Nawezaje kuishtaki kampuni ya simu?

Nawezaje kuishtaki kampuni ya simu?

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Kuna mchezo nimegundua kuwa nafanyiwa na Kampuni fulani ya simu kwa kunikata pesa zangu bila ridhaa yangu ile airtime, ukiwapigia wanasema kuwa ulijiunga na huduma hizi. Nimewalalamikia mara nyingi sana ila wameendelea kunikata tu. Kila ukiwaambia wanakuambia jitoe, najitoa lakini baada ya muda unakuta unakatwa tena.

Wasi wasi wangu ni Watanzania wangapi ambao huenda wanakatwa bila ridhaa yao na bila wao kufahamu? Maana hadi uwe makini ndio utagundua kuwa wanakukata! Nikipata ushauri mzuri na mwana sheria anayeweza kunisimamia katika hili nitashukuru sana ili haki itendeke.
 
Bila shaka hao ni tigo,

Cha msingi nenda customer centre yao, Waambie wakufute kweye huduma zote za kijinga jinga
 
Bila shaka hao ni tigo,

Cha msingi nenda customer centre yao, Waambie wakufute kweye huduma zote za kijinga jinga
Mpwa naomba nisikubali au kukataa kuwa ni Tigo au lah ila nimeshwapigia mara nyingi sana, wanachokifanya ni kwamba leo wanakutoa baada ya week unashtuka unakuta salio limepungua ukifuatailia unakuta wanakukata, unawasiliana nao tena inakua the same same story. Yaani ninachoomba hapa ni namna tu ya kuwashtaki, staki tena.
 
Ndo mchezo wao mimi voda kila nikiweka vocha wanakata sh 42..yani nimewapigia wanadai sikatwi. Natafuta muda nawaibukia alafu napiga hesabu 42 mara siku nilizokatwa
 
Ndo mchezo wao mimi voda kila nikiweka vocha wanakata sh 42..yani nimewapigia wanadai sikatwi. Natafuta muda nawaibukia alafu napiga hesabu 42 mara siku nilizokatwa
Kulikua na Uzi wa tpaul nimeutafuta sijauona alikua akielezea wizi unaofanywa na haya makampuni aiseeee. Hivi bado TCRA wako humu ndani??
 
Kuna mchezo nimegundua kuwa nafanyiwa na Kampuni fulani ya simu kwa kunikata pesa zangu bila ridhaa yangu ile airtime, ukiwapigia wanasema kuwa ulijiunga na huduma hizi. Nimewalalamikia mara nyingi sana ila wameendelea kunikata tu. Kila ukiwaambia wanakuambia jitoe, najitoa lakini baada ya muda unakuta unakatwa tena.

Wasi wasi wangu ni Watanzania wangapi ambao huenda wanakatwa bila ridhaa yao na bila wao kufahamu? Maana hadi uwe makini ndio utagundua kuwa wanakukata! Nikipata ushauri mzuri na mwana sheria anayeweza kunisimamia katika hili nitashukuru sana ili haki itendeke.
mkuu, kabla ya kuwanyoosha inabidi kwanza uende kwao physically uwaombe wakutoe kwenye huduma hiyo na ikibidi uwarekodi kwa siri kama ushahidi...kama bado wataendelea kukukata, ukipata wakili mzuri kama Tundu Lissu atawanyoosha hawatakuja kusahau.
 
Ikiwa utafungua huduma hiyo ukiwa na salio, salio lako lote litakombwa sawia! Kuna mtandao mmoja wa simu unajinadi kwamba unatoa huduma ya fesibuku bure wakati ni uongo mtupu. Ingia kwenye hiyo fesibuku uone utakavyoliwa fedha! Aidha kuna mtandao mmoja uliwahi kuwa na fesibuku ya bure siku za nyuma (kama mtakumbuka).
Kumbe huu mchezo sio wa leo wala wa Jana eeghhh, na mimi nimeambiwa hivyo hivyo
 
Back
Top Bottom