Nawezaje kushtaki vyombo vya habari kwa kutumia picha yangu bila ridhaa yangu?

Trubarg

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2020
Posts
4,388
Reaction score
7,223
Kuna picha huwa zinazagaa mtandaoni na zinatumiwa Sana na vyombo vya habari bila kuziba privacy ya muhusika..mfano Ni picha iloyozagaa kwenye vyombo vya habari hasa kipindi hichi Cha sikukuu.

Picha hiyo inaonyesha mtu akipuliza kipimo Cha pombe kwenya habari iliyotolewa na jeshi la polisi kuhusu ulevi. Naomba kuelewa iwapo hujahusishwa kwenye matumizi ya picha hiyo unawezaje kudai fidia kwa watu kukuvunjia privacy yako.
 
Ko uyo ni wewe??unaonekana mlevi kbsπŸ˜€πŸ˜€
 
Tulia, Mambo Haya Hayawezekani Tanzania
Nakukumbusha, Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Alipofanya Ziara Mkoani Mwanza Hasa Gereza La Butimba
-----------------------------------------------------------------------
Mkuu Wa Usalama Gerezani Aliambiwa
Inaonekana Una Kiburi Sana Wewe, Hivi Nikinyoa Hizo Nyota Zako!! Baadaye Akahamishwa Huko.
 
Sidhani kama hawakukupata na ulevi mkuu..πŸ˜‚ but wacheki wanahabari husika waambie haupendi na hautaki.. Kama utataka kushindana nao Basi kusanya ushahidi wakutosha na ziba mipenyo yote..
 
Duh mkuu una sura mbaya, kama Meko
 
Je, wewe umepata ridhaa ya hao polisi na huyo dereva ya kupost picha yao? Kama hapana na wewe unastahili kushtakiwa.
 
Inategemea na maelezo ya hiyo picha, kama umedhalilishwa unaweza kushtaki
 
Nje ya mada;
Hivi hicho kipimo kinapima mpaka stim za marryjane?
Hicho kinapima mpaka ngono kabisa kama umefanya kinaonyesha[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Kinachokuuma nini kumkamatia mkono huyo askari au kutaka kumeza kipimo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…