NBA 2016/2017 Season Special Thread


Asante kwa majibu yako mkuu.

Mfumo uko namna hii,

NBA ina timu 30, kila timu ina washabiki wake tufanye average ya mil 1 kwa kila timu (huu ni mfano tu),

Sasa kama timu ikiwa ni nzuri sana ina maana itakuwa inazifunga hizo timu zingine, wale washabiki mil 1 wa hiyo timu watakuwa wanafurahi sana, ila wale washabiki wengine mil 29 kwa vyovyote hawawezi kufurahi, isipokuwa kila hiyo timu nzuri itakapokuwa inacheza wataishangilia timu pinzani dhidi yake.

Msimu ulioisha GSW amezifunga timu zote kwenye regular season na kaweka rekodi ya kushinda gane 73 kati ya 82 huku Steph Curry akiwa ndo chachu ya hayo mafanikio, je unataka washabiki wa timu pinzani wafurahie?

Ni kama hata kwenye mpira, utakuta kwamba wachezaji wanaofanya vizuri ndo wanaoonekana kuchukiwa, au timu zenye kufanya vizuri zinakuwa zinaonekana kuchukiwa.

Kifupi ni kwamba, kama unanifunga, unanizidi uwezo kwa nini kwa nini nikushangilie?
 
Ahahaaaaaah...
Nimekuelewa bradha...
Ila msimu uliopita bingwa si Cavs...
Sasa mashabiki wa timu zote zilizobaki ilibidi wahamishie chuki zao kwa Cavs na Irving...
Kwasababu hao ndio MABINGWA...
Au haiko hivyo..!?
 
Ahahaaaaaah...
Nimekuelewa bradha...
Ila msimu uliopita bingwa si Cavs...
Sasa mashabiki wa timu zote zilizobaki ilibidi wahamishie chuki zao kwa Cavs na Irving...
Kwasababu hao ndio MABINGWA...
Au haiko hivyo..!?

Msimu ulianza kwa GSW warriors kushinda mechi 24 mfululizo, na hapo ndo walipoanza tambo za kwamba hakuna timu yoyote ile inayoweza kuwasimamisha.

NBA Season 2015 - 2016: Special thread

Waliendelea kuzishinda timu pinzani kwa point nyingi ngingi sana, na mpaka ile regular season inaisha walikuwa wameshinda game 73 kama nilivyokwambia awali.

Sasa walipoingia fainali na Cavs, washabiki wa zile timu zingine zilizofungwa na GSW ilibidi wawe upande wa Cavs, ndo kilichotokea sasa.

Baada ya GSW kufungwa kwa aibu (kwa kupoteza ushindi wa 3 - 1), iliwauma sana ikabidi wamsajili Kevin Durant ili aje aongeze nguvu kwenye kikosi kupambana na LeBron James. Na hii imewaongezea chuki zaidi kwa sababu wapinzani wanaona sasa GSW inatisha, kilichobaki ni kuiombea mabaya tu maana katika hali ya kawaida wanatisha.
(Ila kwa LBJ watakaa tu).

Kuna kitu kimoja ukielewe, tatizo la washabiki wengi huwa hatupendi timu zetu zisemwe vibaya, au wachezaji tunaowapenda wasemwe, ambacho ni kitu usichoweza kukiepuka kwenye michezo na ushabiki.

Humu ndani kuna watu hawataki kusikia GSW ikisemwa vibaya, au tukimsema Curry vibaya basi kinanuka humu.
 
This proves the statement 'Hopefully it still smells a little bit like champagne'. tormented LBJ Long enough not to let it go..It's a good revenge however..

Lazima iume aisee, na jamaa naona anawalipizia sasa.

Hii itaongeza ushindani hizi timu zitakapokuwa zinakutana.
 
Baada ya michael jordan kustaafu nami nikaacha ishabikia chicago bulls na kikapu kizimaaaa sasa hawa GSW wamenifanya nirudi tena shabikia kikapu na hii ndio timu yangu mpya kwa sasa
 
Gsw ni manchester United ya u.s.a curry anachukiwa kama pogba na Man U inachukiwa kama hao GSW
 
phoenix vs portland 101-101...15sec rem...........Now we all now what time it is....Lillard Time
 
Lazima iume aisee, na jamaa naona anawalipizia sasa.

Hii itaongeza ushindani hizi timu zitakapokuwa zinakutana.
haya sasa his hometown MLB Team (Cleveland Indians) wameblow 3-1 lead (WORLD SERIES) Cubs waleee wamechukua ndoo...πŸ˜€πŸ˜€
 
View attachment 428573
haya sasa his hometown MLB Team (Cleveland Indians) wameblow 3-1 lead (WORLD SERIES) Cubs waleee wamechukua ndoo...πŸ˜€πŸ˜€

DRaymond Green pia ka-tweet!

Hii inaongeza chachu ya ushindani, make sasa hivi ni vita kuu kati ya Cavs na GSW, ninaamini hata game za regular season zitakuwa high rated this time.
 
Karibuni sana George Betram na ze-dudu...GSW ndio gumzo la jiji na Steph Curry ndiye that baby-faced assassin anayetungua bila kumtazama mchawi usoni.
Ahsante sana mkuu...
Tutakuwa pamoja mwanzo mwisho...
Tena ninashukuru nimeanza kuishabikia GSW kipindi KIGUMU..!
Hapa nasubiria game yetu na OKC...
I hope Steph atampoteza Westbrook..!
 
DRaymond Green pia ka-tweet!

Hii inaongeza chachu ya ushindani, make sasa hivi ni vita kuu kati ya Cavs na GSW, ninaamini hata game za regular season zitakuwa high rated this time.
yeah 3-1 sucks...
 
Ahsante sana mkuu...
Tutakuwa pamoja mwanzo mwisho...
Tena ninashukuru nimeanza kuishabikia GSW kipindi KIGUMU..!
Hapa nasubiria game yetu na OKC...
I hope Steph atampoteza Westbrook..!

Mzee wa fungu la kukosa, we mwenyewe umeona msimu ulioisha jinsi ambavyo Cavs walivyowatanguliza mbele GSW kwa baiskeli za mbao then wakawapita shaaa, halafu eti ndo uliochagua kuwashabikia.

Subiri vipigo tu kutoka kwa mmiliki wa ligi.
 
Umeuona moto wa James Harden?

Yuko vizuri msimu huu, akiendelea hivi hivi u-MVP unamuhusu aisee, nadhani ni baada ya kuachana na Khloe ndo karudi kwenye mstari.
hakika...amekuwa ''Point Guard'' sasa....He is Running the offence like never before..Somethings happen as a blessing in disguise..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…