitumie nyakati hizi zinazohesabika na ambazo hazikawii kuisha, kwa kuwa karibu na kujenga upendo mkubwa na familia yangu,

Kwa kushikana mikono ya faraja, kufurahia hizi nyakati bora na nzuri ambazo zitajenga kumbukumbu na kuchora alama ndani yetu kwa kina.
( Those would certainly be the most beautiful and best moments to remember and imprinted deep within ourselves. )

Mapambano ya utafutaji yataendelea( With no regrets). Nitakalopata nitashukuru, nitakalopoteza nitaliacha liende pasina majuto, na nitalokosa sitaki liniumizi (no much expectation)

HUU MDA NITATUMIA KUISHI NA KU ENJOY HIZI NYAKATI FUPI NILIZONAZO NA NDUGU,JAMAA NA MARAFIKI WAKATI WA MUNGU UKIFIKA NITAUPOKEA. Hii dunia sio yetu, tumejiegesha tu .😒
Ndugu katika yote uliyoandika ni mapito tu lakini maisha yako yapo katika kipande hicho kifupi hapo juu. Kamwe usitukuze huzuni kwani huzuni huuwa. Maandiko ya Biblia yanasema hivyo.

Mimi niliishi kwa mwaka mzima nikiwa na huzuni kubwa mno na kushindwa kulala zaidi ya masaa 3 na kweli nilijawa na hofu na kila kitu kiligeuka kuwa meaningless. Lakini nilipoweza kuacha kuweka mawazo yangu kwenye fears and failures, maisha yamekuwa na furaha hata kama bado sijapata nilichotaka matumaini ni mengi na naona kila dadili za kupata yote niliyoyapoteza.
 
Nashukuru kwa ku share mkuu, hakuna kukata tamaa na ushindi sio option ni lazima, tukaze.
 
upo uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana. Siku ukimpa Bwana
Ivi Umewahi kufikiria hili?

Katika miaka mia ijayo, mwaka 2124, sisi sote hatutakawapo hata jamaa na marafiki zetu pia.

Watu wasiojulikana wataishi katika nyumba zetu ambazo tumejenga kwa jitihada kubwa na kwa Majaribu mengi. Watakuwa na vitu vyote tulivyo navyo au Vingine kuvitupa majalalani.

Hata gari, ambalo tumetumia Gharama kubwa, litakuwa mahala fulani kwenye dampo.

Wazawa wetu hawatatukumbuka sisi, na wachache pekee watajua kama tulikwepo.

Ni nani kati yetu anayemjua baba wa Babu wa babu yake?
View attachment 2868732

Baada ya kifo, watatukumbuka kwa miaka michache zaidi, kisha picha zetu zitahifadhiwa kwenye shelf za kabati za Vitabu.

Miaka michache baadaye, picha zetu na matendo zitasahaulika. Hatutakuwa tena katika kumbukumbu za yeyote.

Kama siku moja ungekaa kufikiria hili , unaweza kuelewa jinsi isivyokuwa na maana kutembea na kuhangaika kwa muda mrefu kwa nguvu kubwa .

Tukifikiri na kuelewa kuwa sisi ni kidoti tu katika historia ya binadamu, Tutaiacha dunia au ulimwengu kama ulivyo , Tutaishi Maisha yetu kwa jinsi ya utofauti zaidi

HUWENDA BADO MNA MASWALI MENGI KWANINI NAANDIKA HAYA

Wakuu ni kwamba leo imenichukua takribani siku nzima ndani ya chumba changu kukaa pasina kutoka nje na pasina kula, nikiwaza na kujaribu kutafuta hasa maana na dhima kuu ya haya maisha Yangu.

Ni hivi wadau, Binafsi nimetokea kwenye Familia yenye maisha Duni kidogo, na kwa kiasi hakuna Yeyote ndani ya Familia au koo kwa ujumla , ambae naweza kujivunia kapiga hatua tofauti ya kimaendeleo.

Binafsi ni wa kwanza kuzaliwa katika familia yangu, Na kipekee nimebahatika kusoma kwa Shida sana,

Wazazi wangu wamepambana sana, Mama yangu kwa kuuza Vitumbua na Maandazi na pia akishilikiana na Baba yangu kwenye kilimo cha Jembe la mkono.

Nachoweza kusema Wazazi waliwekeza kwangu, wakiamini mimi kama mzawa wa kwanza nitafanya kitu na kwa wadogo zangu.

Mara kadhaa nilikua nikisikia Mama akisema "Unajua Babako jana usiku kucha hajalala alikua amekaa tu kitandani akifikiri kwa jinsi gani atakulipia ada ya shule "

Au mara nyingine pia utasikia Mama akisema Unajua siku fulani tulivyokutumia ile hela ya matumizi , tulibaki mikono mitupu kabisa pasina chochote na wadogo zako, na Mara nyingine pia walikosa hata chakula

Na nukuu maneno ya mama
"Mwanangu najua sipaswi kusema haya yote kwako na Baba yako pia hapendi nizungumze haya yote kwako, ila Ukumbuke mwanangu Maisha yetu na ya wadogo zako, yako kwenye misingi yako, Katika kila unalolifanya Kumbuka tuko nyuma yako Mwanangu, kwa Gharama yoyote utasoma.

Hujawahi kutuona mimi au Babako tukienda Kulewa pombe au starehe zozote. Mawazo yetu yote ni kwako mwanangu. Mchana na Kila ifikapo usiku tunakuombea Mwanangu na wewe jiombee daima,

Kuanguka ni sehemu ya maisha ila Chunga usijidondoshe mwenyewe tupo nyuma yako mwanangu"

Haya maneno ya Mama siku zote hayaachi kujiludia kwenye fikra zangu na mara zote yakinijia najihisi machozi .

Kwakua ni dhahiri niliona Juhudi za wazazi wangu. Asubuhi hadi jioni Shambani, Mvua na jua vyao.

Nimefanikiwa kumaliza chuo miaka takribani kadhaa iliyopita, bado sijaajiliwa licha ya kutembeza bahasha isivyokua kawaida,

Kwenye makundi ya Whatsapp nashuhudia shuhuda za wenzangu niliosoma nao jinsi wakielezea walivyopata kazi kwenye kampuni fulani au serikalini, lakini mimi milango bado ni migumu.

nimeenda nje ya boksi pia kwa kuweka kisomo changu pembeni na kuingia shambani na kuzamia huko vilivyo na kwa nguvu zote, lakini shughuli bado ni tete na mtaji ni issue nyingine pasua kichwa.

Toka nikiwa mdogo nimeona na nimefunzwa na Wazazi, katika kila ninalolifanya, na katika kila nyakati yani shida, raha , Njaa au Shibe MUNGU kwanza(nisiache kuomba)
Lakini bado maombi yangu hayazai matunda. Kadili mda uendavyo najiona kukosa nguvu ya kuomba tena😢


Wazazi nawaona wakizidi kuchoka na kuzeeka ilihali bado ile ndoto yao bado sijaitimiza.

Kwakweli natumia mda mwingi kuwaza hasa majira ya usiku pasina kupata usingizi hali ambayo sasa inanipelekea kupata maradhi ya presha na Vidonda vya Tumbo.

Hii hali ndio iliyopelekea leo nijifungie ndani na kutathimini Nilipotoka na mwafaka mzima wa maisha yangu.

Ni ivi wadau naenda kuhitimisha ;

Kama nilivyotangulia awali kwa hoja ya jinsi nilivyong'amua mzunguko wa mwanadamu ni mfupi sana na hupita kama upepo,

Sasa kuna maana gani kuwa na mfululizo wa nyakati za majonzi, Huzuni na misongo ya mawazo ambayo ni chanzo cha maradhi kwangu ilihali nafukuzia upepo na maisha haya ni mpito na mwisho kila kitu na kila historia itaenda kufutika na kusahaulika kabisa

Ni hivi;
Kwa huu mda sasa nitafurahia matembezi ambayo kamwe sikupata muda kabla.

Na haswa nataka nitumie nyakati hizi zinazohesabika na ambazo hazikawii kuisha, kwa kuwa karibu na kujenga upendo mkubwa na familia yangu,

Kwa kushikana mikono ya faraja, kufurahia hizi nyakati bora na nzuri ambazo zitajenga kumbukumbu na kuchora alama ndani yetu kwa kina.
( Those would certainly be the most beautiful and best moments to remember and imprinted deep within ourselves. )

Mapambano ya utafutaji yataendelea( With no regrets). Nitakalopata nitashukuru, nitakalopoteza nitaliacha liende pasina majuto, na nitalokosa sitaki liniumizi (no much expectation)

HUU MDA NITATUMIA KUISHI NA KU ENJOY HIZI NYAKATI FUPI NILIZONAZO NA NDUGU,JAMAA NA MARAFIKI WAKATI WA MUNGU UKIFIKA NITAUPOKEA. Hii dunia sio yetu, tumejiegesha tu .😒
[/

upo uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana, siku ukimpa Bwana Yesu maisha yako utabaini kuwa wewe ni kiumbe wa kiroho ambaye huna ukomo wa maisha.
 
Back
Top Bottom