Nawezaje kuachana na mwenza wa miaka mingi tuliyezaa watoto 5 pamoja?

Nawezaje kuachana na mwenza wa miaka mingi tuliyezaa watoto 5 pamoja?

Na tunampa matunzo ya maana sio hizi habari za laki moja kwa week. Ni zaidi ya Mil 2.5 kwa mwezi na yuko kijijini. Kawekewa hata na mfanya kazi wa ndani. Ni yeye tu akituona tunavyo mtendea wema aanza kulia kwa kukumbuka makosa yake ya ujanani... fainali uzeeni kwa kweli.
Maskini Nafsi inamsuta. Hata hizo pesa mnazompa hana amani nazo😅😅
 
Hatumpi kisago wala nini...ila kiukweli ameacha au na kutengezza makovu ya kudumu katika mioyo yetu watoto wake kwa kitendo chake kile cha kutukimbia...

Ni yeye tu anakumbuka ule msemo wa mbegu ya haladari kwenye mafundisho ya biblia. Dingi alikuwa mseminari haswa ila kuna kisa kimoja kilimponza huko na akaachana kabisa na habari za kanisani. Hata Hata mimi niklikuwa mseminari sana, ila nikaambiwa utakuja kuwa kama baba yako, na nikapigwa chini kuendelea na habari za upadri. ni stori ndefu sana ndugu yangu, nimeadhibiwa sana kwa makosa ya mzee wangu na hili la kuadhibiwa haya yeye analijua. siwezi sema haya mambo humu maana yapo deep sana na ni ya familia.

Nili comment tu kumpa onyo mtoa mada kama yupo tayari watoto wake waadhibike au waadhibiwe kwa makosa ya wazazi wao... mimi ni living proof wa hili ambo.

Mama alikuwa hohehahe- primary school teach watoto 11 na akastaafu kwa lazima ya ugonjwa mwaka 1985 mimi nikiwa na miaka 9. Nikaanza la kwanza nikiwa 11 yrs kwa sababu mama hakumudu elfu 7 ya wakti huo, ingawaje wakati mwingine serikali muda huo ilikuwa inatupa madaftari bure huko primary school.
Baba akakimbia familia- -ugonjwa wa mama na hali ngumu ya Maisha- kufyatua wengi kunahusika.
watoto tukaishi kama kuku wa kienyeji- free range hadi tumetoboa sote na maisha ni safi.
baada ya kuona tumetoboa ndio sasa mzee anarudi kuomba msamaha- ni mtihani mkubwa sana.

Ilifika mahala sisi watoto tukawa tunajadiri namna ya kunywa sumu tuondokane na mateso ya dunia.
chakula kilikuwa taabu sana- chai ya rangi iliyotengezwa kwa mtama ilikuwa ya kugombania
wali ulikuwa unapikwa xmas pekee bila maharagwe au nyama na kwa jinsi tulivyo kuwa wengi ilikuwa ni sagura sagura ya uhakika, tonge moja tu na unaridhika.

haya mambo yasikie tu kwa wengine ndugu yangu. Niki- reflect nilipotokea, nilipo na ninapo jwenda , nazidi kumtukuza Mungu Muumba, maana alinipitisha katika yote na bila yeye, sijui kama ningekuwa hapa kuandika habari hizi. Nahisi hata unyonge kufikiria tu nilipo toka, ila kwa sasa, Namshukuru Mungu sana, na hawajahi kunitupa kwa kweli katika shida zangu zote - achana na habari hizi za dingi. Mungu yupo na ni wa kweli. Nimemuona katika maisha yangu ya utotoni, ujanani na sasa uzeeni nikikaribia kustaafu kazi.

Ni hayo. Pokea litakalo kufaa.
A Living Miracle😅😅
 
Huo ni Ukatiri kumtia mtu mimba ndio kwanza ametoka operation hata miezi sita bado.

Ni matokeo ya watu kuwaza sana ngono kuliko mambo mengine.

Unachakata mtu kila siku kila wiki mwaka hadi mwaka huo ni ukatiri hakuna mapenzi hapo.

Operation ziko sasa, zamani watu walikuwa wanazaa kawaida tu vizuri.. sasa hivi njaa za madaktari, aina za vyakula na uzungu unasabisha wanawake kupenda kuzaa kwa operation.
 
Operation ziko sasa, zamani watu walikuwa wanazaa kawaida tu vizuri.. sasa hivi njaa za madaktari, aina za vyakula na uzungu unasabisha wanawake kupenda kuzaa kwa operation.
Kaka usitukane Mamba kabla hujavuka mto ......unasema ni njaa za Madaktari?😅😅😅
 
Daah haya maisha bwana.......umemchakata mwenzio hadi umefikia watoto 5.

Ndio kusema hadi unafikisha uzao wa tano kulikuwa hakuna mapenzi?

Bado naamini kuna sababu nyingi za kuwaunganisha na kuendelea kuliko sababu kiduchu za kuwatenganisha.
Hata mi nashangaa five children si mmeshakuwa wazee.
 
Tayari uhusiano huu umezalisha watoto watano.

Wakuu tupeane maujanja ya namna ya kutoka kwenye mahusiano haya na matokeo yake (yote mazuri na mabaya) ya kuachana huko.

**Sitaki ushauri wa kurudiana maana maamuzi ya kuachana tayari yameshafanyika.
OK. Very simple. Mpe haki yake.
Halafu ukitoka hapo nje, ujue Ibilisi yupo hapo anakusubiri kwa hamu kubwa sana. Kila la kheri mkuu. :KEKBye:
 
Kaka usitukane Mamba kabla hujavuka mto ......unasema ni njaa za Madaktari?😅😅😅

Wakifanya operation wanapata posho zaidi. Kwa hiyo fasta tu utasikia wamemwambia watafanya upasuaji. Ndio first option, wakati mara nyingine mtu angeweza kujifungua kawaida.
 
Amani ya moyo ni muhimu sana,baba na mama waliachana wakiwa na watoto 7 including me,niliachwa na kulelewa na baba nikiwa na mwaka 1.8 na leo hii nipo,kupitia hali hii sina huruma na mwanamke atayeniletea ujinga ujinga,nikuachana na kuoa tena,hata kama nitaoa mara 100 sitajari.



Mkuu tafuta amani ya moyo wako,usiwaze juu ya watoto,ikiwa mimi nimekuwa toka kuachwa nikiwa na mwaka1.8 sasa hofu yako ni ipi? Mwambie huyo huyo mwanamke humtaki tena ikiwa una sababu kuu ya kufanya hivyo,huhitaji kujiuliza.
Maelezo yako yamejaa shida kubwa, ila bado huoni kama uko na shida iliyosababishwa na hukohuko kutengana kwa wazazi wako.
 
Km maamuzi ya kuachana mmeshafanya, si kila mtu aelekee kwake.
Na maisha yaanze upyaa, kwa kila m1 wenu.
 
Tayari uhusiano huu umezalisha watoto watano.

Wakuu tupeane maujanja ya namna ya kutoka kwenye mahusiano haya na matokeo yake (yote mazuri na mabaya) ya kuachana huko.

**Sitaki ushauri wa kurudiana maana maamuzi ya kuachana tayari yameshafanyika.
kisa kuachana ni nini
 
Hujatoa sababu za kuachana kumbukeni Watoto ndio watakaopata shida ya kukosa malezi ya Wazazi wote wawili.
 
Jijibu kwanza haya maswali kabla ya kufikia hiyo hatua;
1. Watoto watalelewa na nani?
2. Yeyote atakaekuwa na hao watoto, je watoto watapata nafasi ya malezi ya mzazi ambae hatakuwa nao kikamilifu?
.
.
Kaeni chini wawili kama mlivyokutana myamalize(sio hapo nyumbani mlipopazoea)
 
Jijibu kwanza haya maswali kabla ya kufikia hiyo hatua;
1. Watoto watalelewa na nani?
2. Yeyote atakaekuwa na hao watoto, je watoto watapata nafasi ya malezi ya mzazi ambae hatakuwa nao kikamilifu?
.
.
Kaeni chini wawili kama mlivyokutana myamalize(sio hapo nyumbani mlipopazoea)
Huyo bwana ni kama ameshajiwekea hitimisho- hapa amekuja kutuchosha tu na mambo yake. Ameshatekwa tayari bado tu kupotezwa.
 
Huyo bwana ni kama ameshajiwekea hitimisho- hapa amekuja kutuchosha tu na mambo yake. Ameshatekwa tayari bado tu kupotezwa.
Cha muhimu achanganye na ushauri wa wengine hapa then achambue ndio afanye maamuzi
 
Back
Top Bottom