Yanapelekana kama hayana akili, watu wazima hovyo. Badala ya kuboresha movie zao wanalazimisha watu kununua uchafu wao. Mbona kina diamond wanaeleweka tu na wanasonga mbele na miziki ya inauzwa na kupigwa kama kawaida? Wanashindwa kuboresha kazi zao wanatafuta umaarufu wa kijinga kwenye majukwaa ya siasa na magazeti ya udaku kisha wanategemea kazi zao zitapendwa. Kwa style hii kuliko kununua cd ya bongo movie ni heri hiyo hela kuigawa bure.
Kwanza wasanii wenyewe hawajiheshimu wanategemea kukuza kazi zao kwa skendo. Wanaiga mambo ya ulaya kisha mimi niangalie wakati kuna uwezekano wa kuangalia ulaya halisi. Wanatoa movie hazina uhalisia hawataki kuwekeza. Gharama za kutafuta umaarufu ni kubwa kuliko wanazofanya kwenye uwekezaji. Mtu movie ya masaa mawili anataka kutumia mil10 kuitoa na wakati mwanamuziki video ya dakika 4 anatumia 50 au 100 mil halafu wanategemea kupata soko kwa kuzuia masoko ya nje.
Yaani kwa akili zao wanadhani mtu uache kununua fast and furious pale kariakoo uangalia movie ya Ray au Vicent kigosi aliyesuka nywele na kuvaa hereni halafi ana act yupo ofisi kubwa ya serikali, hakuna uhalisia wowote. Yaaani hawa bongo movie ukiangalia movie zao unashindwa kuelewa ni movie au ni komedi. Nachowashauri watoe movie wasubiri kipindi cha kampeni kisha wakaoneshe huko kwenye kampeni. Walitugawa watanzania kipindi cha kampeni leo wanataka tununue movie zao kirahis.