Nayaona mabadiliko Baraza la Mawaziri

Nayaona mabadiliko Baraza la Mawaziri

Rigidity

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2024
Posts
391
Reaction score
482
Nimatumaini yangu kumekucha salama, wagonjwa na wenye changamoto ninaungana nao kuomba na kupambana ahueni ipatikane.

Aidha ninaungana na wafiwa na wale walioguswa na msiba wa mzee wetu Ali Magoma kwa udhalilishaji na mateso aliyefanyiwa na hatimaye mauti kumkuta.

Kelele zimekua nyingi hadi waziri wa mambo ya ndani bwana Masauni kuzomewa msibani. Huu ujumbe mzito alioupata unaihusu serikali wala sio Masauni.

Nimesema bwana masauni kwakua wananchi hawaoni huo uheshimiwa tena kwa namna walivyomzomea
Kwa zomeazomea ile maana yake serikali imezomewa hadharani na walioiweka.

Mambo haya ya mauaji ninayoimani kabisa kwamba hata kama waziri hajamtuma mtu lakini sijaona akifanya juhudi kupambana na watekaji na wauaji. Zaidi ya yote alipuuzia kama hakuna hali hiyo.

Zaidi ya yote ninaamini kwamba hii dhuluma ya kutolewa nafsi za watu haina Baraka kutoka kwa mh. Rais. Hivyo muda wowote kuanzia sasa mabadiliko kwenye Baraza la Mawaziri yatafanyika. Lengo nikulinda heshima ya mamlaka na mamlaka ijitetee kwamba haijatuma wahalifu kufanya hayo.
 
Mabadiliko ya baraza bila watu kufikishwa kwenye vyombo vya haki kujibu jinai zao ni kazi bure... mabadiliko yafanyike na waziri anayebadilishwa atuambie wasiojulikana ni nani na wanafanya hayo wanayofanya kwa faida ya nani!
 
Nimatumaini yangu kumekucha salama,wagonjwa na wenye changamoto ninaungana nao kuomba na kupambana ahueni ipatikane
Aidha ninaungana na wafiwa na wale walioguswa na msiba wa mzee wetu Ali Magoma kwa udhalilishaji na mateso aliyefanyiwa na hatimaye mauti kumkuta.
Kelele zimekua nyingi hadi waziri wa mambo ya ndani bwana Masauni kuzomewa msibani. Huu ujumbe mzito alioupata unaihusu serikali wala sio Masauni
Nimesema bwana masauni kwakua wananchi hawaoni huo uheshimiwa tena kwa namna walivyomzomea
Kwa zomeazomea ile maana yake serikali imezomewa hadharani na walioiweka
Mambo haya ya mauaji ninayoimani kabisa kwamba hata kama waziri hajamtuma mtu lakini sijaona akifanya juhudi kupambana na watekaji na wauaji. Zaidi ya yote alipuuzia kama hakuna hali hiyo.

Zaidi ya yote ninaamini kwamba hii dhuluma ya kutolewa nafsi za watu haina Baraka kutoka kwa mh. Rais. Hivyo muda wowote kuanzia sasa mabadiliko kwenye Baraza la Mawaziri yatafanyika. Lengo nikulinda heshima ya mamlaka na mamlaka ijitetee kwamba haijatuma wahalifu kufanya hayo
mabadiliko hayo kwiyo, yaani mama amtoe mpwa wake Thubutuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu, tumekubaliana kwamba tufe tu maana machogo nyie wa bara hamna maana kabisa
 
Back
Top Bottom