Nawezaje kumtoa pusha wa mtaani bila kutumia Polisi, sitaki dhambi ya kumfanya mtu atoke jela akiwa mzee

Nawezaje kumtoa pusha wa mtaani bila kutumia Polisi, sitaki dhambi ya kumfanya mtu atoke jela akiwa mzee

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
1641900797314.png


Mtaani kwangu kuna kijana yupo hapa kwa miezi miwili, yupo kwenye rika la miaka 24 hivi, ana frem anauza mahitaji ya nyumbani na vilevi, lakini biashara yake kuu yenye wateja wengi ni Bangi ambayo wanunuzi huvuta hapo hapo ama maeneo ya karibu, eneo sio la barabarani, huwa kuna watu wachche wanatumia hii njia.

Ni kijana mjanja mjanja, nilienda siku moja hapo kumcheki, kiukweli ana kipaji kikubwa sana cha kutengeneza urafiki, ndani ya dakika 4 tu tushazoeana na matani ya hapa na pale maana mimi pia nipo miaka 31 so ni kijana mwenzangu.

Sina tatizo na dogo ila ni hawa wavuta bangi, wengi hawana shughuli za kuwaingizia vipato, wakivuta bangi wanasizi tu, Pia bangi wanazovuta ni haya makapi ya shilingi 500 yanayouzwa karibu kila kona ya nchi, sasa hawa vijana kama hawajishughulishi na wanapenda bangi kinachofuata huwa ni wizi / utapeli, pia hatari kubwa ipo kwa ma house girl tunaowaachia nyumba zetu tukiondoka, wanaweza kurubuniwa na hawa vijana kirahisi.

Nyumba zipo 9 kwenye huu mtaa na zote zina fensi na mageti lakini kuna matukio kadhaa yamewahi kutokea watu kuibiwa nguo, tv, n.k. japo ni nadra, hatutaki yajirudie mara kwa mara.

Sasa ili kutatua matatizo hayo kabla hayajatokea mimi nimeona nishughulike haraka, ila kwa sharti moja tu, sitaki kushirikisha mkono wa sheria kwa sababu dogo anaweza kuishia mahabusu kesi yake ikasikilizwa 2040 na akienda mahakamani ni miaka 30 jela. Kinachonifanya nikwepe kutumia sheria ni hayo maisha ya Jela na Mahabusu kwa huku bongo, asikwambie mtu hizo sehemu hazifai hata kidogo, sikiaga tu flani yupo huko, sio kuzuri hata chembe.

Niliwahi kumwambia hio ishu itamuharibia life lakini dogo yeye anasema hakuna pusha asiejua hatari ya biashara anayofanya, anasema hajaingia kichwa kichwa anajua anachokifanya, kiufupi anajiamini sana lakini haiondoi uhalisia kwamba bado yupo hatarini.

Kijana ana miaka 24, haitakuwa vema mimi nihusike kwa yeye kutoka jela akiwa kamalizia ujana nyuma ya nondo.

Ni vipi nitaweza kutatua hili tatizo bila kushirikisa polisi.
 
Mwite faragha umueleze kuwa aachane na hiyo kazi ya uuzaji wa bangi aendelee na hiyo nyingine sababu itamletea matatizo,na umwambie umesikia kuna mpango mkakati wa kumkamata ili aweke ndani ikibidi afungwe.

So kwa vile ww ni rafiki yake umeamua kumueleza ili achukue hatua mapema kabla hakijamsanukia.

Ukiona haelewei somo,tafuta askari polisi umueleze kama ulivyo eleza hapa kuwa hataki afungwe ila unataka kumtisha tu aachane na hiyo kazi so aende akiwa na Uniform then amwite faragha pia amueleze kuwa wamepokea malalamiko kutoka kwa wananchi juu ya biashara yake hiyo haramu.

Hivyo anamuomba aachane nayo kabla hawajamchukulia hatua zinazostahiki.asipoelewa tena hapo mm pamoja na ww tunatakiwa kunawa mikono kama alivyofanya pilato.
 
Bangi iko poa tu ihalalishwe
Hizi bangi zetu za bongo asilimia kubwa ni kushabu, kushabu ni haya makapi makapi yanayouzwa kwa 500 tu mtaani, hizi sio bangi bali ni uchafu unaoharibu akili, sasa hawa wavutaji wa hapa mtani wengi hata hawajishugulishi kuingiza vipato, pesa ikiisha hapo na mtu ana kiu kali ya kuvuta bangi, hapo ndio mambo ya uhalifu yanaanza
 
Weka fence ya umeme kwako, hao mapusha hawatasogelea kwako.

Kifupi ni kwamba wewe imarisha ulinzi wa nyumbani kwako tuu basiii, mengine achana nayo.
Hauko serious mkuu, siku ndugu zake wanakuja mtembelea waanze kukabwa njiani na wavuta bangi
 
Mwache auze ganja! Bangi haisababishi watu kuwa waovu, ila dini ndo zimetudanganya kuwa uovu mwingi unasababishwa na bangi na pia ukichaa.

Vuta bangi kama research yako then uine kama kweli ganja husababisha hizo mambo.

Usisababishie watu matatizo, mimi nimeanza kuvuta bangi mwaka juzi, na sijutii kuvuta bange inasaidia vitu vingi na wala haishawishi kufanya jambo baya bali inakupa hali ya kutulia.

Wavuta bange ni watu wa hisia za kutulia sio machafuko.
 
Kwani bangi Ina shida gani? Mbona mi nawajua matajiri wengi tu Wana hela kuliko wewe Mara milioni, wanavuta bangi na sio wezi?

Kwanza Mimi mtu ambae hajawahi kuvuta bangi maisha yake yote, huwa namuona kama mjinga mjinga flani tu. Siku hizi hadi warembo hao unawajua na kuwaona kwenye tv wanavuta bangi, wewe unakaa unapiga vita bangi...mi nilijua unalalamika labda ni unga..
 
Kwann usimfate ukamwambia hii biashara hili eneo utapotea achana nayo? Au unaogopa atakuvutia bangi.
 
Kwani bangi Ina shida gani? Mbona mi nawajua matajiri wengi tu Wana hela kuliko wewe Mara milioni, wanavuta bangi na sio wezi?

Kwanza Mimi mtu ambae hajawahi kuvuta bangi maisha yake yote, huwa namuona kama mjinga mjinga flani tu. Siku hizi hadi warembo hao unawajua na kuwaona kwenye tv wanavuta bangi, wewe unakaa unapiga vita bangi...mi nilijua unalalamika labda ni unga..
Dawa haina shida
 
Kwani bangi Ina shida gani? Mbona mi nawajua matajiri wengi tu Wana hela kuliko wewe Mara milioni, wanavuta bangi na sio wezi?
Kuna makapi haya yanayouzwa kwa 500 karibu kila kona ya nchi haya ni kwajili ya watu wasiojua wanachovuta ama hawana pesa, hata ho kina afande sele nao na urasta wao huenda wanavuta makapi a.k.a kushabu.

Kwa mtu tajir ndio anavuta bangi, bangi anayovuta ni ile inayochambuliwa pembeni kivyake, haichanganywi na hayo makapi a jero
 
Kuna makapi haya yanayouzwa kwa 500 karibu kila kona ya nchi haya ni kwajili ya watu wasiojua wanachovuta ama hawana pesa.

Kwa mtu tajir ndio anavta bangi, hizi huwa ni kwa order unawekewa kitu chenyewe, sio uchafu huu wa 500
Sasa wewe unajuaje kuwa jamaa anachouza ni makapi wakati huvuti? Huoni kama wewe ni mnafiki tu na miongoni mwa wale watu wajinga wanaodhani kuwa mvuta bangi ni mwizi, mzembe, kichaa na aliyefeli maisha. Kwa taarifa yako marais wote wa Marekani kuanzia Clinton, Bush, Obama wamevuta bangi sana..na wameongoza taifa kubwa lenye nguvu zaidi
 
Weka fence ya umeme kwako, hao mapusha hawatasogelea kwako.

Kifupi ni kwamba wewe imarisha ulinzi wa nyumbani kwako tuu basiii, mengine achana nayo.
Ni ngumu kuishi karibu na kijiwe cha wavuta bangi kama una familia. Wavuta bangi hawazoweleki!

Tatizo la wavuta bangi wao huvuta bangi hata karibu na nyumba. Hali hii hupelekea harufu ya bangi kuingia hadi ndani hata kama una fensi.


Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Sasa wewe unajuaje kuwa jamaa anachouza ni makapi wakati huvuti? Huoni kama wewe ni mnafiki tu na miongoni mwa wale watu wajinga wanaodhani kuwa mvuta bangi ni mwizi, mzembe, kichaa na aliyefeli maisha. Kwa taarifa yako marais wote wa Marekani kuanzia Clinton, Bush, Obama wamevuta bangi sana..na wameongoza taifa kubwa lenye nguvu zaidi
Mkuu hizo bangi mimi sio mgeni....


Hivi kwa akili yako unadhani haya makapi ya jero (shilingi 500) yanafikia hata robo ya hadhi ya kitu chenyewe??

Huku kwetu kuna ardhi nzuri sana yenye rotuba yenye uwezo wa kuitesha bangi nzuri sana yenye kiwango ila hiu bado haitoshi,,, unakuta wauzaji wanawahi sana kuvuna bangi iliyo mbichi kuogopa itagundulika na kufyekwa, bangi wanaiacha ijiotee bila hata kutoa wadudu wanaoharibu maua, vifundo vilivyooza, n.k. nae pusha ni mweupe tu yeye anachojua ni kusambaza tu ilimradi iwe bangi tu hata akipewa ambayo haijakomaa ama ambayo imevunwa miezi mitatu iliyopita ananunua hivyo hivyo tu, huku kwa wateja ndio nawaonea huruma maana wanavuta uchafu wa 500 wakidanganyana wanavuta kitu chenyewe kumbe ni uchafu tu, tena wauzaji wengine wakitaka kuongeza stim kwenye mzigo wanamwagia sumu za panya, gundi, wino, n.k. matokeo yake ndio haya wengine vichwa vinauma, macho yanakuwa mekundu kuzidi kiwango cha kawaida cha bangi halisi, wengine wanakuwa vichaa kabisa.

Unaeza kusoma uzi wangu huu wa elimu kamili ya kujua kutofautisha makapi na bangi.

Kuna siku nimepita hapo kwa dogo asubuhi, niliucheki mzigo wake ni makapi yale yale tu ya jero, siwezi vuta uchafu huo, ni heri ninunue skank kitu orijino kwa elf 10 kuliko huu uchafu wa jero

 
Back
Top Bottom